Uchaguzi 2020 Dkt. Charles Kimei aonesha ukomavu, awashukuru wanachama kwa kumuamini katika hatua ya awali

Uchaguzi 2020 Dkt. Charles Kimei aonesha ukomavu, awashukuru wanachama kwa kumuamini katika hatua ya awali

Nahisi hapa labda wapindue meza. BTW ameshindwa pia kwa kura chache, kwa hiyo hata wakipundua meza kuna justification wanaweza toa.

Lakini muda mwingine huwa nawashangaa wapiga kura kumtosa mtu kama Kimei (Phd Holder in Economics, Corporate leader) hawa ndo watu wa kupigiwa kura jamani
Nini maana ya kupiga kura ili kumpata mshindi?
Hata Kimei angeachwa kwa kura moja tu, bado atakuwa ameshindwa. Ni vyema aliyeshinda akaheshimiwa na kupewa haki yake ya kugombea.

Kuhusu Elimu na umaarufu, kwenye kura za maoni sio kigezo kabisa, na huwa hakiangaliwi kabisa na wajumbe wa CCM.
Kuna mamia ya wasomi na watu maarufu kama Kimei wameangukia pua. Kwanini upendeleo uwe kwa Kimei tu?

Jiulize tu hili swali, Kimei ameifanyia nini CCM Vunjo mpaka awe mgombea wao?

Yote kwa yote, kwangu ningependekeza kuwa mahali popote ambapo mshindi ameongoza kwa tofauti ya kura chache, basi kinyang'anyiro kirudiwe tena, wagombea wasiozidi watatu wenye kura nyingi ndio washindane.
 
Kimei lazima atinge bungeni either kwa Kuchaguliwa au kwa kuteuliwa nahisi Phd nyingi zimekimbilia majimboni kama kina Ndalichako, Philip Mpango, Kabudi n.k ivo mzee baba katika zile nafasi zake 10 za wabunge atavuta PHD nyingine ili Cabinet yake ishibe Wasomi kuanzia Naibu mpaka Waziri
Mambo sio rahisi na mepesi namna hiyo.
Ngoja nikupe somo kidogo kuhusu zile nafasi kumi za bure kutoka kwa Rais.

-Kwanza kikatiba zimegawanywa kijinsia (Ni lazima wanawake wasipungue watano!)

-Pia zipo kimkakati, rais anazitumia kuingiza watu wake bungeni waliopo tayari karibu yake au katika serikali yake (Magufuli ndio amefanya hivyo), au kulipa fadhila (Mkapa alifanya hivyo) au Zawadi (Kikwete alifanya hivyo).

-Kiufundi Rais hapaswi kuzitumia zote kwa wakati mmoja, anapaswa kuzitumia kama spare tyre ya kisiasa!

Binafsi sioni nafasi kwa Kimei kuambulia chochote hapo. Kulingana na kabila alilopo Kimei (mchaga), hivyo vyeo vya kupewa ubunge+uwaziri ni ngumu kuvipata kutoka kwa Magu.
 
Dr Kimei awe na shukrani, ajipongeze kawazidi Mwijaku na Mpoki.
 
Hapa ndo ujue kwamba ulimwengu wa wapigakura ni tofauti sana na ile dunia tunaoishi tunaojifanya wasomi na wajuzi wa mambo.

Same same kwa kilichompata ndugu Pasco Mayalla, ujuaji mwingi wa hoja ila wakulungwa wamemkata.

Ila nadhani kamati kuu hapa kwa Kimei lazima wapindue meza
Mkuu Naantombe Mushi, kuna watu mliona mbali!, kama vikao vya CCM vilivyopindua meza na kumpitisha, ila kiukweli huyu ni mtu muhimu kwasababu ndiye Waziri wetu mpya wa fedha. Japo nasikia wana Vunjo nao wana jambo lao!, lakini kwa sasa hali ilivyo, hakuna jambo lolote popote, chama cha ushindi ni kimoja tuu, the one and only !.
P
 
Back
Top Bottom