Dkt. Philip Mpango: Vijana kama wazazi wenu wapo hai watunzeni

Dkt. Philip Mpango: Vijana kama wazazi wenu wapo hai watunzeni

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango amewataka vijana nchini waliobahatika kuwa na wazazi walio hai kujenga utamaduni wa kuwatunza, kuwalea na kuwaonyesha upendo akimtaja mzazi kama kiungo muhimu katika familia na wakili wa Mwenyezi Mungu hapa duniani.

Dkt Mpango ameyasema wakati wa ibada ya misa ya mazishi ya mama wa Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Prof Adolf Mkenda,Bi Sekunda Massawe (82), misa iliyofanyika kanisa katoliki la Mtakatifu Pius wa X, Parokia ya Tarakea, wilaya ya Rombo, Mkoani Kilimanjaro.

Mama Sekunda, ambaye alifariki Januari 30, mwaka huu akisumbuliwa na ugonjwa wa saratani, amezikwa katika makaburi ya familia yaliyopo katika Kijiji cha Mbomai Juu, kata ya Tarakea Motamburu, wilayani hapa.
Screenshot 2025-02-07 144450.png
 
Hakuna binadamu mwenye akili timamu asiye penda hayo yaliyo semwa na muheshimiwa lakini tatizo ni hali ya uchumi.
 
Lakini yupo sahihi nadhani
Huyu bwana hanaga majukum kabisa..leo ataamka na mabadiliko ya tabia nchi..kesho paroko ilimradi tu tujue yupo ila all in all Makamu wa rais yupo yupo tu kwa kua katiba imetamka hivyo
 
Huyu bwana hanaga majukum kabisa..leo ataamka na mabadiliko ya tabia nchi..kesho paroko ilimradi tu tujue yupo ila all in all Makamu wa rais yupo yupo tu kwa kua katiba imetamka hivyo
kwamba kikubwa ofisi imejazwa ...wabongo!
 
Back
Top Bottom