Dkt. Slaa: Niliudhika kwa maneno ‘Mbowe si gaidi’, nyie ni nani mpaka kusema siyo gaidi? Ataka wananchi wanyamaze Mahakama ifanye kazi yake

Shikamoo jamiiforums!!
 
Hao ndo zao wanamchukia mtu kwa sababu ya dini yake yani hii nchi tuna wapumbavu wengi sana.

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 
Mbona hapa Tanzania kuhonga upate tender ni jambo la kawaida Tokea Enzi za Nyerere Mwinyi Mkapa Kikwete Magufuli nini ambacho ni cha ajabu?
So umekiri palikuwa na harufu ya RUSHWA, hapo hapo unapinga kuwa mkataba Ule si BATILI na FAKE?
 
So umekiri palikuwa na harufu ya RUSHWA, hapo hapo unapinga kuwa mkataba Ule si BATILI na FAKE?
Labda wewe ni mgeni hapa Tanzania sisi tulioanza na Nyerere tunajua Tanzania bila hongo hakuna kitu kinachoendelea

Na ukijifanya Mzalendo saana utakufa masikini
 
Unasemaje sasa.
Muwe mna kuwa na akiba ya maneno.
Acheni kiburi cha uhai na uzima.
 
To prove the point
Tulimwambia Jpm aache kiburi cha uzima, tulimwambia pia na Slaa. Yako wapi sasa.
Sisi sio manabii lakini tunatumia ufahamu wa kawaida tu.

Injustice to some people is injustice to you too. Ni swala la muda tu.
 
Aisee acha Mungu aitwe Mungu tu wakuu.

Najua kuna watu wana macho, lkn hawaoni. Wana vichwa lkn hawana akili.

View attachment 2719183
Aisee mkuu, kumbe ule muda umeshika jembe na chepeo/spade ukatupita pale tumekaa kwenye kivuli cha mti wa Mvule tukiwa tunacheza draft, kumbe ulikua unaelekea Makaburini kufukua Kaburi?.
 

CROCODILETOOTH: Niliudhika kwa maneno ‘SLAA si gaidi’, nyie ni nani mpaka kusema siyo gaidi? Ataka wananchi wanyamaze Mahakama ifanye kazi yake!😁😁😁​

N.b/KARMA!
 
Dr. Slaa sio mhaini, kama ambavyo ilithibitika Mbowe hakuwa gaidi.

Ni hivyo tu.

Kama mnamfahamu mwanasiasa malaika mtajeni hapa tumjue......
 
Hahahahaha internet huwa haisahau!
 
Kupinga bandari zetu kugawiwa Bure Kwa RUSHWA kamwe haiwezi kuwa uhaini!!!!
Nakuonea huruma sana kijana kama wewe kugeuzwa daraja na wanasiasa uchwara wakishirikiana na wakili njaa.

Bahati nzuri mimi sio mtu wa kushikiwa akili wala kugeuzwa daraja. Mwanasiasa uchwara au wale walioshikiwa akili wakiniambia kuwa bandari imeuzwa kitu cha kwanza nitahitaji ushahidi wa kuona na macho ili niamini kile wanachosema.

Hizi sio zile zama za Lowasa, kukusanya watu kule mwembeyanga na kudanganya watu kwamba Lowasa ni fisadi eti na ushahidi wanao, afu mwisho mwaka 2015 kwenye uchaguzi wanasema eti Lowasa sio fisadi.
Hivi inawezekana vipi leo useme fulan mwizi afu kesho useme sio mwizi, kama wewe sio muongo ni kitu gani.

Mwl Nyerere aliwahi kuwaonya watanzania juu ya hawa wanasiasa uchwara waongo ambao wanatumia ujinga wa watanzania kama wewe kufanya siasa za uongo kwa faida zao na familia zao.

Unashindwa kutumia akili kuwaza hata jambo dogo tu kwamba kama wamekamatwa kwa sababu ya kupinga mkataba mbona kina kardinal Pengo, mzee Warioba, prof Tibaijuka, Mbowe, Lisu na wengine wengi wapo mtaani wanadunda.

Hebu weka mkataba hapa ili tuone kipengele kilichoandikwa kuwa bandari imeuzwa ili iwe rahisi na sisi kuunga na wapinga bandari, sio ulete maneno matupu yasiokuwa na maana hapa JF
 
Pole
Tulia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…