Dkt. Slaa Afuatiliwa na watu wasiojulikana kutoka Iringa hadi Dar Es Salaam

Dkt. Slaa Afuatiliwa na watu wasiojulikana kutoka Iringa hadi Dar Es Salaam

Confederate Spy

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2012
Posts
426
Reaction score
145
WANABODI,

Usalama wa viongozi wa chama kikuu cha upinzani Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) upo hatarini.Akiwa njia ni kutokea Iringa, Dr. Slaa amefuatiliwa na Gari aina ya Landcruiser yenye vioo vya giza (Tinted) lenye namba za usajili T963 ABN. Awali waliokua ndani ya gari la Dr. Slaa hawakushtuka sana japo waliona kuna mchezo wa gari hilo kuwapita kwa kasi na kisha kupunguza mwendo ghafla na kisha gari la Dr. Slaa kuwapita tena.Walichukulia kama vile ni mchezo wa kawaida hadi walipofika Morogoro na kushtuka zaidi na kuanza kuchukua tahadhari kwa kunakili namba ya gari hilo

Walipofika kibaha ilibidi watoe taarifa kwa askari wa usalama barabarani.

Dr. Slaa na maofisa wa chama akiwemo afisa habari walishtuka zaidi walipofika njia panda ya Tamko-Bunju ambayo mara nyingi hutumika kunapokua na foleni kubwa ya maghari(Traffic Jam) na kulikuta gari hilo likiwasubiri

Baada ya kufuata barabara kuingia jijini Dar Es Salaam gari hiyo ghafla ikaingia nyuma ya gari aliyokua akitumia Dr. Slaa aina ya Landcruiser yenye namba za usajili namba T834 BJG. Ndipo afisa wake aliyekua ndani ya gari akapanda juu (Roof Top) na kufanikiwa kulipiga picha gari hilo.

Kuona hilo likifanyika gari hilo likapaki pembeni na ghafla likaondoka na kupotea hadi muda huu walipoingia Ubungo.

Sasa katika mazingira haya taifa linaelekea wapi? Kama watu wanafuatiliwa na kufanyiwa vituko mchana kweupe usalama wa Watanzania na hasa wanaharakati na viongozi wa upinzani Tanzania uko wapi? Mambo haya ni bora yafahamike mapema na watanzania wayajue. Hili ni tukio lisilo la kawaida kipindi hiki ambacho umma umekosa imani (loose confidence) na vyombo vya dola vinavyotumika kwa matakwa ya kisiasa.

Kuna matukio kadhaa yametokea miaka na miezi michache iliyopita yanayotoa taswira mbaya juu ya usalama wa raia na baadhi ya viongozi wanaokosoa utawala. Siku za karibuni Viongozi wa CHADEMA wamekua wakiwindwa sana na tayari chama hiki kikuu cha upinzani kilishatoa tuhuma kwa Usalama wa Taifa na baadhi ya viongozi wa juu serikali kuhusika katika mipango haramu ya kukihujumu chama hicho na hata kufikia hatua ya kuwabambikia kesi viongozi wake.
WanaJF,

Mimi Dr Slaa ambaye kwa siku 4 nimekuwa na ziara ya mkoa wa Iringa,Mbeya na Njombe nilikuwa narudi Dar jana baada ya kulala Iringa mjini kutokea Njombe.

Tukio linaloelezwa ni la kweli na nimelishuhudia mwenyewe. Nimeingia kwa jina langu na ID yangu ili kuondoa dhana ya Spinning.
Namshukuru sana aliyetoa Taarifa, na kuliwasilisha kama ilivyotokea bila kuongeza wala kupunguza kitu.

Tuliondoka Iringa majira ya saa 3.30 hivi. Kwa mwanzo hatukutambua kitu, ila mara ya kwanza tuliona gari hilo likitupita kwa kasi km kama 20 hivi baada ya kupita junction ya Ipogolo. Tuliona kawaida. katika hatua hiyo tulijua ni wasafiri wenzetu. baadaye tukawa tunawapita, wanatupita kasi na kupotea, lakini baada ya muda tunawakuta na kutupisha. hatukustuka sana, japo kuanzia Ilula tukaanza kuulizana.

Mlima Kitonga wakatipita kwa kasi sana japo mbele yetu kulikuwa na semitrela kama 4 zikiteremka pole pole sana na nabasi 2 kwenye kona moja basi lililpkuwa mbele yetu kikakwaruzwa na lori lililokuwa lunapanda. Tukachukua tahadhari sana.

Tulipovuka daraja la Mtp Ruaha tukalikuta L/cruiser hiyo imesimama pembeni lakini abiria wake wote walikuwa ndani. tulipolikaribia likaondoka kwa kasi. kidogo tulistuka. sisi tukaamua makusudi kusimama na kununua vitunguu. Tulipofika Mikumi mjini tukalikuta tena likienda taratibu. kuanzia hapo tukawa makini sana hasa kwenye kona na au vichaka vikubwa. kimsingi tukajiweka kwenye hali ya tahadhari kubwa.

Moro tuliingia Petrol Station nao pia wakaingia nyuma yetu lakini hawakujaza mafuta. Punda wakaondoka direction ya Dodoma. Ikumbukwe sisi tumetoka Njombe tumetangaza tunaenda Kongwa ,Jimbo la Ndugai. mimi nikakapata dharura nikapaswa kurudi Dar. hivyo baada ya mufuta tukafuata direction ya Dar. Punde likatokeza tena na kutupita. Tukalipita kidogo kabla ya Chalinze. Baada ya Chalinze hatukuliona tena mpaka tulipolikuta Junction ya Tamko limepaka. mata nyibgine huwa natumia hiyo junction badala ya kuingia Jijini. Na kweli driver akapiga indicator nyingie hapo. nikaagiza tuelekee jijini Dar. ndipo ghafla nao wakaingia barabarani nyuma ya gari langu kabisa. ndipp nikaagiza afisa wangu apande juu ya gari letu -roof top na kulipga picha. kuona hivyo ghafla likatoka pembeni na kupaki. sisi tukaendelea, ndipo mbele kidogo tukakuta askari walioko zamu yao ya kawaida wakatusimamisha na tukawapa taarifa ya halu hiyo.

Sasa katika mazingira hayo kuna mtu bado anafikiria ni spinning anaweza kuamini hivyo hatuwezi kumlazimisha.

Natumaini nimefafanua ya kupotosha. Nawashukuru wote waliotupa pole. Tunaanza na Mungu tunabaki na Mungu. Hatumwogopi Binadamu na mapambano ya ukombozo hayatakoma kwa vitisho vya aiina hiyo, ndiyo kwanza vinatupa ari na mori.
PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana

~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
 
Spinning at the highest order.

Hivi wewe kwa akili zako kama kweli kuna watu wanataka kuwadhuru viongozi wa CHADEMA watahangaika kwa jinsi unavyoelezea hapa.

Siyo kila jambo ni siasa siasa siasa. Siku hizi mwanasiasa hata akikumbana na vibaka anadai wanasiasa wanamfanyizia.

Jifunzeni kutokuwa wepesi wa kupata majibu kabla ya uchunguzi makini.

Cha kushangaza hao hao watu wa usalama mnaowatuhumu kwa matukio mbali mbali yanayowahusu, ndiyo hao hao mnaotueleza mlienda kulipoti tukio.

Yaani umeamua kuja na ID mahususi kwa ajiri ya SPINNING za kiulinzi.

Kweli tutasikia mengi.
 
CHADEMA mmezidi sasa hadi inatia kinyaa! Mnashindwa hata kutunga uongo ukafanana japo kidogo na ukweli?

Njoo na ID yako verified halafu uone kama wiki ijayo hukupelekwa mahakamani kwa kumchafua anayetumia hilo gari ulilotaja namba zake (Kama sio feki).
 
Hizi mbinu za kifedhuli zinazotumika kukabiliana na Chadema na viongozi wake ni za kulaaniwa kwa nguvu zote.

Niwapongeze maofisa hao waliocharuka na kunakili namba za gari pamoja na kupiga picha gari hilo

Tumeshabihiana sasa na utawala wa makaburu.Ni jambo la hatari sana
 
You seem to be too desperate for power!!

Uongozi mwanana wa kuongoza jamii unakuja automatically kwa mapenzi ya waongozwa. Mwl. Nyerere alisema kiongozi mzuri ni yule asiyetaka kuongoza. Ninyi kwa sasa inavyoonekana mnataka kuongoza kwa hali na mali.

Hizi spinning mnazozianzisha zitakuja kuwarudieni ninyi wenyewe. Historia ya chaguzi nyingi za nchi za Afrika imebainisha hili. You're setting the spinning bar very high kiasi kwamba hata mkiingia madarakani hamuwezi kuwapa wananchi kile mnacho spin kucha kutwa kama kinawezekana. otherwise, tunaanza kuona kama mko na mission za kutaka kujinufaisha kibinafsi
 
Chezea chama chetu cha ccm nin? Ccm itaongoza milele, kwani watanzania ni waoga! Umeona kule Arusha kuna mwananchi analeta fyokofyoko? Ccm itatawala daima tanzania! Mpe pole dr slaa kwa safari, teh,teh..!
 
Spinning at the highest order.

Hivi wewe kwa akili zako kama kweli kuna watu wanataka kuwadhuru viongozi wa CHADEMA watahangaika kwa jinsi unavyoelezea hapa.

Siyo kila jambo ni siasa siasa siasa. Siku hizi mwanasiasa hata akikumbana na vibaka anadai wanasiasa wanamfanyizia.

Jifunzeni kutokuwa wepesi wa kupata majibu kabla ya uchunguzi makini.

Cha kushangaza hao hao watu wa usalama mnaowatuhumu kwa matukio mbali mbali yanayowahusu, ndiyo hao hao mnaotueleza mlienda kulipoti tukio.

Yaani umeamua kuja na ID mahususi kwa ajiri ya SPINNING za kiulinzi.

Kweli tutasikia mengi.
Du! Kumbe nayo hii imekuwa stori, hamna chochote ni mimi nilikuwa natoka zangu Iringa nikaamua ili niende mwendo mzuri basi nifukuzane na dreva wa Dr Sllaa kumbe nayo imekuwqa issue, kweli TISS mtawasingizia mengi mpaka kufika 2015
 
You seem to be too desperate for power!!

Uongozi mwanana wa kuongoza jamii unakuja automatically kwa mapenzi ya waongozwa. Mwl. Nyerere alisema kiongozi mzuri ni yule asiyetaka kuongoza. Ninyi kwa sasa inavyoonekana mnataka kuongoza kwa hali na mali.

Hizi spinning mnazozianzisha zitakuja kuwarudieni ninyi wenyewe. Historia ya chaguzi nyingi za nchi za Afrika imebainisha hili. You're setting the spinning bar very high kiasi kwamba hata mkiingia madarakani hamuwezi kuwapa wananchi kile mnacho spin kucha kutwa kama kinawezekana.

Taarifa hizi zinakufurahisha sana wewe na wasiopenda mabadiliko.Mbinu hizi za vitisho na majaribio mabaya kwa viongozi wa upinzani hazitafanikiwa kamwe.

Sasa jeshi la polisi litoe taarifa kuhusu watu hawa ni akina nani na malengo yao ni nini hasa.Kauli zebu huku hazisaidii bali jeshi la polisi sasa linalojigamba kutenda kwa weledi litoke hadharani
 
namba zenyewe zinaweza kuwa za bajaji
 
mtafakali juu ya haya yote yatokeayo sasa ni kwa nini na kwa nini sasa na sio badae na kwanini si wakati mwingine wowote isipokua wakati huu yamekuwa mengi na kila kukicha huibuka mengine,,,
 
Lol yaani huwezi kuamini kama sasa watu wanalazimisha nchi kuingia kwenye machafuko hivi inakuaje kuanzia utawala huu mambo ya ajabu ajabu yanatokea kuna siri gani?Au ndio wanaogopa Chadema wakikamata dola wataishia The Hague na wengine Ukonga?Sasa wanaona ni kheri kuwapotezea viongozi wa Chadema muda ili wahangaike nao lakini washachelewa wanakumbuka shuka wakati tayari kumeshakucha Lol!!Aibu yao
 
Back
Top Bottom