Dkt. Mollel: Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote itatangazwa kuanza kutumikia April hii 2024 kwa tarehe itakayotajwa!

Dkt. Mollel: Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote itatangazwa kuanza kutumikia April hii 2024 kwa tarehe itakayotajwa!

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Naibu waziri wa Afya Dr Mollel amesema Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote itaanza kutumikia mwezi huu wa April 2024 katika tarehe itakayopangwa

=====

1712149754611.png

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel amesema kuwa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote itatangazwa kuanza kutumika kabla ya Mwisho wa Mwezi wa Nne Mwaka 2024 kwa tarehe itakayotajwa.

Dkt. Mollel amebainisha hayo leo kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 15 na kikao cha kikao cha pili wakati akijibu swali Namba 27 kutoka kwa Mbunge wa Viti Maakum Mhe. Furaha Ntengo Matondo aliyeuliza Je, lini Bima ya Afya kwa Watu Wote itaanza kutumika.

Dkt. Mollel amesema Serikali imeanza maandalizi ya kuanza kutumika kwa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ambapo kwa Mujibu wa Kifungu cha 1 cha Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote Waziri anaweza kuteua Baadhi ya Vifungu vya kuanza kutumika.

“Baadhi ya Vifungu ambavyo vinaweka Mifumo imara ya kutekeleza Bima ya Afya kwa Wote vimeshaainishwa na kuwasilishwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Sheria itatangazwa kuanza kutumika kabla ya Mwisho wa Mwezi wa Nne Mwaka 2024 kwa tarehe itakayotajwa”, ameeleza Dkt. Mollel.

Dkt. Mollel amesema kuwa serikali imeshaainisha vyanzo vitakavyo hudumia watu wasio kuwa wa uwezo wakiwemo wajane na watoto wa mitaani.

Source: Clouds TV
 
Wamesharekebisha kitita chao upande wa dawa ama wanataka kuwatapeli wananchi?
Hao ni matapeli wala hawajarekebisha kitita chao.watakuja na swaga kama za CAG ati wastaafu na wenza wao ndio wanaufirisi mfuko.hawasemi Mikopo ya serikali na watumishi wa mfuko na wenza wa viongozi
 
Naibu waziri wa Afya Dr Mollel amesema Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote itaanza kutumikia mwezi huu wa April 2024 katika tarehe itakayopangwa

Source: Clouds TV
Hii kitu IMEFELI kabla haijaanza au kisayansi tunasema ni ectopic.

Kama wameshindwa kutoa huduma nzuri kwa watu 10% ya Watanzania ambao wamejiandikisha mpaka sasa, je wataweza nchi nzima?

Ni sawa na gari ya IST kuvuta semi traillor
 
Hii kitu IMEFELI kabla haijaanza au kisayansi tunasema ni ectopic.

Kama wameshindwa kutoa huduma nzuri kwa watu 10% ya Watanzania ambao wamejiandikisha mpaka sasa, je wataweza nchi nzima?

Ni sawa na gari ya IST kuvuta semi traillor
Dr Mollel: Wajane watapewa Bima Bure
 
Screenshot_20240413-191433.png


Mnakumbuka alichokisema Shabiby? Au mko bize na mambo ya umbea?
Screenshot_20240413-191900.png


Niendelee kuwakumbusha ama nowaache na umbea wenu?
 
Mapato yatokanayo na mitandao ya simu, mabenki na makusanyo\kodi nyingine nyingi ndodo ndogo, unaweza kuta ndizo zinazoendesha Nchi.
 
Back
Top Bottom