#COVID19 Dkt. Mwigulu: Chanjo ya Corona itakayotumika Tanzania itakuwa sawa na ile inayotumika Marekani

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Waziri wa fedha Dkt. Mwigulu Nchemba amesema kipaumbele namba moja cha Rais Samia ni afya za Watanzania hivyo chanjo ya Corona itayotumika Tanzania itakuwa sawa na ile iliyoidhinishwa na Ikulu ya Marekani kwa ajili ya kuwachanja Wamarekani.

Chanzo: ITV habari

Nawasalimu kwa jina la JMT!
 
Walete katiba ya marekani pia
 
Obviously haiwezi kuwa sawa, yaani wewe una per capita GDP below $1,500 unataka kuwa sawa na mwenye per capital above $ 80,000 ??

Ushaona wapi wa kula dagaa akakaa meza moja na mla nyama ya kuku?
Usikariri bwashee!
 
Neno "sawa" limetumika kuashiria kitu gani? Itakuwa sawa kwa namna gani?

Itakuwa sawa na chanjo ipi? Maana Marekani ina chanjo nyingi.

Tanzania imepewa ama itapewa leseni ya uzalishaji? Ama itanunua dozi zilizokwisha zalishwa?
 
Neno "sawa" limetumika kuashiria kitu gani? Itakuwa sawa kwa namna gani?

Itakuwa sawa na chanjo ipi? Maana Marekani ina chanjo nyingi.

Tanzania imepewa ama itapewa leseni ya uzalishaji? Ama itanunua dozi zilizokwisha zalishwa?
Sawa katika kipaumbele!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…