The Palm Beach
JF-Expert Member
- Dec 30, 2015
- 1,967
- 4,267
Fuatilia kwa umakini minyukano ya siasa za uchaguzi wa Mwenyekiti CHADEMA Taifa utakaofanyika tarehe 21/01/2025 inayoendelea ndani ya chama hiki kisha husianisha na matukio haya👇..
TUKIO #1: Tundu Lissu atangaza nia ya kugombea u - Rais wa JMT 2025 iwapo chama chake kitampa ridhaa. Asema, tayari ameshaiweka nia yake hiyo kwa barua (maandishi) na kuiwasilisha kwa katibu mkuu.
TUKIO#2: Sambamba na kuweka wazi nia yake kugombea u - Rais wa JMT, TL pia atangaza kusudio lake la kuwania Umakamu mwenyekiti wa CHADEMA kwa awamu ya pili 2024 - 2025..
TUKIO #3: Ghafla, Tundu Lissu aondoa kusudio lake la kuwania Umakamu mwenyekiti wa CHADEMA na badala yake kutangaza kuwania nafasi ya juu zaidi (Uenyekiti) wa CHADEMA...
TUKIO #4: Tundu Lissu apokea vitisho vya kuuwawa tena kama ilivyokuwa mwaka 2017 alipopigwa risasi 37. Anasema mtu muhimu na mzito sana ndani ya serikali kampa siri ya mipango inayosukwa na kikosi kazi cha siri ndani ya serikali. Aambiwa achukue tahadhari zote kwa usalama wake. Aanza kuvaa "bullet proof" kila anapokuwa ktk shughuli zake za nje.
TUKIO #5: Katibu mkuu John John Mnyika, atangaza rasmi tarehe ya uchaguzi, kuchukua na urejeshaji fomu za kuomba kuteuliwa kugombea nafasi mbali ndani ya chama ikiwemo Uenyekiti Taifa. Tundu Lissu siku ya kwanza tu aenda kuchukua fomu na kesho yake akalipia 1,500,000 (pesa ambayo anasema ilitolewa na mwanaharakati Sativa kama njia ya kumsapoti)
TUKIO #6: Wanaosemekana wafuasi na wapenzi wa M/Kiti kadhaa wafika kwake kwa kile walichodai kumshawishi achukue fomu Ili naye agombee (atetee nafasi). Asita kukubali siku hiyo. Awaambia wasubiri, atafakari kwanza aone mambo yanavyokwenda na akiona "chama chake kinaparanganyika, ataingia mzigoni" na masaa 48 atakuwa analo jibu. Masaa 48 yakaisha, akatoa jibu la NDIYO na kutangaza rasmi kuwa atachukua fomu na kutetea kiti chake...!
TUKIO #7: Freeman Mbowe baada ya siku kadhaa kuwa kimya, aonekana kwenye kituo kimoja cha TV ya matandaoni (Online TV) akifanya mahojiano na mwandishi wa habari maarufu Salimu Kikeke. Mahojiano yake hayo yanazua maswali mengi. Anasema, haelewi ni kwanini Makamu wake (Tundu Lissu) ameamua kugombea uenyekiti kwa kuwa walikaa, wakazungumza na kukubaliana. Hakuweka wazi walizungumza na kukubaliana nini. Anamshauri mwandishi aende akamuulize swali hili Tundu Lissu, maana yeye hana jibu. Japo hakusema wazi, lakini inawezekana makubaliano yao ni "NANI AWE MWENYEKITI WA CHADEMA TAIFA" tena 2024 - 2029...
TUKIO #8: Hili ndilo msingi mkuu wa mjadala huu na hayo mengine yote yatakuwa ni rejea.
Katika audio video hiyo👆👆, ni Dr Wilbroad Slaa (Balozi) akiwa kwenye mjadala wa Moja ya Club 🏠 House mtandaoni akichambua hoja za Freeman Mbowe ktk interview ile ya kwenye Online TV....
Dr Slaa anasema, kiini cha vita hii ya siasa za madaraka ya uongozi kati ya FREEMAN MBOWE na TUNDU LISSU, ni kwa sababu mapatano ya Samia na Mbowe ni kuwa, yeye Freeman Mbowe ndiyo agombee u - Rais ktk uchaguzi mkuu mwaka huu 2025 kwa tiketi ya CHADEMA na sio Tundu Lissu. Mama Abdul atatoa mapesa mengi kwa CHADEMA na watapata/achiwa/shindishwa kwenye majimbo kadhaa ya ubunge...!
✓ Inasemekana Moja ya makubaliano ya kilichoitwa "maridhiano" ni Freeman Mbowe kuhakikisha Tundu Lissu "anatoka katika picha" kabisa ya CHADEMA kwa kutokuwa na nafasi yoyote ya uongozi. Sasa anza kuunganisha dots:
✓ Ndiyo maana TL aliwekewa Hezekiah Wenje apambane naye kwenye nafasi ya Umakamu mwenyekiti. System ingehakikisha Wenje anashinda iwe mvua au jua huku Freeman Mbowe naye akiwa mgombea pekee au akiwekewa mshindani dhaifu kwenye Uenyekiti..
✓ Tundu Lissu akatonywa mkakati huu, akaambiwa, mfuate huko huko juu naye akajibu "sasa nampandia huko huko juu", kwenye Uenyekiti....
✓ Kwa mujibu wa Dr Wilbroad Slaa, ni kuwa mapatano ya Samia Suluhu Hassan, Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa JMT na Freeman Mbowe (Mwenyekiti wa CHADEMA) kwenye "maridhiano" yao ni:
Moja; Ni kuhakikisha Tundu Lissu hana nafasi yoyote ya uongozi ndani ya chama na ikibidi afukuzwe uanachama kabisa. Kwa njia hii hatakuwa na jukwaa la kusemea.
Pili, kuhakikisha yeye Freeman Mbowe ndiye anakuwa mgombea u - Rais wa CHADEMA na siyo Tundu Lissu. Lengo sio Mbowe ashinde bali kutoa unafuu wa Samia Suluhu na CCM kushinda kilaini. Mtu kama Tundu Lissu kwa ushawishi alionao kwao CCM na Samia wao ni hatari, atakuwa anawalaza na viatu...
##Sasa unaweza kuelewa ni kwanini TL mara kwa mara anayaponda maridhiano hayo na kusema wazi "Kuna mengi nyuma ya pazia ambayo Mwenyekiti huwa hawaambii wenzake kwenye hii kitu inayoitwa maridhiano..."
✓Pamoja na mikakati na figusufigisu hizi zinazoendelea ndani ya CHADEMA kuhakikisha TL "is out of the picture" kwa vihoja vya mara oh anatoa siri za chama, mara ooh hana busara, au amevunja na kukiuka katiba au mara hivi au vile; ieleweke tu kuwa, yote haya ni harakati za kujaribu kumjengea hoja ya "kumkosesha sifa ya haki ya kugombea uongozi na uanachama" Ili lengo na kusudi la kumtoa ktk chama (to take him out of the picture) litimie, ili CCM na Samia wao wapumue..!
✓ Lakini pia moja ya "option" iliyosukwa kama njia hizi za ndani ya chama zinashindikana, ni kumuua kabisa au kumdhuru au kumjeruhi vibaya kabla ya uchaguzi Ili atumie muda mwingi kujiuguza hospitalini, akitoka huko akute mwana si wake.
✓ Huu mkakati wa kumdhuru TL unasukwa na "wasiojulikana" ndani ya serikali/CCM na wengine wako ndani ya CHADEMA na Freeman Mbowe anajua fika.
Sasa unaweza kuelewa ni kwanini Team Campaign ya Freeman Mbowe ni wakali na wanahakikisha yanakuwa kama ilivyopangwa iwe jua au mvua kwa sababu ya ahadi walizopewa ikiwemo viti kadhaa vya ubunge, fedha za kampeni ya u - Rais nk
Aidha unaweza sasa pia kuelewa ni kwanini Chawa wa Freeman Mbowe wanatumia kauli au kigezo cha fedha kama turufu yao. Kwamba, hata akiwa Mwenyekiti huyu TL atatoa wapi pesa za kuendesha chama, kampeni ya u Rais nk iwapo TZS 30,000,000 tu za kuchangia gharama za mkutano mkuu wa uchaguzi ameshindwa kutoa. Msingi wa hoja hii, ni kuwa, wao wanategemea pesa za Abdul na mama yake alizohongwa na waarabu DP World na Oman kwa kuwapa rasrimali asili zetu bandari, misitu na mbuga za wanyama..!!
Sharti ni Moja tu: Mdhibitini huyu bwana.....Tundu Lissu
TUKIO #1: Tundu Lissu atangaza nia ya kugombea u - Rais wa JMT 2025 iwapo chama chake kitampa ridhaa. Asema, tayari ameshaiweka nia yake hiyo kwa barua (maandishi) na kuiwasilisha kwa katibu mkuu.
TUKIO#2: Sambamba na kuweka wazi nia yake kugombea u - Rais wa JMT, TL pia atangaza kusudio lake la kuwania Umakamu mwenyekiti wa CHADEMA kwa awamu ya pili 2024 - 2025..
TUKIO #3: Ghafla, Tundu Lissu aondoa kusudio lake la kuwania Umakamu mwenyekiti wa CHADEMA na badala yake kutangaza kuwania nafasi ya juu zaidi (Uenyekiti) wa CHADEMA...
TUKIO #4: Tundu Lissu apokea vitisho vya kuuwawa tena kama ilivyokuwa mwaka 2017 alipopigwa risasi 37. Anasema mtu muhimu na mzito sana ndani ya serikali kampa siri ya mipango inayosukwa na kikosi kazi cha siri ndani ya serikali. Aambiwa achukue tahadhari zote kwa usalama wake. Aanza kuvaa "bullet proof" kila anapokuwa ktk shughuli zake za nje.
TUKIO #5: Katibu mkuu John John Mnyika, atangaza rasmi tarehe ya uchaguzi, kuchukua na urejeshaji fomu za kuomba kuteuliwa kugombea nafasi mbali ndani ya chama ikiwemo Uenyekiti Taifa. Tundu Lissu siku ya kwanza tu aenda kuchukua fomu na kesho yake akalipia 1,500,000 (pesa ambayo anasema ilitolewa na mwanaharakati Sativa kama njia ya kumsapoti)
TUKIO #6: Wanaosemekana wafuasi na wapenzi wa M/Kiti kadhaa wafika kwake kwa kile walichodai kumshawishi achukue fomu Ili naye agombee (atetee nafasi). Asita kukubali siku hiyo. Awaambia wasubiri, atafakari kwanza aone mambo yanavyokwenda na akiona "chama chake kinaparanganyika, ataingia mzigoni" na masaa 48 atakuwa analo jibu. Masaa 48 yakaisha, akatoa jibu la NDIYO na kutangaza rasmi kuwa atachukua fomu na kutetea kiti chake...!
TUKIO #7: Freeman Mbowe baada ya siku kadhaa kuwa kimya, aonekana kwenye kituo kimoja cha TV ya matandaoni (Online TV) akifanya mahojiano na mwandishi wa habari maarufu Salimu Kikeke. Mahojiano yake hayo yanazua maswali mengi. Anasema, haelewi ni kwanini Makamu wake (Tundu Lissu) ameamua kugombea uenyekiti kwa kuwa walikaa, wakazungumza na kukubaliana. Hakuweka wazi walizungumza na kukubaliana nini. Anamshauri mwandishi aende akamuulize swali hili Tundu Lissu, maana yeye hana jibu. Japo hakusema wazi, lakini inawezekana makubaliano yao ni "NANI AWE MWENYEKITI WA CHADEMA TAIFA" tena 2024 - 2029...
TUKIO #8: Hili ndilo msingi mkuu wa mjadala huu na hayo mengine yote yatakuwa ni rejea.
Katika audio video hiyo👆👆, ni Dr Wilbroad Slaa (Balozi) akiwa kwenye mjadala wa Moja ya Club 🏠 House mtandaoni akichambua hoja za Freeman Mbowe ktk interview ile ya kwenye Online TV....
Dr Slaa anasema, kiini cha vita hii ya siasa za madaraka ya uongozi kati ya FREEMAN MBOWE na TUNDU LISSU, ni kwa sababu mapatano ya Samia na Mbowe ni kuwa, yeye Freeman Mbowe ndiyo agombee u - Rais ktk uchaguzi mkuu mwaka huu 2025 kwa tiketi ya CHADEMA na sio Tundu Lissu. Mama Abdul atatoa mapesa mengi kwa CHADEMA na watapata/achiwa/shindishwa kwenye majimbo kadhaa ya ubunge...!
✓ Inasemekana Moja ya makubaliano ya kilichoitwa "maridhiano" ni Freeman Mbowe kuhakikisha Tundu Lissu "anatoka katika picha" kabisa ya CHADEMA kwa kutokuwa na nafasi yoyote ya uongozi. Sasa anza kuunganisha dots:
✓ Ndiyo maana TL aliwekewa Hezekiah Wenje apambane naye kwenye nafasi ya Umakamu mwenyekiti. System ingehakikisha Wenje anashinda iwe mvua au jua huku Freeman Mbowe naye akiwa mgombea pekee au akiwekewa mshindani dhaifu kwenye Uenyekiti..
✓ Tundu Lissu akatonywa mkakati huu, akaambiwa, mfuate huko huko juu naye akajibu "sasa nampandia huko huko juu", kwenye Uenyekiti....
✓ Kwa mujibu wa Dr Wilbroad Slaa, ni kuwa mapatano ya Samia Suluhu Hassan, Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa JMT na Freeman Mbowe (Mwenyekiti wa CHADEMA) kwenye "maridhiano" yao ni:
Moja; Ni kuhakikisha Tundu Lissu hana nafasi yoyote ya uongozi ndani ya chama na ikibidi afukuzwe uanachama kabisa. Kwa njia hii hatakuwa na jukwaa la kusemea.
Pili, kuhakikisha yeye Freeman Mbowe ndiye anakuwa mgombea u - Rais wa CHADEMA na siyo Tundu Lissu. Lengo sio Mbowe ashinde bali kutoa unafuu wa Samia Suluhu na CCM kushinda kilaini. Mtu kama Tundu Lissu kwa ushawishi alionao kwao CCM na Samia wao ni hatari, atakuwa anawalaza na viatu...
##Sasa unaweza kuelewa ni kwanini TL mara kwa mara anayaponda maridhiano hayo na kusema wazi "Kuna mengi nyuma ya pazia ambayo Mwenyekiti huwa hawaambii wenzake kwenye hii kitu inayoitwa maridhiano..."
✓Pamoja na mikakati na figusufigisu hizi zinazoendelea ndani ya CHADEMA kuhakikisha TL "is out of the picture" kwa vihoja vya mara oh anatoa siri za chama, mara ooh hana busara, au amevunja na kukiuka katiba au mara hivi au vile; ieleweke tu kuwa, yote haya ni harakati za kujaribu kumjengea hoja ya "kumkosesha sifa ya haki ya kugombea uongozi na uanachama" Ili lengo na kusudi la kumtoa ktk chama (to take him out of the picture) litimie, ili CCM na Samia wao wapumue..!
✓ Lakini pia moja ya "option" iliyosukwa kama njia hizi za ndani ya chama zinashindikana, ni kumuua kabisa au kumdhuru au kumjeruhi vibaya kabla ya uchaguzi Ili atumie muda mwingi kujiuguza hospitalini, akitoka huko akute mwana si wake.
✓ Huu mkakati wa kumdhuru TL unasukwa na "wasiojulikana" ndani ya serikali/CCM na wengine wako ndani ya CHADEMA na Freeman Mbowe anajua fika.
Sasa unaweza kuelewa ni kwanini Team Campaign ya Freeman Mbowe ni wakali na wanahakikisha yanakuwa kama ilivyopangwa iwe jua au mvua kwa sababu ya ahadi walizopewa ikiwemo viti kadhaa vya ubunge, fedha za kampeni ya u - Rais nk
Aidha unaweza sasa pia kuelewa ni kwanini Chawa wa Freeman Mbowe wanatumia kauli au kigezo cha fedha kama turufu yao. Kwamba, hata akiwa Mwenyekiti huyu TL atatoa wapi pesa za kuendesha chama, kampeni ya u Rais nk iwapo TZS 30,000,000 tu za kuchangia gharama za mkutano mkuu wa uchaguzi ameshindwa kutoa. Msingi wa hoja hii, ni kuwa, wao wanategemea pesa za Abdul na mama yake alizohongwa na waarabu DP World na Oman kwa kuwapa rasrimali asili zetu bandari, misitu na mbuga za wanyama..!!
Sharti ni Moja tu: Mdhibitini huyu bwana.....Tundu Lissu