Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli ataka Watanzania kukataa ubaguzi

Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli ataka Watanzania kukataa ubaguzi

Alwatan Mabruki

Senior Member
Joined
Sep 20, 2020
Posts
132
Reaction score
116
2CDBC5CA-4BCD-4CB6-A6F3-549D56A96184.jpeg


Ikiwa ni siku saba zimebaki kuelekea uchaguzi mkuu, mgombea wa Urais kupitia CCM Mhe. Dkt. John Magufuli, amewataka Watanzania kujitenga na propaganda za ubaguzi zinazoenezwa na baadhi ya wagombea.

D2557E48-934D-44D7-85E0-49E444A1CDF6.jpeg


Pia amewatahadhalisha Watanzania wakiona mtu anaongea kuhusu chuki, wafahamu kwamba hayupo kwa maslahi ya Taifa, bali ana malengo mabaya ya kuleta machafuko nchini.

3F0334D9-5EB6-4639-ACAD-137DE4B48C10.jpeg


Alitoa rai hiyo jana wilayani Korogwe mkoa wa Tanga wakati akihutubia wanachama wa CCM waliojitokeza kwenye viwanja vya chuo cha walimu Korogwe.

ABDEC33B-EFA6-4538-8C88-D95CA6DD7E7A.jpeg

 
Kuna mwanasiasa mbaguzi na mwenye chuki nchi hii kumzidi Jiwe? Jiwe aliwaambia wapiga kura wakichagua chama tofauti na ccm hatawapelekea miradi ya maendeleo. Huo ni ubaguzi, na ni siasa za chuki.
 
amewataka watanzania kujitenga na propaganda za ubaguzi zinazoenezwa na baadhi ya wagombea.
NI KWELI
Na ili kujitenga na huu ubaguzi inabidi Magufuli akataliwe na watanzania wote 28/10/2020. Kwasbb yy ndiye muasisi na mpigania ubaguzi hapa nchini.

Ametamka zaid ya mara 100 kwamba maeneo yatakayo chagua upinzani hapeleki huduma za kijamii.

Ajiandaye kurudi Chato.
 
Kama kunajambo limemshinda kulificha moyoni mwake nihuo ubaguzi. Inafikia hatua anasema hatagawa chakula kwa mtoto wa kambo akaacha mwanae,akiyaita majimbo ya upinzani watoto wa kambo. Tena kauli hii haizungumzi kwa bahati mbaya anamaanisha manake ameizungumza Korogwe,Mara,Same nk
 
Kama kunajambo limemshinda kulificha moyoni mwake nihuo ubaguzi. Inafikia hatua anasema hatagawa chakula kwa mtoto wa kambo akaacha mwanae,akiyaita majimbo ya upinzani watoto wa kambo. Tena kauli hii haizungumzi kwa bahati mbaya anamaanisha manake ameizungumza Korogwe, Mara, Same nk
 
..kuna mwanasiasa mbaguzi na mwenye chuki nchi hii kumzidi Jiwe? Jiwe aliwaambia wapiga kura wakichagua chama tofauti na ccm hatawapelekea miradi ya maendeleo. Huo ni ubaguzi, na ni siasa za chuki.
Hizo ndio propaganda zenyewe sasa!

Yeye alikuwa anapiga kampeni, sasa ulitaka aseme chagueni yeyote wakati anakinadi chama chake cha ccm?
Kwani Lisu anaposema msichague wana ccm huwa anakuwa anaeneza ubaguzi
 
Amewabagua kaskazini ajawafanyia chochote amewabagua anaenda kuwaomba kura wao ni muhimu wkt wa uchaguzi tu
 
Ikiwa ni siku saba zimebaki kuelekea uchaguzi mkuu, mgombea wa Urais kupitia CCM Mhe. Dkt. John Magufuli, amewataka watanzania kujitenga na propaganda za ubaguzi zinazoenezwa na baadhi ya wagombea...
Huyu ndie mbaguzi nambari one Tanzania halafu anasema nini? Lissu ndiye mwenye mamlaka ya kusema hayo sio jiwe.
 
Nimeshangaa Aliposema Hawezi Kuifanya Moshi Kuwa Jiji Sababu Ilikuwa Chini Ya Upinzani
Wakichagua Ccm Itapewa Hadhi Hiyo!!!😁😂🤣
Kuna Mambo Yanatia Kinyaa 😏😏😏😐
Kwani hats likiwa jiji wakazi wake watagaiwa hela? Ajira zitatolewa na ukaliwamaisha utapungua? Mimi siwapendi sana wanasiasa manake wanaomba huku wanatukana. Sasa hapo ndio atapewa kura ili pawe jiji?
 
Hizo ndio propaganda zenyewe sasa!

Yeye alikuwa anapiga kampeni, sasa ulitaka aseme chagueni yeyote wakati anakinadi chama chake cha ccm?
Kwani Lisu anaposema msichague wana ccm huwa anakuwa anaeneza ubaguzi
Kwaiyo hawezi kunadi chama chake hadi awatishie wananchi kwa kauli za kibaguzi? Kiongozi mwema asiye m'baguzi hawezi kuwachimbia wananchi mikwara ya kutowapelekea maendeleo maeneo ambayo hakitachaguliwa Chama chake.

Kiongozi mwema huwahudumia wananchi wake bila kubagua imani ya chama mana kila mmoja ana uhuru kuchagua anachokipenda, na yeye pia ni wajibu wake kuwapelekea maendeleo wananchi wake kwa sababu kwenye hayohayo maeneo yanayoongozwa na wapinzani kuna watu hawana vyama, hao pia wanahitaji kupelekewa maendeleo pia.
 
Back
Top Bottom