Dkt. Samia, Mchumi aliyehitajika kukinusuru kilimo na kuwafuta machozi wakulima

Dkt. Samia, Mchumi aliyehitajika kukinusuru kilimo na kuwafuta machozi wakulima

FPT

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2017
Posts
1,216
Reaction score
1,848
Kilimo ni uti wa mgongo wa taifa ketu ambapo kilimo pekee kimeweza kutoa ajira kwa 70%. Kilimo ni biashara kwa sababu mkulima anaweza kuuza mazao anayolima kibiashara na kumtengenezea kipato. Na zaidi kilimo kinachangia 27% katika Pato la taifa.

Kwa kipindi kirefu kilimo kimeshindwa kwa namna au nyingine kumheshimisha mkulima lakini kipindi hiki Dkt.Samia amekipeleka kilimo kwenye viwango vya juu sana. Katika hili, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni..

Kinavyozungumzwa kilimo ni vema yakaangaliwa maslahi na changamoto za wakulima kwa kuwa ndipo tutajua vilio na vicheko vya wakulima. Ningependa kuangalia upande wa changamoto na namna zilivyofanywa fursa za kumnufaisha mkulima.

Changamoto kuu zinazosemwa sana na wakulima ni ukosefu wa pembejeo(mbolea), ukosefu wa masoko na Bei za mazao kuwa chini, sio tu serikali imezitatua bali sasa kilimo kinafanyika kiushindani na kibiashara zaidi. Hii ni kuonesha ni kwa namna gani Dkt. Samia kadhamiria kukipaisha.

Serikali ya Dkt. Samia imepanga kukuza mauzo ya nje yatokanayo na kilimo kutika dola za kimarekani bilioni 1.2 mpaka kufikia dola bilion 5 mwaka 2030 na hapa serikali imeonesha ni kwa namna gani itavyohakikisha inaboresha kilimo kuweza kumnufaisha mkulima.

Kwa upande wa changamoto, nikianza na changamoto ya ukosefu wa pembejeo(mbolea) serikali katika Mwaka wa fedha 2022/2023 imetenga kiasi Cha shilingi bilion 150 kwa ajili ya kutoa ruzuku kwa mazao yote ya kilimo. Hiki ni kiwango kikubwa sana. Pia, serikali imedhibiti Bei ya mbolea ya kupandia kutoka 140,000 hadi 70,000 na mbolea za kukuzia kutoka 110,000 hadi 70,000 hii itasaidia wakulima kujikitika kwenye kilimo cha kisasa na kupata mazao mengi zaidi.

Changamo nyingine ambayo ni ukosefu wa masoko, serikali imerahisisha utolewaji wa vibali vya kusafirisha mazao nje hivyo wakulima wataweza kuuza mazao yao nje kwenye masoko ya uhakika. Pia, Serikali imerahisisha na kuboresha utambuzi wa masoko ya kimkakati kwa kushirikiana na shirika la chakula na kilimo duniani(FAO) ambapo wauzaji na wanunuaji hukutana. Uwepo wa masoko haya ya kimkakati unasaidia kukuza fursa za uwekezaji kwenye kilimo. Mfano wa masoko hayo ni soko la kibaigwa mkoani Dodoma.

Pia, katika hili la ukosefu wa masoko Serikali kupitia Mamlaka ya Afya ya mimea na viuatilifu(TPHPA) imepata cheti Cha ithibati ya kimataifa ambacho kitasaidia bidhaa kutoka nchini kutambulika kimataifa. Hii itasaidia mazao ya kilimo kupata masoko nje na kumsaidia mkulima moja kwa moja.

Changamoto nyingine ya Bei za mazao kuwa chini, hapa ndipo kilio Cha wakulima kwa muda mrefu kilikuwepo. Bei ni kichocheo kikubwa katika uwekezaji na Bei ya vyakula kupanda ni fursa na kukuza kilimo. Kilio hiki kimepata mfutaji machozi na Dkt. Samia amefanikisha ndoto ya mkulima kunufaika kutokana na kilimo kutimia. Kwa mtazamo wangu, kupanda kwa Bei ya mazao ya kilimo na vyakula sio mfumuko wa Bei ila ni kupanda kwa thamani ya kilimo.

Twendeni mbele turudi nyuma, Mhe.Rais Dkt.Samia amefanya mambo makubwa na mazuri kwenye sekta ya kilimo. Wakulima wanafuraha sana kipindi na ninaamini kilimo kitaajiri watu wengi zaidi kukiendelea kuwa na maboresho kwenye ya kilimo.

Tumuite mama shujaa wa kilimo lakini Mimi namuona Dkt Samia kama mchumi aliyehitajika sana kukinusuru kilimo na kuwafuta machozi wakulima.
 
Kilimo cha kutegemea jembe la mkono na mvua zisizo tabirika kwenye karne hii ya 21, nacho ni cha kupongezana!

Kisa tu mmetoa vimbolea vyenu vya ruzuku, basi hatunywi maji!!
 
Changomoto kuu ya kilimo ni miondombinu ya barabara na umwagiliaji.
Nyingine zote ni siasa tu zinazoweza kubadilika na wakati.
 
Peleka barabara za lami kote vijijini kuhakikisha wakulima wanasafirisha pembejeo na mazao yao kwa uhakika kwa gharama nafuu na jenga miundombinu ya umwagiliaji kuhakikisha wakulima wanaweza kulima bila kutegemea mvua. Matatizo mengine yote yaliyobaki ni sawa na kachumbari tu kwenye pilau.
 
Peleka barabara za lami kote vijijini kuhakikisha wakulima wanasafirisha pembejeo na mazao yao kwa uhakika kwa gharama nafuu na jenga miundombinu ya umwagiliaji kuhakikisha wakulima wanaweza kulima bila kutegemea mvua. Matatizo mengine yote yaliyobaki ni sawa na kachumbari tu kwenye pilau.
Miundombinu ya umwagiliaji huwezi kuweka kila mahali kutokana na kwamba umwagiliaji unafayika sehemu zenye vyanzo vya maji vya uhakika kama mito, mabwawa na maziwa ,maeneo yasiyo na vyanzo vya maji vya uhakika sio rahisi kufanyika.

Pia, gharama za kutengeneza skimu za umwagiliaji na papo hapo hata uwe na skimu bado mbolea itatumika.

Bado inabidi tukubali kilimo cha
 
Tatizo la sekta ya kilimo kwa Tanzania ni kuwa watu wengi sana wapo kwenye kilimo.

Tukiwa hivi hatuwezi kuendelea. hamna nchi yenye watu asilimia 67 wapo kwenye kilimo ikaendelea.

Tuwatoe watu kutoka kwenye kilimo kwa kadri ya uwezo wetu na tuwaachie watu wachache wenye mitaji mikubwa ardhi walime.
 
Nakuunga mkono asilimia mia, huwa najiuliza maswali mengi sipati majibu, yaani kilimo kimeajiri 70% ya Watanzania wote, pili 27% ya pato la Taifa hutokana na kilimo lakini viongozi huwa hawakipi tention!

JK alikuja na mpango wa Kilimo kwanza yakanunuliwa matrekta kibao badae ikapotea sijui ilienda wapi!

Na kwa nchi, Rais atakayeikwamua nchi kutoka ilipo hadi uchumi wa kila mtu ni yule pekee atakayejikita katika kilimo!

Samia anaonesha njia nzuri tumuunge mkono! Nimeenda Ukraine na nikafanikiwa kuyatembelea mashamba yao ya ngano...aisee unaweza ukalia.. Sisi tuna ardhi kubwa sana lakini......
 
Kilimo ni uti wa mgongo wa taifa ketu ambapo kilimo pekee kimeweza kutoa ajira kwa 70%. Kilimo ni biashara kwa sababu mkulima anaweza kuuza mazao anayolima kibiashara na kumtengenezea kipato. Na zaidi kilimo kinachangia 27% katika Pato la taifa.

Kwa kipindi kirefu kilimo kimeshindwa kwa namna au nyingine kumheshimisha mkulima lakini kipindi hiki Dkt.Samia amekipeleka kilimo kwenye viwango vya juu sana. Katika hili, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni..

Kinavyozungumzwa kilimo ni vema yakaangaliwa maslahi na changamoto za wakulima kwa kuwa ndipo tutajua vilio na vicheko vya wakulima. Ningependa kuangalia upande wa changamoto na namna zilivyofanywa fursa za kumnufaisha mkulima.

Changamoto kuu zinazosemwa sana na wakulima ni ukosefu wa pembejeo(mbolea), ukosefu wa masoko na Bei za mazao kuwa chini, sio tu serikali imezitatua bali sasa kilimo kinafanyika kiushindani na kibiashara zaidi. Hii ni kuonesha ni kwa namna gani Dkt. Samia kadhamiria kukipaisha.

Serikali ya Dkt. Samia imepanga kukuza mauzo ya nje yatokanayo na kilimo kutika dola za kimarekani bilioni 1.2 mpaka kufikia dola bilion 5 mwaka 2030 na hapa serikali imeonesha ni kwa namna gani itavyohakikisha inaboresha kilimo kuweza kumnufaisha mkulima.

Kwa upande wa changamoto, nikianza na changamoto ya ukosefu wa pembejeo(mbolea) serikali katika Mwaka wa fedha 2022/2023 imetenga kiasi Cha shilingi bilion 150 kwa ajili ya kutoa ruzuku kwa mazao yote ya kilimo. Hiki ni kiwango kikubwa sana. Pia, serikali imedhibiti Bei ya mbolea ya kupandia kutoka 140,000 hadi 70,000 na mbolea za kukuzia kutoka 110,000 hadi 70,000 hii itasaidia wakulima kujikitika kwenye kilimo cha kisasa na kupata mazao mengi zaidi.

Changamo nyingine ambayo ni ukosefu wa masoko, serikali imerahisisha utolewaji wa vibali vya kusafirisha mazao nje hivyo wakulima wataweza kuuza mazao yao nje kwenye masoko ya uhakika. Pia, Serikali imerahisisha na kuboresha utambuzi wa masoko ya kimkakati kwa kushirikiana na shirika la chakula na kilimo duniani(FAO) ambapo wauzaji na wanunuaji hukutana. Uwepo wa masoko haya ya kimkakati unasaidia kukuza fursa za uwekezaji kwenye kilimo. Mfano wa masoko hayo ni soko la kibaigwa mkoani Dodoma.

Pia, katika hili la ukosefu wa masoko Serikali kupitia Mamlaka ya Afya ya mimea na viuatilifu(TPHPA) imepata cheti Cha ithibati ya kimataifa ambacho kitasaidia bidhaa kutoka nchini kutambulika kimataifa. Hii itasaidia mazao ya kilimo kupata masoko nje na kumsaidia mkulima moja kwa moja.

Changamoto nyingine ya Bei za mazao kuwa chini, hapa ndipo kilio Cha wakulima kwa muda mrefu kilikuwepo. Bei ni kichocheo kikubwa katika uwekezaji na Bei ya vyakula kupanda ni fursa na kukuza kilimo. Kilio hiki kimepata mfutaji machozi na Dkt. Samia amefanikisha ndoto ya mkulima kunufaika kutokana na kilimo kutimia. Kwa mtazamo wangu, kupanda kwa Bei ya mazao ya kilimo na vyakula sio mfumuko wa Bei ila ni kupanda kwa thamani ya kilimo.

Twendeni mbele turudi nyuma, Mhe.Rais Dkt.Samia amefanya mambo makubwa na mazuri kwenye sekta ya kilimo. Wakulima wanafuraha sana kipindi na ninaamini kilimo kitaajiri watu wengi zaidi kukiendelea kuwa na maboresho kwenye ya kilimo.

Tumuite mama shujaa wa kilimo lakini Mimi namuona Dkt Samia kama mchumi aliyehitajika sana kukinusuru kilimo na kuwafuta machozi wakulima.
Yaani tuna hekta zaidi ya milioni 40 zinazofaa kwa kilimo alafu tunalima hekta 700 alafu unamsifu Samia kwa lipi?na hizo zinazolimwa kazikuta,yeye kaongeza hekta ngapi?
Kama tunataka Tanzania tuwe food basket ya Afrika na Dunia,inabidi angala 10%-30% ya bajeti ya nchi iende kwenye kilimo.Hapo ndiyo tutaweza kuwa na bajeti kubwa ya utafiti wa mbegu bora,huduma bora za ugani,Agro machineries and processing industries, Quality Irrigation systems,nk.
Sasa wewe icho Kilimo cha pinda mgongo kitatupeleka wapi?
Punguzeni uchawa kidogo basi,kha!
 
Kilimo ni uti wa mgongo wa taifa ketu ambapo kilimo pekee kimeweza kutoa ajira kwa 70%. Kilimo ni biashara kwa sababu mkulima anaweza kuuza mazao anayolima kibiashara na kumtengenezea kipato. Na zaidi kilimo kinachangia 27% katika Pato la taifa.

Kwa kipindi kirefu kilimo kimeshindwa kwa namna au nyingine kumheshimisha mkulima lakini kipindi hiki Dkt.Samia amekipeleka kilimo kwenye viwango vya juu sana. Katika hili, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni..

Kinavyozungumzwa kilimo ni vema yakaangaliwa maslahi na changamoto za wakulima kwa kuwa ndipo tutajua vilio na vicheko vya wakulima. Ningependa kuangalia upande wa changamoto na namna zilivyofanywa fursa za kumnufaisha mkulima.

Changamoto kuu zinazosemwa sana na wakulima ni ukosefu wa pembejeo(mbolea), ukosefu wa masoko na Bei za mazao kuwa chini, sio tu serikali imezitatua bali sasa kilimo kinafanyika kiushindani na kibiashara zaidi. Hii ni kuonesha ni kwa namna gani Dkt. Samia kadhamiria kukipaisha.

Serikali ya Dkt. Samia imepanga kukuza mauzo ya nje yatokanayo na kilimo kutika dola za kimarekani bilioni 1.2 mpaka kufikia dola bilion 5 mwaka 2030 na hapa serikali imeonesha ni kwa namna gani itavyohakikisha inaboresha kilimo kuweza kumnufaisha mkulima.

Kwa upande wa changamoto, nikianza na changamoto ya ukosefu wa pembejeo(mbolea) serikali katika Mwaka wa fedha 2022/2023 imetenga kiasi Cha shilingi bilion 150 kwa ajili ya kutoa ruzuku kwa mazao yote ya kilimo. Hiki ni kiwango kikubwa sana. Pia, serikali imedhibiti Bei ya mbolea ya kupandia kutoka 140,000 hadi 70,000 na mbolea za kukuzia kutoka 110,000 hadi 70,000 hii itasaidia wakulima kujikitika kwenye kilimo cha kisasa na kupata mazao mengi zaidi.

Changamo nyingine ambayo ni ukosefu wa masoko, serikali imerahisisha utolewaji wa vibali vya kusafirisha mazao nje hivyo wakulima wataweza kuuza mazao yao nje kwenye masoko ya uhakika. Pia, Serikali imerahisisha na kuboresha utambuzi wa masoko ya kimkakati kwa kushirikiana na shirika la chakula na kilimo duniani(FAO) ambapo wauzaji na wanunuaji hukutana. Uwepo wa masoko haya ya kimkakati unasaidia kukuza fursa za uwekezaji kwenye kilimo. Mfano wa masoko hayo ni soko la kibaigwa mkoani Dodoma.

Pia, katika hili la ukosefu wa masoko Serikali kupitia Mamlaka ya Afya ya mimea na viuatilifu(TPHPA) imepata cheti Cha ithibati ya kimataifa ambacho kitasaidia bidhaa kutoka nchini kutambulika kimataifa. Hii itasaidia mazao ya kilimo kupata masoko nje na kumsaidia mkulima moja kwa moja.

Changamoto nyingine ya Bei za mazao kuwa chini, hapa ndipo kilio Cha wakulima kwa muda mrefu kilikuwepo. Bei ni kichocheo kikubwa katika uwekezaji na Bei ya vyakula kupanda ni fursa na kukuza kilimo. Kilio hiki kimepata mfutaji machozi na Dkt. Samia amefanikisha ndoto ya mkulima kunufaika kutokana na kilimo kutimia. Kwa mtazamo wangu, kupanda kwa Bei ya mazao ya kilimo na vyakula sio mfumuko wa Bei ila ni kupanda kwa thamani ya kilimo.

Twendeni mbele turudi nyuma, Mhe.Rais Dkt.Samia amefanya mambo makubwa na mazuri kwenye sekta ya kilimo. Wakulima wanafuraha sana kipindi na ninaamini kilimo kitaajiri watu wengi zaidi kukiendelea kuwa na maboresho kwenye ya kilimo.

Tumuite mama shujaa wa kilimo lakini Mimi namuona Dkt Samia kama mchumi aliyehitajika sana kukinusuru kilimo na kuwafuta machozi wakulima.
Hivi mpiga debe wa daladala anaweza kuwasemea wavuvi? Hiki ulichoandika kwa maneno makali ni utumbo! Wewe hujui chochote kuhusu kilimo bora kukaa kimya! Masoko gani ya uhakika yaliyopo? Sera zipi zitawezesha kilimo biashara? Mwaka juzi serikali ikasisitiza kilimo cha alizeti ili nchi ijitegemee mafuta. Mwaka jana serikali ikatunga sheria kuingiza mafuta bila kodi. Alizeti imeshuka bei. Kwa vile mahindi yamepanda bei mwakali serikali itaagiza mahindi toka nje. Hawa watu ni bure kabisa.
Narudia kusema umeandika utumbo. Acha sisi wakulima tukwambie.
 
Kilimo ni uti wa mgongo wa taifa ketu ambapo kilimo pekee kimeweza kutoa ajira kwa 70%. Kilimo ni biashara kwa sababu mkulima anaweza kuuza mazao anayolima kibiashara na kumtengenezea kipato. Na zaidi kilimo kinachangia 27% katika Pato la taifa.

Kwa kipindi kirefu kilimo kimeshindwa kwa namna au nyingine kumheshimisha mkulima lakini kipindi hiki Dkt.Samia amekipeleka kilimo kwenye viwango vya juu sana. Katika hili, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni..

Kinavyozungumzwa kilimo ni vema yakaangaliwa maslahi na changamoto za wakulima kwa kuwa ndipo tutajua vilio na vicheko vya wakulima. Ningependa kuangalia upande wa changamoto na namna zilivyofanywa fursa za kumnufaisha mkulima.

Changamoto kuu zinazosemwa sana na wakulima ni ukosefu wa pembejeo(mbolea), ukosefu wa masoko na Bei za mazao kuwa chini, sio tu serikali imezitatua bali sasa kilimo kinafanyika kiushindani na kibiashara zaidi. Hii ni kuonesha ni kwa namna gani Dkt. Samia kadhamiria kukipaisha.

Serikali ya Dkt. Samia imepanga kukuza mauzo ya nje yatokanayo na kilimo kutika dola za kimarekani bilioni 1.2 mpaka kufikia dola bilion 5 mwaka 2030 na hapa serikali imeonesha ni kwa namna gani itavyohakikisha inaboresha kilimo kuweza kumnufaisha mkulima.

Kwa upande wa changamoto, nikianza na changamoto ya ukosefu wa pembejeo(mbolea) serikali katika Mwaka wa fedha 2022/2023 imetenga kiasi Cha shilingi bilion 150 kwa ajili ya kutoa ruzuku kwa mazao yote ya kilimo. Hiki ni kiwango kikubwa sana. Pia, serikali imedhibiti Bei ya mbolea ya kupandia kutoka 140,000 hadi 70,000 na mbolea za kukuzia kutoka 110,000 hadi 70,000 hii itasaidia wakulima kujikitika kwenye kilimo cha kisasa na kupata mazao mengi zaidi.

Changamo nyingine ambayo ni ukosefu wa masoko, serikali imerahisisha utolewaji wa vibali vya kusafirisha mazao nje hivyo wakulima wataweza kuuza mazao yao nje kwenye masoko ya uhakika. Pia, Serikali imerahisisha na kuboresha utambuzi wa masoko ya kimkakati kwa kushirikiana na shirika la chakula na kilimo duniani(FAO) ambapo wauzaji na wanunuaji hukutana. Uwepo wa masoko haya ya kimkakati unasaidia kukuza fursa za uwekezaji kwenye kilimo. Mfano wa masoko hayo ni soko la kibaigwa mkoani Dodoma.

Pia, katika hili la ukosefu wa masoko Serikali kupitia Mamlaka ya Afya ya mimea na viuatilifu(TPHPA) imepata cheti Cha ithibati ya kimataifa ambacho kitasaidia bidhaa kutoka nchini kutambulika kimataifa. Hii itasaidia mazao ya kilimo kupata masoko nje na kumsaidia mkulima moja kwa moja.

Changamoto nyingine ya Bei za mazao kuwa chini, hapa ndipo kilio Cha wakulima kwa muda mrefu kilikuwepo. Bei ni kichocheo kikubwa katika uwekezaji na Bei ya vyakula kupanda ni fursa na kukuza kilimo. Kilio hiki kimepata mfutaji machozi na Dkt. Samia amefanikisha ndoto ya mkulima kunufaika kutokana na kilimo kutimia. Kwa mtazamo wangu, kupanda kwa Bei ya mazao ya kilimo na vyakula sio mfumuko wa Bei ila ni kupanda kwa thamani ya kilimo.

Twendeni mbele turudi nyuma, Mhe.Rais Dkt.Samia amefanya mambo makubwa na mazuri kwenye sekta ya kilimo. Wakulima wanafuraha sana kipindi na ninaamini kilimo kitaajiri watu wengi zaidi kukiendelea kuwa na maboresho kwenye ya kilimo.

Tumuite mama shujaa wa kilimo lakini Mimi namuona Dkt Samia kama mchumi aliyehitajika sana kukinusuru kilimo na kuwafuta machozi wakulima.
Iko hivi Serikali inunue mahindi, maharage nk iweke kwenye magala. Wakati huo wanunue mazao hayo mapya na wananchi wasihangaike kutafuta wateja. Hivi nasikia bei ya nafaka kutoka kwetu kwenye nchi za Jirani ni ya chini kuliko hapa. Nilishindwa kujitetea kwa bei ya nafaka kuwa ya chini HUKO. Nilichogundua WAKULIMA WANAPIGWA SANA YAANI MAZAO WANAUZIA WALANGUZI KWA BEI YA CHINI SANA NDIO SABABU BEI IKO CHINI YANAKOPELEKWA.
 
Alizeti ni zao mhimu ila linakufa. Korosho nazo ni changa la moto.
 
Kilimo cha kutegemea jembe la mkono na mvua zisizo tabirika kwenye karne hii ya 21, nacho ni cha kupongezana!

Kisa tu mmetoa vimbolea vyenu vya ruzuku, basi hatunywi maji!!
Hata kukiwa na skimu za umwagiliaji kama masoko ya uhakika hakuna ,Bei za mazao ziko chini na upatikanaji wa pembejeo sio wa hakika bado mkakati wa kukuza na kuinua kilimo utakuwa hauna tija.

Ni budi tuipongeze serikali kwa hatua hizi za awali za kukusa kilimo na kumsaidia mkulima.
 
Hivi mpiga debe wa daladala anaweza kuwasemea wavuvi? Hiki ulichoandika kwa maneno makali ni utumbo! Wewe hujui chochote kuhusu kilimo bora kukaa kimya! Masoko gani ya uhakika yaliyopo? Sera zipi zitawezesha kilimo biashara? Mwaka juzi serikali ikasisitiza kilimo cha alizeti ili nchi ijitegemee mafuta. Mwaka jana serikali ikatunga sheria kuingiza mafuta bila kodi. Alizeti imeshuka bei. Kwa vile mahindi yamepanda bei mwakali serikali itaagiza mahindi toka nje. Hawa watu ni bure kabisa.
Narudia kusema umeandika utumbo. Acha sisi wakulima tukwambie.
Sio tu kuingiza ndani( import) bali hata kutoa nje(export) kwa bidhaa za kilimo kumeondolewa baadhi ya Kodi ili kurahisisha upatikanaji wa bidhaa hizo.

Ndio maana nimesema Dkt. Samia ni mchumi aliyehitajika kukinusuru kilimo lakini kwa njia za kiuchumi. Wakulima wa alizeti Tanzania hawawezi kutosheleza mahitaji ya soko kwa sasa hivyo ili kuepusha scarcity na upandaji holela wa mafuta serikali kazi yake ni kufanikisha upatikanaji wa mafuta na sio kwamba yakiletwa ya nje ya hapa yatapungua sana Bei hapana.
 
Yaani tuna hekta zaidi ya milioni 40 zinazofaa kwa kilimo alafu tunalima hekta 700 alafu unamsifu Samia kwa lipi?na hizo zinazolimwa kazikuta,yeye kaongeza hekta ngapi?
Kama tunataka Tanzania tuwe food basket ya Afrika na Dunia,inabidi angala 10%-30% ya bajeti ya nchi iende kwenye kilimo.Hapo ndiyo tutaweza kuwa na bajeti kubwa ya utafiti wa mbegu bora,huduma bora za ugani,Agro machineries and processing industries, Quality Irrigation systems,nk.
Sasa wewe icho Kilimo cha pinda mgongo kitatupeleka wapi?
Punguzeni uchawa kidogo basi,kha!
Mpango wa serikali ni kukuza mauzo ya nje ya bidhaa za kilimo kutoka dola bilion 1.2 mwaka 2022 mpaka kufikia dola bilion 5 mwaka 2030 ambayo ni sawa na ongezeka la asilimia 400. Hivi kwa ongezeko hilo la mauzo unafikiri linaweza kufanyika kwenye shamba lenye ukubwa ule ule?
 
Nilichogundua WAKULIMA WANAPIGWA SANA YAANI MAZAO WANAUZIA WALANGUZI KWA BEI YA CHINI SANA NDIO SABABU BEI IKO CHINI YANAKOPELEKWA.
Ni wapi huko mkulima analanguliwa na ni mazao gani hayo!?

Mimi ni mkulima na kwa mara ya kwanza nimeonja ladha ya utamu wa kazi za mikono yangu baada ya miaka mingi.
Kitendo cha serikali kuruhusu soko kuamua bei kimekuwa faraja kubwa sana kwa mkulima.

Hii itakuwa hamasa kwa watu wengi haswa vijana wasomi kujiingiza kwenye kilimo.
Jambo ambalo litachochea mavuno kuongezeka na hao vijana kutumia elimu yao kusaka masoko mapya duniani....hayo yatakuwa ndiyo maendeleo na mapinduzi katika kilimo.
 
Tatizo la sekta ya kilimo kwa Tanzania ni kuwa watu wengi sana wapo kwenye kilimo.

Tukiwa hivi hatuwezi kuendelea. hamna nchi yenye watu asilimia 67 wapo kwenye kilimo ikaendelea.

Tuwatoe watu kutoka kwenye kilimo kwa kadri ya uwezo wetu na tuwaachie watu wachache wenye mitaji mikubwa ardhi walime.
Hapa kwetu kilimo ni mkombozi pale unapokuwa huna jengine la kufanya au unapostaafu, hawakusomea kilimo popote lakini ni kuamka asubuhi na kuamua leo mimi nitakuwa mkulima. Hao wanaoamua ndiyo wamestaafu wamechoka na maisha ati ndiyo wanakwenda kuwa wakulima. Aidha vijana wanakimbia vijijini kuja mjini kufanya shughuli zisizoeleweka alimradi wamekimbia kilimo.

Wakulima hasa serious ni wachache.

Niliwahi kwenda nchi moja ya Scandinavia kwenye course moja ya kilimo na walituambia moja ya masharti yao ya kuwa mkulima basi lazima uwe umekwenda (enzi zile) course ya kilimo, bila ya hivyo huwezi kuruhusiwa kuwa mkulima.

Ni muda muafaka sasa angalau vijana wahamasishwe kujiunga na kilimo lakini kwanza wapewe mafunzo ya lile zao wanalotaka kulishughulikia ili kumfanya awe mkulima mzuri
 
Ni wapi huko mkulima analanguliwa na ni mazao gani hayo!?

Mimi ni mkulima na kwa mara ya kwanza nimeonja ladha ya utamu wa kazi za mikono yangu baada ya miaka mingi.
Kitendo cha serikali kuruhusu soko kuamua bei kimekuwa faraja kubwa sana kwa mkulima.

Hii itakuwa hamasa kwa watu wengi haswa vijana wasomi kujiingiza kwenye kilimo.
Jambo ambalo litachochea mavuno kuongezeka na hao vijana kutumia elimu yao kusaka masoko mapya duniani....hayo yatakuwa ndiyo maendeleo na mapinduzi katika kilimo.
Huko ambako mahindi na maharage yananunuliwa na kuuzwa kwa bei ya chini kuliko hapa. Nimekudokeza nawe ulizia kilo moja wanauziwa kwa bei gani KTK NCHI HIZO. UTASHANGAA
 
Yaani tuna hekta zaidi ya milioni 40 zinazofaa kwa kilimo alafu tunalima hekta 700 alafu unamsifu Samia kwa lipi?na hizo zinazolimwa kazikuta,yeye kaongeza hekta ngapi?
Kama tunataka Tanzania tuwe food basket ya Afrika na Dunia,inabidi angala 10%-30% ya bajeti ya nchi iende kwenye kilimo.Hapo ndiyo tutaweza kuwa na bajeti kubwa ya utafiti wa mbegu bora,huduma bora za ugani,Agro machineries and processing industries, Quality Irrigation systems,nk.
Sasa wewe icho Kilimo cha pinda mgongo kitatupeleka wapi?
Punguzeni uchawa kidogo basi,kha!
Well put.
Hawa ngamia wanajibebesha hoja wasizoweza hata kuzijibu. Siasa kilimo ya vimbolea viwili vitatu ndio sifa kedekede...adterall, zilikuwepo tangu hapo, zilikuwa zinpigwa na sasa zipo na zinapigwa vilevile.

Pathetic.
 
Back
Top Bottom