Dkt.Slaa: Mabadiliko ya Mawaziri, Serikali haijui inataka nini, kubadili viongozi kama Gauni haisaidii kitu

Dkt.Slaa: Mabadiliko ya Mawaziri, Serikali haijui inataka nini, kubadili viongozi kama Gauni haisaidii kitu

.......kubadilisha watu kama anabadilisha gauni lake.......
Mwisho wa kunukuu
 
Haya si Maneno yangu, ni Maneno ya Dkt Slaa


MWANASIASA mkongwe na Katibu Mkuu wa zamani wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa amesema mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yanayofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan kila mara yamedhihirisha kuwa Serikali haijui inataka nini kwa sababu hata viongozi wanaorejeshwa kwenye baraza hilo na katika nafasi nyingine, hawana manufaa yoyote kwa Taifa zaidi ya kujipanga na uchaguzi ujao.

Akizungumza na MwanaHALISI Online leo Jumatatu ametoa mfano namna aliyekuwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye alivyoikosesha Tanzania uwekezaji mkubwa wa kiteknolojia kutoka kwa Elon Musk ambaye ni tajiri namba mbili duniani.

“Watanzania tutengeneze mshikamano wetu ambao utalenga kujipanga kwenye uchaguzi unaokuja na kushinikiza upatikanaji wa katiba mpya ili haya yanayotokea leo ya rais kubadilisha watu kama anabadilisha gauni lake, sioni kama yanatusaidia kwani gauni analivaa yeye mwenyewe,” amesema Dk. Slaa.

Chanzo: Mwanahalisi Digital

Pia soma > Uteuzi na Utenguzi: Nape, January na Byabato out! Jerry Silaa ahamishiwa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
Mzee Slaa na wengine humu wanaokosoa wasome hadi kupatikana Putin, Boris Yeltsin aliteua na kutengua mawaziri wakuu wangapi na kwa muda gani hadi akampata Putin. Tuiache mamlaka ya Rais ifanye kazi yake. Inajua kuliko sisi.🙏🙏🙏
 
Kwenye organization yoyote ukiona kila siku manager au CEO unafanya reshuffle kila kukicha ujue na bado mambo hayaendi ujue shida ni wewe Manager au CEO na only solution ni wewe kuresign.

Haiwezekani tukawa tunachukulia ni hali ya kawaida kuteua na kutengua halafu bado kila mahala ni shida tu, inawezekana shida ikawa Kwa mteuaji/mtenguaji au mfumo mzima umeoza na hauna watu, njia pekee ni kuubadirisha mfumo ili kila Mtanzania aweze kuingia kwenye system kuliko hii ya sasa kutegemea uteuzi ndani inner circle.
 
kwani yeye aliefukuzwa upadre na alikua anabadilisha vyama vya siasa na wanawake alikua anawabadili kama gauni au soksi?🐒

kwanza yeye yupo chama gani saivi kama sio tamaa tu zimemjaa hajui hata ajiunge chama gani kote anataka awepo 🐒
Mmmmmmh
 
Haya si Maneno yangu, ni Maneno ya Dkt Slaa


MWANASIASA mkongwe na Katibu Mkuu wa zamani wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa amesema mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yanayofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan kila mara yamedhihirisha kuwa Serikali haijui inataka nini kwa sababu hata viongozi wanaorejeshwa kwenye baraza hilo na katika nafasi nyingine, hawana manufaa yoyote kwa Taifa zaidi ya kujipanga na uchaguzi ujao.

Akizungumza na MwanaHALISI Online leo Jumatatu ametoa mfano namna aliyekuwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye alivyoikosesha Tanzania uwekezaji mkubwa wa kiteknolojia kutoka kwa Elon Musk ambaye ni tajiri namba mbili duniani.

“Watanzania tutengeneze mshikamano wetu ambao utalenga kujipanga kwenye uchaguzi unaokuja na kushinikiza upatikanaji wa katiba mpya ili haya yanayotokea leo ya rais kubadilisha watu kama anabadilisha gauni lake, sioni kama yanatusaidia kwani gauni analivaa yeye mwenyewe,” amesema Dk. Slaa.

Chanzo: Mwanahalisi Digital

Pia soma > Uteuzi na Utenguzi: Nape, January na Byabato out! Jerry Silaa ahamishiwa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
Kama nyumba yako inavuja hata ukipanguwa vipi furniture, bado iatavuja tu.
Ukitaka isivuje badilisha paa.

Paa ni serikali au nibaraza lote la mawaziri au chama au mfumo mzima.
 
Waafrika hasa watanzania hawawezi kujiongoza wenyewe.
Inabidi mkoloni mjerumani arudi kuongoza hii nchi kwa viboko na mijeledi.
 
Back
Top Bottom