ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 66,537
- 75,687
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hayo yameelezwa na KM wa CCM Dkt.John Nchimbi wakati wa ziara yake ya Mikoa 6 akiwa Njombe.
DK Nchimbi ameonekana kushangazwa na kufurahishwa na Wingi wa miradi na maendeleo yaliyofanyika na yanayoendelea kufanyika akisema ni kama miujiza maana kilichotakiwa kufanyika Kwa muda mrefu kimewezekana ndani ya mda mchache kabisa.
Kwa wasio fahamu,haters na wabishi hii hapa ni summary tuu ya kilichofanywa na Samia.👇👇
1-Mapato ya TRA kuongezeka kutoka wastani wa 1.5T Hadi 2.2T(ongezeko bil.700 )
2-Makusanyo ya Halmashauri kuongeza kutoka Bil.800 Hadi Trilioni 1.2(Ongezeko Bil.400)
3-Ongezeko la Mapato ya Utalii Hadi 3.5T(Watalii 1.9m) kutoka 3T(Watalii 1.5mln).
4-Ujenzi wa Bandari Ziwa Nyasa(MbambaBay),Ziwa Tanganyika(Kigoma),Ziwa Victoria (Mwanza,Bukoba,Chato) na Bhari ya Hindi(Dar,Tanga,Kilwa na Mtwara).
5-Ujenzi wa viwanja wa ndege 15 Unaendelea Tanzania nzima eg Sumbawanga,Tabora,Shinyanga,Kigoma,Ruaha NP,Nyerere NP,Moshi,Iringa nk huku akikamilosja viwanja vya Songwe, Songea,Iringa na Katavi.
6-Ujenzi wa Hospital za Wilaya mpya 129 ,Mikoa 7 na Rufaa za Kanda 3(Mtwara,Kigoma na Ukerewe).
7-Ujenzi wa Vituo vya Afya vipya 402 kwenye kata za kimkakati hapo tozo za miamala (234).
8-Ununuzi wa vifaa tiba ambavyo havikuwahi kuwepo Kwenye hospital za Tanzania mfano Ultra Sound 192 ,Digital X-rays 147,CT Scan 32,MRI machines 7.
9-Ujenzi wa majengo ya Wagonjwa Mahututi(ICU) 28 na Dharula 127,
10-Upanuzi na Ujenzi wa Vyuo Vikuu vipya na kampasi za Vyuo kwenye Mikoa 14 ambayo swali haikuwa na Vyuo Vikuu au kampasi eg Kigoma,Simiyu,Njombe,Ruvuma, Rukwa,Katavi,Shinyanga,Lindi,Mtwara nk.
11-Kaongeza Bajeti Kila Wizara ila Kwa upekee ni Wizara ya Kilimo(Umwagiliaji )kutoka Bil.270 Hadi Bilioni 950.Skimu Mpya za uwamwagiliaji hectare 95,000 zimejengwa na kufufuliwa,kafungua ofisi za Kilimo Kila Wilaya na kaajiri Wataalamu na kawapa vitendea kazi.
12-Kaondoa shida ya vitambulisho NIDA,zaidi ya vitambulisho 12,000,000 vimegawiwa.
13-Ujenzi wa minara mipya 1,200 ambapo Kupitia mradi wa Tanzania ya Kidijitali minara 728 inaendelea na Ujenzi Kwa Bilioni 126.(Kijijini kama mjini)
14-Amefikisha maji ya Bomba Kwa zaidi ya Vijiji 11,000.(Kampeni ya kumtua Mama ndio kichwani).
15-Amefikisha umeme Kila Kijiji,kazi inaendelea kwenye vitongoji na migodi ya umeme.
16-Amewasha Umeme gridi ya Taifa Mikoa Kigoma,Katavi na kazi zinaendelea Rukwa ,Lindi, Mtwara.
17-Kazi zinaendelea ujenzi wa Vyanzo vipya vya Umeme eg Mto Malagalasi,Kakono,Umeme Jua Kishapu,Joto Ardhi Mbeya nk
18-Amejenga zaidi ya Shule Mpya za Sekondari 3,200 ,shule za msingi zaidi ya 300 na madarasa 24,000 ,mabweni 137 nk
19-Kupitia TanRoads amekamilisha zaidi ya km 1,000 za lami na zingine zaidi ya 3,700 zinaendelea na Ujenzi.
20-Kupitia Tarura amejenga zaidi ya km 800 za lami na zingine zaidi ya 500 zinaendelea na Ujenzi (Hapa amefungua maelfu ya Vijijini Kwa Barabara Mpya za changarawe na madaraja). Bajeti ya Tarura aliongeza kutoka bil.270 Hadi Bil.800.
21-Sekta ya mifugo amegawa Boti za Kisiasa zaidi ya 200 na viximba zaidi ya 1300 Kwa Vijana.
22-Sekta ya Elimu kaongeza mikopo Kwa wanafunzi ambapo Sasa Diploma Hadi Chuo Kikuu wanapata,chekechea Hadi form six Elimu Bure(kafuta ada ya form Six),Kafuta Mapenato na mambo ya hivyo ya Bodi ya Mikopo.
23-Katoa Ajira zaidi ya 55,000 kada zote huku Elimu na Afya wakipewa kipaombele.
24-Anajenga na kukamilisha zaidi ya miradi ya maji 3,700 mikubwa Kwa midogo mfano mradi wa Miji 28,bwawa la kidunda na kukwamua miradi iliyokwamba kama same-mwanga,Tarime-Kiabakari nk.
25-Kwenge sekta ya biashara baada ya maboresho maelfu ya miradi imemenika Kila sekta baada ya Wafanyabiashara kurejesha Imani Kwa Serikali Kupitia sera ya Diplomasia ya Uchumi na kuifungua Nchi.Hakuna ziara ambayo mama alifanya Nje ya Nchi hajakutana na Wafanyabiashara wa Kimataifa.
26-Sekta ya michezo na Burudani.Huko Kila mtu anajua kwamba Mama alikatabati viwanja,akaleta ufunguzi wa AFL na sasa ameileta Afcon 27 na uwanja Mpya inajengwa Arusha.Likewise kuwapa mikopo Wasanii.
27-Ujenzi wa Vyuo vya Ufundi Stadi (VETA) 100 .Lengo Kila Wilaya na Mkoa iwe na Chuo Cha ufundi.
28-Kaongeza Boom Kutoka 8,500 Hadi 10,000
29-Amefufua sekta ya Nyumba ilivyokuwa imekufa
30-Amefungua Uchumi,Watalii na Biashara Vinamiminika mfano ni kuzinduliwa Kwa viwanda vya Vioo,magari na mbolea.
Kiufupi ni vigumu kuelezea vyote,pamoja na Changamoto ila Mama kaupiga mwingi ,Anatosha na Chenji inabakia.
View: https://www.instagram.com/p/C59CY7uMJC5/?igsh=MTNiYnozM2hubjMwZQ==
My Take
Yote hayo kafanya na anaendelea kufanya lakini hajawahi acha mradi hata 1 aliourithi kutoka Kwa Mwendazake kama Bwawa la JNHPP,Daraja la JPM,EACOP,SGR,Ndege Mpya,Ujenzi wa Mji wa Serikali na hajatoa visingizio.
Au siyo?Acha kuropoka wewe Sukuma gang,sijaweka mradi hata mmja wa Mwendazake au umeona nimetaja Sgr na bwawa hapo?85% ya hayo uliyiyata hapo juu ni Miradi iliyoanzishwa na Magufuli.....
Kuanzia Hospital,Shule,Mahakama,Bandari hadi Viwanja vya ndege ni miradi ambayo ilisha sainiwa na kuanza katika awamu ya Magufuli.
Uko sahihi kabisa chief ndio maana miradi yote imesimama 😂😂👇👇Ameshindwa kuwalipa wazabuni
Anakopa mpaka anadhalilika
Huku street vijana wamekata tamaa mpaka wachoms picha yake
Au siyo?Acha kuropoka wewe Sukuma gang,sijaweka mradi hata mmja wa Mwendazake au umeona nimetaja Sgr na bwawa hapo?
Miradi aliyoanzisha Magufuli 😂😂😂👇👇
View: https://youtu.be/s9KmFmsFr5c?si=5U2PjvNaFjNEc08q
My Take: Bado hamjasema Hadi mseme.👇👇
View: https://twitter.com/TZMsemajiMkuu/status/1810568327422444000?t=0KmrDjQ8NuTTHnDfk4wtyQ&s=19
Au siyo?Acha kuropoka wewe Sukuma gang,sijaweka mradi hata mmja wa Mwendazake au umeona nimetaja Sgr na bwawa hapo?
Miradi aliyoanzisha Magufuli 😂😂😂👇👇
View: https://youtu.be/s9KmFmsFr5c?si=5U2PjvNaFjNEc08q
My Take: Bado hamjasema Hadi mseme.👇👇
View: https://twitter.com/TZMsemajiMkuu/status/1810568327422444000?t=0KmrDjQ8NuTTHnDfk4wtyQ&s=19
Nawewe nitajie 5 Mojor construction ambazo ni mawazo ya awamu ya 5..Sema Kwakuwa ujenzi siyo fani yako sishangai kama haujui hivyo....
Taja 5 major construction projects ambazo ni mawazo ya awamu hii na imeanza utekelezaji....mitano tu.
Okie kabla ya Magufuli hajawa Rais ,hayo yote uliyotaja hayakuwepo?Hiyo miradi yote hapo juu -ilianzishwa na Magufuri na ilishatiwa saini....
- Ujenzi na Ukarabati wa viwanja vya ndege
- Ujenzi wa hospitali za Wilaya
- Ujenzi wa stendi za MABASI ya mikoani.
- Ujenzi na ukarabati shule za Advance
- Upanuzi wa Bandari za Bahari
- Upanuzi wa Bandari za Ziwani
- Ujenzi wa Bandari kavu I.e Kwara
- Ujenzi wa One stop border posts katika mipaka
- Ujenzi wa Mahakama za Wilaya nchi nzima.
- Ujenzi wa Ofisi za NIDA katika kila Wilaya
- Ujenzi wa Mabwawa ya kufua Umeme Rufiji na kule Kagera.
- Ujenzi wa vituo vya kuuzia madini kila mkoa.
- Ujenzi wa Mwendokasi Phase ya 2 ,3 na 4
- Masoko makubwa ya mikoa
- Masoko makubwa jijini Dar.
- Madaraja makubwa ya Kigongo busisi,Wami na Tanzanite.
- Flyovers zote
- Vivuko vya barabarani pale Kawe bondeni,Buguruni na Furahisha.
- Meli
- Vivuko vya Ziwani na mtoni.
Wewe Kejeli na hata utusi...lakini huo ndiyo ukweli...
Wakati wewe unakaa na kuishia kukaa kwenye Kompyuta,siye tunakuwa site....
Mkuu nimekutajia miradi zaidi ya ishirini....siyo mawazo bali ilisainiwa na kuanza kutekelezwa....Nawewe nitajie 5 Mojor construction ambazo ni mawazo ya awamu ya 5..
Pili mawazo sio hela, Nyerere alianza kuwaza tangu anapata uhuru ila vitu ndio vinafanyika Sasa hivi.
Mwisho aliyekwambia sio fani yangu ni nani? Kwenye List hapo Juu umeona ni miradi ya ujenzi pekee?
Wewe ni mbumbumbu eti? Nitajie mradi specific uliosainiwa awamu ya 5 na inatekelezwa awamu ya 6?Mkuu nimekutajia miradi zaidi ya ishirini....siyo mawazo bali ilisainiwa na kuanza kutekelezwa....
Nimekwambia taja miradi 5 mikubwa ya ujenzi ambayo imekuwa initiated na awamu hii na kuanza ujenzi....mitano tu....
Miradi yote imeanza kujengwa na awamu ya tano....Okie kabla ya Magufuli hajawa Rais ,hayo yote uliyotaja hayakuwepo?
Nitajie mmja tuu wa hiyo miradi ambayo ilitiwa saini na uweke ushahidi hapa.
Mwisho Kwa nini haikufanyika awamu ya 5 badala yake ije ifanyike awamu ya 6? Kwa nini Bwawa la Nyerere halikujengwa awamu ya Mwalimu likaja kujengwa awamu ya 5 na 6? Leta majibu
Mada yangu umeielewa? Ndio maana umeshindwa kujibu maswali yangu hapo Juu unarukia rukia ujinga wako,achukiwe Kwa Ajili ya nini? 😂😂Miradi yote imeanza kujengwa na awamu ya tano....
Yani hata mjamaa achukiwe kiasi gani lakini alitenda kwa vitendo....siyo lazima mpaka mtu...
Hata hilo Jiji la Dodoma unalo lisifia kila siku Magufuli ndiyo kaanzisha ujenzi.
Mama kaikutana apongezwe kwa kuimalizia.