Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli ongea na wazee, wakuu wa Taifa! Sioni mwisho mwema kama nabii

Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli ongea na wazee, wakuu wa Taifa! Sioni mwisho mwema kama nabii

Pole kwa msongo wa mawazo.
Uhalisia ni kwamba Magu amewakonga nyoyo wanyonge na amewaudhi majizi.
Hakuna mgonjwa yeyote atakaye sema ovyo kwa Magu.
Huo ndiyo uhalisia 91% wanampa kura ya ndiyo.

Check likes za comment yako. Ni 6 tu.

Ila linganisha na comment pinzani zina likes 50+

Utagundua ulichokiandika siyo uhalisia
 
Mh Rais, pole kwa mihangaiko ya kupiga kampeni ila nina neno moja juu yako usiku Waleo nalo ni siri japo sio Siri baada yakuandika hapa.

Hali inayoendelea hata tukiwa wanafiki na kuwa tumekunywa maji ya bendera mwisho pumzi zitakata na zikikata mashambulizi yatakuwa makali zaidi kuliko wakati huu tuna nguvu.

Asikudanganye mtu, hali sio hali, yani hata kama ni kwa goli la mkono, ila mtiti huu utakusumbua katk awamu yako ya pili kiasi utahisi kila mtu ni msaliti.

Kuna hali sio ya kawaida huku uraiani, yani watu wamejawa na machungu kiasi hawana pa kupumulia ila tu 28.10.2020.

Majeshi na idara za usalama hawatoweza kudhibiti hili vuguvugu na wakiweza basi watu wengi watakuwa silence jambo litazidi kuibuwa vuguvugu jingine baya zaidi, jambo litazigawa idara zako za ushauri.

Uongozi ni kuacha alama na ili ufanikiwe kubali yaishe, kaa na waliokuweka vua urais wako omba ushauri Ila kumbuka shida ipo nyingine Nani wakukupa honest feedback kwa aina ya uongoz wako mkali sana Mzee wangu hapa tafuta MTU tu akusaidie upewe honest feed back japo sijui kama utaipata Mungu akusaidie.

Pamoja umefanya yote mazuri Ila trust me umeshindwa ishi mioyoni mwa Watanzania. Embu jiulize why? Umeme umetadanza kama uyoga, maji kama yote, mahospitali kama yote, madege, reli.

Yani hakuna mahali hujagusa, umefanya mambo makubwa sana ila umeshindwa kula na kipofu, sasa kipofu kapata kipofu aliewahi kuona hapo zamani Ila baadae akawa kipofu. Amewaambia vipofu wenzake huko sio, hiyo njia sio, wamemwamini ani ni shida ukiweka Jiwe na Magi watu wanapigia Kura Jiwe. Why umesahau wakolon walitupa shanga Sisi tukawapa madini?

Ona sasa mziki huu jamaa Hana bango Hana vyombo vya habari Ila ameteka nchi kweupe.

Waite wazee wakushauri maana najuwa uchaguzi huu hautokuwa Rahisi kama tunavyodhani.
Too late !
 
Pamoja na kuongea na wazee.
Kubwa zaidi asikae kimya kwenye haki stahiki zake mheshimiwa Lissu.
Akiwa kiongozi mkuu wa serikali na msimamizi wa yote. Alitakiwa kuwa amesimamia na kuruhusu alipwe haki yake kama mbunge na aliyelengwa akiwa kazini!
Je manunuzi ya wabunge wa upinzani kuunga mkono walilipwa stahiki zao.
Kama kuna matumizi mabaya basi ndiyo hayo na ufisadi! HAKI HAKI YA MTU HAIPOTEI.
 
Pole kwa msongo wa mawazo.
Uhalisia ni kwamba Magu amewakonga nyoyo wanyonge na amewaudhi majizi.
Hakuna mgonjwa yeyote atakaye sema ovyo kwa Magu.
Huo ndiyo uhalisia 91% wanampa kura ya ndiyo.
Nyie ndiyo wanafika sema ukweli itakuwa huru
 
Pole kwa msongo wa mawazo.
Uhalisia ni kwamba Magu amewakonga nyoyo wanyonge na amewaudhi majizi.
Hakuna mgonjwa yeyote atakaye sema ovyo kwa Magu.
Huo ndiyo uhalisia 91% wanampa kura ya ndiyo.
Kwa utopolo huu weweutakuwa kidoti
 
Huwa sipendi kuendeshwa na mahaba. Napenda niendeshwe na akili yangu unayolala kwenye ukweli. Mahaba yafuate akili yangu.

Ukweli ni kuwa Magufuli, yapo mambo amefanya vema, na kuna mengine ameharibu.

Amefanya vema kukamilisha miradi iliyokuwa imeanzishwa na mtangulizi wake:

1) kusambaza umeme vijijini
2) kusambaza maji
3) kuendeleza ukarabati wa hospitali
4) Ukarabati na ujenzi wa mashule, mahakama, stand na masoko
5) Ujenzi wa barabara za mitaani
6) Ujenzi wa madarasa

Magufuli amefanya vizuri pia kwenye mambo yafuatayo
1) kusimamia vizuri matumizi ya fedha za serikali
2) kudhibiti ujambazi
3) Kusimamia nidhamu ya wafanyakazi
4) Uanzishaji wa masoko ya kuuzia madini

Miradi mipya mikubwa mitatu - reli, ndege na umeme, ni miradi mizuri lakini hii miradi inatumia fedha nyingi na haiwezi kujihudumia wala kuanza kurudisha fedha hivi karibuni. Miradi hii haikustahili kufanyika yote kwa pamoja. Kwa fikra zangu, angeanza na reli.

MAENEO AMBAYO AMEFANYA VIBAYA KABISA:
1) Ukatili kwa kutumia watu wasiojulikana kuteka, kupoteza na kuua watu. Hili ni kosa kubwa sana lusilostahili msamaha. Na siku moja ni lazima iundwe TUME YA MARIDHIANO ili tujue ni nini hasa kilimtokea Ben Sanane, Azory Gwanda, na tujue kwa nini walitaka kumwua Tundu Lisu, na wengine waliotekwa na kisha kutupwa maporini, na wale wengine waliouawa na miili yao kutupwa kwenye viroba


2) Kubambikia watu kesi za uhujumu uchumi na kutakatisha fedha, na kisha kuwalazimisha wakiri makosa baada ya kuwatesa kwa kuwaweka mahabusu kwa muda mrefu

3) Kufukarisha watu kwa kutumia sheria zisizo rafiki za TRA na uhujumu uchumi

4) Kuharibu mazingira ya uwekezaji kiasi cha kuua na kufukuza uwekezaji

5) Kutowajali wafanyakazi kwa kutowapa ongezeko la mishahara

6) Kutoheshimu utu na kuwaona watu wengine hawastahili heshima. Na yeye pekee na wateule wake kuwa ndio wenye mamlaka yasiyohojiwa wala kukosolewa

7) kutoheshimu katiba, sheria na kanuni. Kupalilia ubaguzi na kuendekeza upendeleo. Ili kudumisha upendeleo, badala ya kuheshimu taaluma, kila eneo akawajaza makada wa CCM, na zaidi watu wa kanda moja. Hili ni kosa kubwa kabisa la pili. Ni kinyume na kiapo chake

8) Kutoheshimu mipaka na kuingikia utendaji wa mihimili mikuu ya Jamhuri

9) Kudhamiria na kusimamia kifo cha demokrasia, haki na uhuru wa raia na vyombo vya habari, vyama vya siasa na maoni ya raia

10) Kutunga sheria mbaya kwa nia ya kuwadhibiti watu, kuondoa uwazi wa matumizi ya fedha ya Serikali

11) Kuhatibu mahusiano mazuri ya kidiplomasia yaliyokuwepo kwa kujrnga hisia za kibaguzi na kupandikiza fikra kwa watu waamini kuwa kila mzungu ni mnyonyaji na adui. Kuharibu mahusiano yetu ya karibu na nchi ya Kenya. Na kwenye hili kama si busara za Kenyata, huenda hata mipaka ya nchi ingekuwa tayari imefungwa


Sent using Jamii Forums mobile app
A fair assessment of magufuli, which by any means reflects his inability to lead not only a country, but even a political party!
 
Mh Rais, pole kwa mihangaiko ya kupiga kampeni ila nina neno moja juu yako usiku Waleo nalo ni siri japo sio Siri baada yakuandika hapa.

Hali inayoendelea hata tukiwa wanafiki na kuwa tumekunywa maji ya bendera mwisho pumzi zitakata na zikikata mashambulizi yatakuwa makali zaidi kuliko wakati huu tuna nguvu.

Asikudanganye mtu, hali sio hali, yani hata kama ni kwa goli la mkono, ila mtiti huu utakusumbua katk awamu yako ya pili kiasi utahisi kila mtu ni msaliti.

Kuna hali sio ya kawaida huku uraiani, yani watu wamejawa na machungu kiasi hawana pa kupumulia ila tu 28.10.2020.

Majeshi na idara za usalama hawatoweza kudhibiti hili vuguvugu na wakiweza basi watu wengi watakuwa silence jambo litazidi kuibuwa vuguvugu jingine baya zaidi, jambo litazigawa idara zako za ushauri.

Uongozi ni kuacha alama na ili ufanikiwe kubali yaishe, kaa na waliokuweka vua urais wako omba ushauri Ila kumbuka shida ipo nyingine Nani wakukupa honest feedback kwa aina ya uongoz wako mkali sana Mzee wangu hapa tafuta MTU tu akusaidie upewe honest feed back japo sijui kama utaipata Mungu akusaidie.

Pamoja umefanya yote mazuri Ila trust me umeshindwa ishi mioyoni mwa Watanzania. Embu jiulize why? Umeme umetadanza kama uyoga, maji kama yote, mahospitali kama yote, madege, reli.

Yani hakuna mahali hujagusa, umefanya mambo makubwa sana ila umeshindwa kula na kipofu, sasa kipofu kapata kipofu aliewahi kuona hapo zamani Ila baadae akawa kipofu. Amewaambia vipofu wenzake huko sio, hiyo njia sio, wamemwamini ani ni shida ukiweka Jiwe na Magi watu wanapigia Kura Jiwe. Why umesahau wakolon walitupa shanga Sisi tukawapa madini?

Ona sasa mziki huu jamaa Hana bango Hana vyombo vya habari Ila ameteka nchi kweupe.

Waite wazee wakushauri maana najuwa uchaguzi huu hautokuwa Rahisi kama tunavyodhani.
Things have gone out of hand already
 
Back
Top Bottom