Uchaguzi 2020 Dkt. Charles Kimei aonesha ukomavu, awashukuru wanachama kwa kumuamini katika hatua ya awali

Uchaguzi 2020 Dkt. Charles Kimei aonesha ukomavu, awashukuru wanachama kwa kumuamini katika hatua ya awali

Inavyoelekea ata angeshinda wangemkata juu kwa juu, kwenye interview yake Dr Bashiru ilikuwa keshaanza kumrushia dongo alianza na kujitolea mfano yeye kuna watu tukishapewa nafasi fulani kugombea zingine inakuwa aiwezekani tena baada ya kumaliza muda wetu.

Wakati anataka kuendelea sasa unakuta mtu keshakuwa mkurugenzi lakini....akawa disrupted na swali lingine, inaonekana wangemlimia mbele ata angeshinda kura za maoni.

Ingelikuwa kweli anataka siasa angeachia nafasi yake CRDB kabla ya umri wa kustaafu akagombea ubunge; unasubiri pepo ipotee ndio ujifanye unajali it doesn’t work that way regardless how qualified he is.
 
Mkurugenzi Mtendaji Mstaafu wa CRDB Dkt Charles Stephen Kimei ambaye alijitosa kutafuta tiketi ya kuteuliwa kuwa mgombea ubunge jimbo la Vunjo kupitia CCM na kupata kura 178 huku mshindi Ndugu Enock Zadock Koola akipata kura 187 amesema anawashukuru wanachama wenzake kwa kumuamini katika hatua hii ya awali.

Na amewaomba kuendeleza umoja na mshikamano ili pale vikao vya uteuzi vitakapokamilisha kazi yake na kutupa mgombea mmoja kwa pamoja tukahakikishe anashinda na CCM inapata ushindi wa heshima kwa ngazi zote.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi
Siasa za bongo kujuana watu hawaangalii uwezo wala CV ya mtu.Yaani kama hujuani na wajumbe basi huchaguliwi.

Ndugu yangu Mayala nae kalala na viatu,japokuwa maarufu humu JF,CV nzuri ila wajumbe wenye CCM yao hawakujui.
 
huyo mangungu ana kasoro gani?Ilitakiwa wampe nani?
Mangungu alishawahi kuwa mbunge 2010..2015 wananchi hawakuona cha maana alichofanya 2015..2020 wakapeleka jimbo upinzani kwa makusudi...... Leo hii kwa tamaa ya pesa walonayo wajumbe wa mkutano mkuu wilaya wamenunuliwa wamempitisha yule yule asiyekubalika
 
ooh hapo kweli wamefanya utopolo
Mangungu alishawahi kuwa mbunge 2010..2015 wananchi hawakuona cha maana alichofanya 2015..2020 wakapeleka jimbo upinzani kwa makusudi...... Leo hii kwa tamaa ya pesa walonayo wajumbe wa mkutano mkuu wilaya wamenunuliwa wamempitisha yule yule asiyekubalika
 
Ila wachaga hawaangali pesa wala vyeo. Ingekuwa Bariadi kwetu basi Kimei angeshinda asubuhi. Chenge alitoka Dar akaja akashinda kirahiiiiisi.
Ulizia The Late Paul Bomani vs Pascal Mabiti , au Jumanne Malecele vs Kibajaji
 
Mkurugenzi Mtendaji Mstaafu wa CRDB Dkt Charles Stephen Kimei ambaye alijitosa kutafuta tiketi ya kuteuliwa kuwa mgombea ubunge jimbo la Vunjo kupitia CCM na kupata kura 178 huku mshindi Ndugu Enock Zadock Koola akipata kura 187 amesema anawashukuru wanachama wenzake kwa kumuamini katika hatua hii ya awali.

Na amewaomba kuendeleza umoja na mshikamano ili pale vikao vya uteuzi vitakapokamilisha kazi yake na kutupa mgombea mmoja kwa pamoja tukahakikishe anashinda na CCM inapata ushindi wa heshima kwa ngazi zote.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi
Ahamishie turufu yake ACT
 
Nahisi hapa labda wapindue meza. BTW ameshindwa pia kwa kura chache, kwa hiyo hata wakipundua meza kuna justification wanaweza toa.

Lakini muda mwingine huwa nawashangaa wapiga kura kumtosa mtu kama Kimei (Phd Holder in Economics, Corporate leader) hawa ndo watu wa kupigiwa kura jamani
Wabunge ni wawakilishi wa wananchi. Inatakiwa mbunge awe mmoja wenu, mwenye kuelewa mahitaji yenu, maisha yenu, na mwenye kuwa na interest zenu moyoni. Sio mtu anayeishi kama malaika, utegemee anakumbuka maisha ya kishetani yalivyo hata kama alitokamo humo.
 
Amefuata nyayo za Makonda za kushukuru wananchi hata ukishindwa
 
Kimei lazima atinge bungeni either kwa Kuchaguliwa au kwa kuteuliwa nahisi Phd nyingi zimekimbilia majimboni kama kina Ndalichako, Philip Mpango, Kabudi n.k ivo mzee baba katika zile nafasi zake 10 za wabunge atavuta PHD nyingine ili Cabinet yake ishibe Wasomi kuanzia Naibu mpaka Waziri
 
Mkurugenzi Mtendaji Mstaafu wa CRDB Dkt Charles Stephen Kimei ambaye alijitosa kutafuta tiketi ya kuteuliwa kuwa mgombea ubunge jimbo la Vunjo kupitia CCM na kupata kura 178 huku mshindi Ndugu Enock Zadock Koola akipata kura 187 amesema anawashukuru wanachama wenzake kwa kumuamini katika hatua hii ya awali.

Na amewaomba kuendeleza umoja na mshikamano ili pale vikao vya uteuzi vitakapokamilisha kazi yake na kutupa mgombea mmoja kwa pamoja tukahakikishe anashinda na CCM inapata ushindi wa heshima kwa ngazi zote.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi
Huyu ametafuta kujidhalilisha tu
 
Ila wachaga hawaangali pesa wala vyeo. Ingekuwa Bariadi kwetu basi Kimei angeshinda asubuhi. Chenge alitoka Dar akaja akashinda kirahiiiiisi.
Wewe ni wa Bariadi au Gitega?
 
Hapa ndo ujue kwamba ulimwengu wa wapigakura ni tofauti sana na ile dunia tunaoishi tunaojifanya wasomi na wajuzi wa mambo.

Same same kwa kilichompata ndugu Pasco Mayalla, ujuaji mwingi wa hoja ila wakulungwa wamemkata.

Ila nadhani kamati kuu hapa kwa Kimei lazima wapindue meza
Itakua sio sawa

Kwa calliber yake alitakiwa awe mshindi wa kishindo

Wakaazi wa kule hawamtaki
 
Nahisi hapa labda wapindue meza. BTW ameshindwa pia kwa kura chache, kwa hiyo hata wakipundua meza kuna justification wanaweza toa.

Lakini muda mwingine huwa nawashangaa wapiga kura kumtosa mtu kama Kimei (Phd Holder in Economics, Corporate leader) hawa ndo watu wa kupigiwa kura jamani
Unawez akuanmaarufu nchini lakini anayekupita kwa kura ni maarufu jimboni kwa mchango wake ki utendaji
 
Ila wachaga hawaangali pesa wala vyeo. Ingekuwa Bariadi kwetu basi Kimei angeshinda asubuhi. Chenge alitoka Dar akaja akashinda kirahiiiiisi.
Kwenu Moshi pesa mbele Mama. Chenge ni maarufu na wanamuamini bila hata ya pesa. Hawafahamu makandokando yake. Kimei yawezekana hakucheza rough ndiyo maana.
 
Back
Top Bottom