BWANKU M BWANKU
JF-Expert Member
- Jan 12, 2019
- 377
- 435
DKT. SAMIZI ACHANJA MBUGA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI NA KUHAMASISHA SENSA JIMBONI.
Leo imekuwa mwendelezo wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Muhambwe Mkoani Kigoma Mhe Dkt. Florence George Samizi ambaye ametembelea kwenye Stendi ya Halmashauri ya Kibondo na kuhamasisha Sensa ya watu na makazi inayofanyika Agosti 23 Mwaka huu ambapo akiwa hapo alipata nafasi pia ya kusikiliza kero na changamoto za Wananchi.
Pia ametembelea Shule ya Sekondari Muhambwe ambapo jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan zimewezesha kutoa Milioni 470 kufanya ukarabati shuleni hapo.
Kwenye Kata ya Kibondo Mjini pia ambayo haikuwa na Kituo cha Afya, Mhe Mbunge ametembelea Kituo cha Afya kinachojengwa ambacho Serikali ya Rais Samia imetoa Jumla ya Milioni 500 kufanikisha Ujenzi huo.
#Muhambwekaziinaendele
Leo imekuwa mwendelezo wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Muhambwe Mkoani Kigoma Mhe Dkt. Florence George Samizi ambaye ametembelea kwenye Stendi ya Halmashauri ya Kibondo na kuhamasisha Sensa ya watu na makazi inayofanyika Agosti 23 Mwaka huu ambapo akiwa hapo alipata nafasi pia ya kusikiliza kero na changamoto za Wananchi.
Pia ametembelea Shule ya Sekondari Muhambwe ambapo jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan zimewezesha kutoa Milioni 470 kufanya ukarabati shuleni hapo.
Kwenye Kata ya Kibondo Mjini pia ambayo haikuwa na Kituo cha Afya, Mhe Mbunge ametembelea Kituo cha Afya kinachojengwa ambacho Serikali ya Rais Samia imetoa Jumla ya Milioni 500 kufanikisha Ujenzi huo.
#Muhambwekaziinaendele