Dkt. John Pombe Magufuli, Dkt. Hussein Mwinyi na Maalim Seif watuzwe udaktari wa heshima

Dkt. John Pombe Magufuli, Dkt. Hussein Mwinyi na Maalim Seif watuzwe udaktari wa heshima

Kabende Msakila

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2020
Posts
1,809
Reaction score
1,692
Wanabodi, Salaam!

Kwanza nianze kwa kukupongezeni kwa uhai wenu ndani ya kundijamii hili - nafahamu kwamba pamoja na kuwa tumo watu wa itikadi tofauti za vyama vya siasa, dini tofauti, jinsia na makabila tofauti lkn bado tunatumia jukwaa hili kutoa ya akikini mwetu ili yasaidie kuijenga nchi yetu. Hongereni!

Pili nchi yetu imekuwa wakati mwingine ikipitia vipindi kadhaa vigumu hususan nyakati za uchaguzi mkuu - migogoro midogo kwa mikubwa imekuwa ikitokea miongoni mwa makundi ya wanasiasa na vyama vyao. Lkn ukomavu wa kidiplomasia walionao viongozi wetu ndiyo imekuwa kinga na msaada kwa taifa kutoingia kwenye machafuko na umwagaji damu.

Nasema haya kwa kuwa kitendo cha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kufikia mwafaka unaotokana na mgogoro wa kiuchaguzi wa nyuma, wakati na baada ya tarehe 28 Oktoba kati ACT Wazalendo (Maalim Seif), na CCM (Dkt Magufuli na Dkt Mwinyi) cha kukubali kufanya kazi kama timu moja kinastahili pongezi nyingi sana na zawadi yenye kumbukumbu isiyofutika kwa viongozi hao.

Ndiyo sababu nashauri, napendekeza, na kuonelea kwamba viongozi hao watatu yaaani:-
(i) Dkt John Pombe Magufuli,
(ii) Dkt Hussein Mwinyi, na
(iii) Maalim Seif S Hamad - watunukiwe udaktari wa heshima kwa kukubali kumaliza mambo magumu na mazito kwa njia ya mazungumzo.

Nanyi CHADEMA, NCCR, CUF, nk jifunzeni maridhiano toka kwa wazee wetu hao. Wakati wa Mungu ukifika mtatawala - na kamwe tusisukumwe na hulka za Wabeligiji na vibaraka wengine ambao wana nia ovu kwa taifa letu

Msakila M Kabende
Bukoba
Kagera
06 Desemba, 2020.

************
Kitendo cha Maalim Seif Sharifu Hamad ukukubali wito wa Dkt John Pombe Magufuli na Dkt Hussein Mwinyi kuunda Serikali ya Umoja wa kitaifa ni cha kupigiwa mstari - hapo hata mabeberu yamevunjika moyo - hili hata Joe Biden USA hataliweza dhidi ya Donald Trump.

Heko JPM, HM, SSH!
Mungu ibariki Tanzania
 
Kwahiyo tena 2025 huku Tume huru ikikosekana, watu wauawe, watiwe vilema halafu tena yafanyike maridhiano kwa mara nyingine tena sindiyo, ndugu Kabende?

Kwakweli mi naona tusiwe tunaharibu pesa kufanya uchaguzi ambao matokeo yake yanajulikana, badala yake pesa hizo zitumike hata kuajiri waalimu ambao katibu alidai wameajiriwa 13000 akidhani bado tu wajinga, kumbe hata 8000 hawajatimia, hadi pale malalamiko yalipoibuka.
 
Hizo PhD si ziko tele kule jalalani si uwapeleke wakachukue na wewe uchukue yako PhD in Political Stupidity? Nshomile huyo!
 
Kabende na wewe akili zako kama za Zito anaesema tumeamua kukubali kutengeneza serikali ya umoja wa kitaifa kama katiba inavyo tutaka lakini msimamo wetu ni ule ule wa kutotambua uchaguzi.

Sasa wewe umeona uchaguzi ulivyoendeshwa, watu waliokufa na si mara ya kwanza ni takribani mara zote Zanzibar inakuwa hivyo.Katika muongozo wa dini yetu tunaamrishwa kutetea haki na kuitafuta mpaka ipatikane.

Haturuhusiwi kuwa wanyonge kila mmoja akukanyage kadiri anavyo taka ,Sasa Maalim Sefu na Zito ni wanafiki sana tena sana ,mnasema hamtambui uchaguzi lakini mnaungna tena na hao madhalim.

Hawa madhalim wauaji Mwinyi na Magufuli ndoo unataka wapewe heshima iliyotukuka kwa kuua raia wasio na hatia ,ambao washakula kiapo ni bora Zanzibar wafe wote lakini Ccm iendelee kuwa madarakani ,daaaa!!! Muogope Mungu wako wewe tena muogope sana.
 
Hapa mjinga ataungana na mtoa hoja ila mwelevu atampinga mtoa hoja. Haiwezekani Nchi hii ambayo kila kiongozi anaapa kulinda katiba yetu na uhai wa watu wake halafu afurahie damu ya mwananchi ikimwagika?halafu useme apewe tuzo?Kwa hyo apewe Tuzo ya Damu au nini?
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Mshindi maalim ameibiwa na amefuata maoni ya wanachama, kwa chadema maoni ya wanachama ni timua Covid-19 na kutopeleka wabunge viti maalumu, pia chadema wako sahihi.

Ila busara anayo Dr. Mwinyi, akulazimisha, alishauri, na kusubiri na wala hakutoa vitisho alikuwa muwazi na alijipambanua, sio huku bara kila mtu nguvu tu, na giliba kulazimisha mambo, kisa hofu kuiba kura kipitiliza!
 
Hao wote ni madaktari tayari.

Sema wapewe nishani ya Desmond Tutu? Au nishani za humu JF?

Muda ukifika dunia inayowamulika itawapa.
 
Hebu tutolee upuuzi wako hapa! Huchoki kuandika upuuzi kila kukicha? 😳
 
Hebu tutolee upuuzi wako hapa! Huchoki kuandika upuuzi kila kukicha? 😳
Jema kwako ni lipi - unapenda tuwe kama Tigray vs Main Ethiopia?

Tanzania tunaishi kwa maridhiano na kupendana ndiyo sababu Katambi, Mughwira, Kitila, Waitara wote wameshajua kazi nzuri ya JMT
 
Siku ukitia akili kichwani UTAELEWA TU kwa sasa endelea na UMBUMBUMBU wako.
Jema kwako ni lipi - unapenda tuwe kama Tigray vs Main Ethiopia?

Tanzania tunaishi kwa maridhiano na kupendana ndiyo sababu Katambi, Mughwira, Kitila, Waitara wote wameshajua kazi nzuri ya JMT
 
1456109.jpg
457901234.jpg
 
Back
Top Bottom