Mtuflani Official
JF-Expert Member
- Dec 31, 2019
- 1,952
- 4,416
J’pili saa nane na nusu mchana angalia marudio ya kipindi EATV ujue kwanini hakutaka kununua kwa mkopo!Mwehu tu, unaomba mkopo unanyimwa unanunua kwa cash, sasa kama cash ilikuwepo kwanini atake mkopo? Alizani mo ataogopa uwaziri wake?
Hawa wote wlifanya michezo ya kitoto sana.
HK kumhoji Mo kupitia social media ilhali ana namba yake na pia kuna vikao vya chama ni uzwazwa wa kiwango cha lami...hata kama angekua na nia njema kiasi gani...kila mtu angehisi ni hasira za kukosa mkopo wa pikipiki.
Kwa mfanya biashara mkubwa kama Mo dewj kumuweka hadharani tena mtandaoni mteja aliyetaka kumkopa...huu nao ni utoto..hakuna aliyetegemea kitu kama kile kutoka kwa mfanya biashara mkubwa Tanzania na Africa kiujumla.
Wangekua na busara hili suala wangeacha kuliongelea kwani hakuna awezaye kujisafisha zaidi kukumbusha watu upuuzi wao.
Hamisi anapenda ubishi na visasi kama Magufuli. Watu wa kanda ile muna shida gani? Mimi mtu wa ukanda wa Pwani nimeolea kule kanda ya Ziwa nazijua vizuri tabia za wakwe zangu na shemeji zangu.
Usimkopeshe mwanasiasa, askari polisi au hawa wanaojiita usalama wa taifa. Huwa hawalipi madeni hawa watu Bwashee! Mo mtoto wa mjini analijua hili.
Huyu Waziri inakuwaga Kama akili yake siyo nzuri, kinachonishtuaga zaidi kwake ni yeye kushindwa kuandika hata sentence mbili za kiingereza kwa usahihi.
Dah...Kwa tuliosoma Political Science…alichofanya Mo ni notes tupu na ameshinda kwa style aliyotumia
Bila ya kutumia Silaha ya 'Mkopo wa Bodaboda' unadhan Mo angejibu kitu gani kuhusu hoja ya Kigwa
Sasa hivi Kigwa kila anapokutana na Watu kazi yake ni kufafanua 'Mkopo wa boda boda' sio tena hiza za 20 billion
Oxford University usifananishe na MUHAS
Hahahaaaa....... Tukutuku aka Vipando!Dah...
Hata huu uzi unaongelea boda boda zaidi.
'…muna…nimeolea…' utakuwa mtu wa pwani ya ziwa Victoria