Dj Fetty awachana BASATA

Dj Fetty awachana BASATA

Ila mbona kuna picha za wanenguaji huwa zinasambaa wamekaa kwenye steji na hawajavaa kofuli, nanihii ziko wazi hadi utumbo unaonekana?au wale sio watz?

Mwisho wa siku ni muhimu sheria ikawa msumeno na kukata bila kuangalia sura.
 
hiyo adhabu ya kijinga huwexi kufungia mtu mwaka mmoja,sasa yeye stakula wapi keann waxingemtoza fine ?

Nini maana ya adhabu tracy martins? Mtajifunzaje sasa au unataka kila alie na uwezo wa kulipa fine basi apate mwanya wa kufanya anachojisikia hata kama ni kosa huku akijua fine anaweza toa..leo hii ukiambiwa adhabu kubwa ya kutukana mtu ni faini ya shilingi mia tano...patakalika hapa?!
 
Last edited by a moderator:
Inatibidi tuangalie na uwezo wa mtoa hoja yaani Dj. Fetty. Ana uwezo mdogo wa kufikiri, ni mtoto ki umri na hana shule. Naona kwa uwezo wake yupo sahihi.

BASATA wapo sahihi, nawaomba huu uwe mwanzo na uwe endelevu ili kuepusha hoja za vilaza siku zijazo.

mkuu Fetty ni degree holder sio kwamba hana shule kama unavyodai
 
Hivi mmemuelewa fetty kweli?.....kuna sehemu kauliza swali....!japokuwa kaanza na mifano? Pia hata kwa wale mliosoma Law chuoni nadhani mnaijua Formula ya IRAC wakati wakujibu maswali ya kesi.....hio R inasimama kama reference

So fetty yupo sahihi........
 
Ila mbona kuna picha za wanenguaji huwa zinasambaa wamekaa kwenye steji na hawajavaa kofuli, nanihii ziko wazi hadi utumbo unaonekana?au wale sio watz?

Mwisho wa siku ni muhimu sheria ikawa msumeno na kukata bila kuangalia sura.

mkuu hadi utumbo????
 
Huyu eti ni mtangazaji, tena eti ni."graduate". Hivi shule alikwenda kujifunza ujinga ?(as FaizaFoxy always ask)

Kutokuchukuliwa hatua kwa "anti virus" HAKUHALALISHI kosa la shilole! Shilole AMEKOSEA, na alipewa nafasi ya kujieleza lakini ALIKAIDI(Kwa mujibu wa barua ya BASATA), Sasa mlitaka BASATA wafanyeje?

Watanzania bwanaaaa...shilole alipoonyesha "MEWATA" hadharani mlilaani kwelikweli humu, leo kachukuliwa hatua mnalalamika, mlitakaje?alishakanywa before na bado akawa anaendelea.

Hivi ikiwa kweli lile tukio lilikuwa bahati mbaya, je baada ya nguo kuachia alikatisha show kwa muda na kwenda kujistiri au aliendelea kupiga mzigo?......she is "un.civi..li..zed" huo ndio ukweli. Acha yamkute.

Interest yangu ni hapo kwenye Graduate. Huyu si jina lake anaitwa Fatuma Hassan, alishiriki chuo kikuu cha Tumaini, Kampasi ya Dar es salaam pale Mikocheni (Barabara ya kuelekea Cocacola), na miongoni mwa Lecturers wake wa somo la Mass communication alikuwa ni Godwin Gondwe na kuhitimu mwaka wa masomo 2013/2014?!!!

Naomba nimuhifadhi...

mkuu Fetty ni degree holder sio kwamba hana shule kama unavyodai

Usiongee usilolifahamu. Sio kila mwanachuo ni Degree Holder mkuu. Wengine tunamfahamu coz tulisoma nae pale chuoni, so tukiona vitu kama hivi tuna-refer tu na kumwombea kwa Mungu 'kimya kimya'.

Kama vipi kausha mumy..
 
Interest yangu ni hapo kwenye Graduate. Huyu si jina lake anaitwa Fatuma Hassan, alishiriki chuo kikuu cha Tumaini, Kampasi ya Dar es salaam pale Mikocheni (Barabara ya kuelekea Cocacola), na miongoni mwa Lecturers wake wa somo la Mass communication alikuwa ni Godwin Gondwe na kuhitimu mwaka wa masomo 2013/2014?!!!

Naomba nimuhifadhi...



Usiongee usilolifahamu. Sio kila mwanachuo ni Degree Holder mkuu. Wengine tunamfahamu coz tulisoma nae pale chuoni, so tukiona vitu kama hivi tuna-refer tu na kumwombea kwa Mungu 'kimya kimya'.

Kama vipi kausha mumy..

Mkuu hebu weka mambo hadharani . kuna vijana wanamchukulia kama "role model"(i am not the one) kwao ,kwa hiyo ni muhimu kujua kama ni kweli ni graduate or not ili pia wajifunze hata kwa mistake za huyo role model wao(kama zipo)
 
Hawa madogo wa xxl nawakubali ila sometimes wanakuwa "very four"

Huwa sielewi uwepo wa Basata ila hata Ng'ombe na udunya wake lakini tukumbuke ana uwezo wa kupiga teke, sasa kama utamuacha mwanao akampapase kwa sababu tu hapo nyumbani mmezoea kumpapasa na hana madhara kuna siku utarudi mtoto taya inaning'inia.

Pili huyo Shilole anayetetewa ni wachache tu wasiojua kuwa amefyatuka, sasa kuanza kumtetea kama vile hilo limemkuta Nyota Waziri ni ajabu.

Hata leo tukipiga kura ya wanaounga mkono adhabu ya Basata mtaambulia kura za baadhi ya Wanaclouds na Nuhu.

Alafu ndugu zangu wa Clouds muache kudhani kwamba ndio mnaopaswa kufahamu kila jambo, nyie wenyewe mpaka wa leo kuna wasanii mmewaweka kifungoni kwa muda usiojulikana....na sijui kama hao BASATA wamewahi kuwahoji...na kama wamewahi kufanya hivyo sijui ni jibu gani mliwapa kuhalalisha kwani mpaka wa leo hatuwasikii kina 20% na wengineo.

Kama nyie mkikerwa mnaumia na kuadhibu basi ndivyo na hao BASATA wanavyolazimika pale wanapokerwa, au kuadhibu muachiwe nyie wengine wabaki kushabikia ?

Na swala la mbona na fulani alifanya hivyo halina mantiki na halipaswi kuhojiwa na mtu yeyote mwenye uwezo wa kupima mambo.

Adhabu ya Shilole ni sahihi na tumieni muda huu kuhimiza Wasanii kujali staha wawapo jukwaani.

Anayekwenda kuangalia Kangamoko huenda kwa ridhaa yake na hutarajia kuona anayoyaona, ila kuandaa jukwaa la muziki na kuwakuta Kangamoko nao wapo ni dhuluma kwa wasiopenda hayo.
 
On Instagram:

@Thebestfetty; "Zilitoka mixtape za matusi za ANTI VIRUS vol 1 na 2, BASATA ilikaa kimya na ilitoa kibali cha uzinduzi wa anti virus volume 2, Viwanja vya posta, licha ya kuwepo kwa malaamiko. SWALI ni, kifungu kilichotumika kumhukumu ni kuwa UCHI au ni UVUNJAJI WA MAADILI????".

=====


Dada naona ana hasira na Vinega.

Na nyie ma bwana mdogo watangazaji wa hapo, this is too big for you, but let me give a little F***K YOU, i know that you under pay, mnaendekeza rushwa sio!! You are next(anti-virus mixtape sauti ya Sugu)
 
Back
Top Bottom