Dj Majizo, Muasisi wa muziki wa Mchiriku, Mnanda, Singeli redioni!

Usijifanye unanjua sana kuliko mama
Usijifanye unanijua sana kuliko wana maskani
 
Halafu naona kama hiyo "Hainaga Ushemeji" ndio imependwa sana humu,
Kunaniiii???
ndo hali halisi ilivyomtaani,demu mmoja anaweza akazungukiwa ba watu hata watano tena wanaofahamiana,leo kaliwa na man fongo,kesho kaliwa na mesen,kesho kutwa na tito yaana mpaka P nae anapita,alafu wote wanafahamiana ndo maana akasema skuiz hamnaga ushemeji watu wanakula tu
 
bado taarab sasa zipate airtime ya kutosha ikibidi ziingia hadi kwenye chart za top 10..top 20 n.k
 
Wakati Msaga sumu anaanza ,Watu wengi waliona kama mziki huu ni wa kihuni ,hivyo ulisikika kwenye shuhuli za uswahilini tu na kwenye vigodoro
Lakini baada ya efm kuingia ikaanza kuusapoti mziki huu kwa kupiga nyimbo zao mara kwa mara mhhhhh hadi watoto wa masaki na mbezi beach nao wanaijua singeli na wanaicheza...

Wakati kipindi kilee ulikuwa mziki wa temeke uswahilini...lakini now singeli inajulikana na kukubalika tz nzima sasa.Na huu mziki umeanza kuwa tishio hata kwa bongo fleva maana vijana wanaukubali sana sasa hivi...pongezi kwenu E- FM.
 
Inasemekana Dj MAJIZZO ndiye kijana tajiri zaidi hapa bongo ukimtoa Mo Dewji.

Inasemekana lakini...
 
Hata mimi nahisi
Mtoto hamisa kavua chipu hivi hivi tuu
 
Mbali na yote mazuri yanayoendelea kuibuka kuto hii radio ya E-fm .. niepnde tu kuchukua nafasi hii kutoka chini ya Uvungu wa moyo wangu kupongeza Uongozi mzima wa E-fm Radio kwa juhudi zao za kuupromoti mziki huu wa jiji Dar-es-salaam kwa Jina maarufu la SINGELI.

vipindi vya Jioni mziki huu hupigwa saana , na mara nyingi pia Asubuhi .. na kuupelekea mziki huu kua maarufu gafla nankua kivutio cha watu wengi.

Mbali na kuweka juhudi katika mziki huo ..pia wamekua na vipindi vinavyovutia ..kama ni mtuamiaji wa Dalaladal ..kila upandapo Radio inayosikilizwa ni E-fm Radio .
Hongereni saana na mmeleta chamgamoto kubwa kwa radio nyingine kutofanya kazi kimazoea ...kuna radio maarufu tutaanza kuzisahau mda si mrefu .
 
Hivi msaga sumu aliimba wimbo wa lowasa kipindi cha kampeni? Nyimbo yake naipenda mpaka leo.
 
Kuna wimbo unaitwa makabila naupenda ile mbaya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…