Dkt. Slaa: Tukio la Tundu Lissu kupigwa risasi na watu ‘wasiojulikana’ ni jambo la kawaida

Dkt. Slaa: Tukio la Tundu Lissu kupigwa risasi na watu ‘wasiojulikana’ ni jambo la kawaida

Balozi Mteule na aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Wilbroad Slaa amesema tukio la Tundu Lissu kupigwa risasi na watu ‘wasiojulikana’ ni jambo la kawaida na ameitaka jamii kuliacha Jeshi la Polisi kukamilisha upelelezi na kutoa majibu.

Dkt. Slaa ametoa kauli hiyo wakati akihojiwa na kituo cha runinga cha Clouds juu ya hali ya kisiasa ya Tanzania na mustakabali wa maisha yake baada ya kuondoka CHADEMA, amesema hafurahishwi na baadhi ya watu kuwataja hadharani watuhumiwa wa tukio hilo kwasababu linaharibu uchunguzi wa polisi.

“Mimi kinachoniudhi ni hii watu kusema hadharani kwamba kuna hiki na hiki tunasuspect (tunahisi) waliofanya ni fulani. Sheria inasema ukihisi nenda polisi katoe taarifa sio unaenda kwenye vyombo vya habari”, amesema Dkt. Slaa.

Amesema hawezi kuzungumzia kwa undani suala la Lissu kupigwa risasi, ikizingatiwa kuwa watu wengi wamepigwa risasi nchini na kazi ya kuwabaini wahalifu waliomshambulia ni ya polisi sio viongozi wa siasa au wananchi.

“Lakini kama binadamu hakuna anayependa binadamu yeyote aumizwe lakini matukio haya ya kuumizwa yametokea nchi hii kwa watu wengi sana. Na mimi sio chombo cha dola kujua kwamba unanyoosha kidole kwa kitu ambacho hatukiamini; mimi ni msomi”, amesema Dkt. Slaa na kuongeza kuwa,

“Ukitoa taarifa za upelelezi unaharibu upelelezi. Mimi niko Canada mauaji yapo kila siku na watu wanapotea, wanapigwa risasi wakiulizwa polisi wanakwambia suala hilo liko kwenye upelelezi tukifikia hatua nzuri tutatoa taarifa”.
Njaa ni kitu kibaya sana. Tumasamehe bure kwa kuwa njaa huondoa akili na maarifa.
 
ab.jpg
Wilbroad Slaa amesema tukio la Tundu Lissu kupigwa risasi na watu ‘wasiojulikana’ ni jambo la kawaida
 
Hivi jamani..Tundu lissu ni nani hapa tanzania? Nchi hii ilipoteza kina sokoine kina nyerere nk. Kwamba yeye hana maadui mtaani? Mbona watu wengi tu wanapigwa risasi na tunalasni basi. Mbona huyu kuna watu wanaona as if he is so importnt than many others
 
Dr Slaa kasema tukio lile ni jambo la kawaida? Kama ni kweli ameongea haya maneno nitamtoa maanani moja kwa moja!

Nadhani anataka kutumika kuendesha propaganda kuwa Lissu hakushambuliwa kwasababu za kisiasa!

Ukisoma btn the lines, kusema ni jambo la kawaida, ni sawa na kudownplay tukio zima! Of which nimeshangazwa sana!

Ubalozi aliopewa, naona mojawapo ya masharti, ni “ubalozi wa propaganda dhidi ya Lissu”

Sasa karata ya serikali ya ccm dhidi ya Lissu ni Slaa, mark my words!
Kuna mitazqmo inaonyesha kuwa tukio lile si la kisiasa wala halihusiani nalo. bali linhusiana na kawi yake ya uwakili kwamba kuna kesi alikuwa anaisimamia kama angekuwepo mtu angefungwa maisha. Ikabidi ifanyike figisu jamaa asiwepo mahakamani.
 
Balozi Mteule na aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Wilbroad Slaa amesema tukio la Tundu Lissu kupigwa risasi na watu ‘wasiojulikana’ ni jambo la kawaida na ameitaka jamii kuliacha Jeshi la Polisi kukamilisha upelelezi na kutoa majibu.

Dkt. Slaa ametoa kauli hiyo wakati akihojiwa na kituo cha runinga cha Clouds juu ya hali ya kisiasa ya Tanzania na mustakabali wa maisha yake baada ya kuondoka CHADEMA, amesema hafurahishwi na baadhi ya watu kuwataja hadharani watuhumiwa wa tukio hilo kwasababu linaharibu uchunguzi wa polisi.

“Mimi kinachoniudhi ni hii watu kusema hadharani kwamba kuna hiki na hiki tunasuspect (tunahisi) waliofanya ni fulani. Sheria inasema ukihisi nenda polisi katoe taarifa sio unaenda kwenye vyombo vya habari”, amesema Dkt. Slaa.

Amesema hawezi kuzungumzia kwa undani suala la Lissu kupigwa risasi, ikizingatiwa kuwa watu wengi wamepigwa risasi nchini na kazi ya kuwabaini wahalifu waliomshambulia ni ya polisi sio viongozi wa siasa au wananchi.

“Lakini kama binadamu hakuna anayependa binadamu yeyote aumizwe lakini matukio haya ya kuumizwa yametokea nchi hii kwa watu wengi sana. Na mimi sio chombo cha dola kujua kwamba unanyoosha kidole kwa kitu ambacho hatukiamini; mimi ni msomi”, amesema Dkt. Slaa na kuongeza kuwa,

“Ukitoa taarifa za upelelezi unaharibu upelelezi. Mimi niko Canada mauaji yapo kila siku na watu wanapotea, wanapigwa risasi wakiulizwa polisi wanakwambia suala hilo liko kwenye upelelezi tukifikia hatua nzuri tutatoa taarifa”.
Kweli Rushwa adui wa haki
 
Kuna mitazqmo inaonyesha kuwa tukio lile si la kisiasa wala halihusiani nalo. bali linhusiana na kawi yake ya uwakili kwamba kuna kesi alikuwa anaisimamia kama angekuwepo mtu angefungwa maisha. Ikabidi ifanyike figisu jamaa asiwepo mahakamani.
Sijakupata vyema mkuu
 
GENTAMYCINE
MKuu kuja usikie maneno ya msomi (PhD) wako unae mkubali anachoongea.

Nayaheshimu maneno yake ya siongezi wala sipunguzi na ninachojua tu ni kwamba kama Tanzania ingekuwa na Watu 100 tu wenye IQ kubwa na za Kuzaliwa kama za Balozi Mteule Dr. Wilbroad Peter Slaa leo hii ama tungekuwa tuko sawa na Malaysia au Singapore au China na hata kukimbizana na London na New York Kimaendeleo tofauti na ilivyo sasa ambapo Tanzania tunapiga tu ' mark time ' katika ' Nyanja ' nyingi.
 
Basi naomba tusaidiane jambo hili kwa wale ambao wanawajua watu wanaohusika katika tukio Zima la Tundu Lissu watujuze ili chombo kinacho husika kikawachukue nawe ukiwa shaidi wa jambno hilo. ila kama hujui chochote wacha.
 
Quite a comedian
Polisi mpaka leo hawajui aliyemuua Mawazo
Polisi hawajui alipo Saanane
Hawajui alipo mwandishi wa mwananchi
Aliyewateka Roma na Ulimboka ni kitendawili hata kama wenyewe wanawafahamu
Nini kina kufanya udhani suala la Lissu litatuliwa?
baba kuna watu ile kuwajibu tu unajidhalilisha,neno ushahidi lisitumike kama bomu kuficha hata yaliyo dhahiri,hii nchi bora ingeongozwa na mbuzi labda wao watatuzidi akili na utu.
 
..Dr.Slaa amejibu kama BALOZI wa Tz.

..kwa wadhifa wake huwezi kutarajia atoe jibu tofauti na alilotoa.

..lakini pia kuna mahali Dr ameteleza.

..kama anadai tukio la TL kushambuliwa kwa risasi ni jambo la kawaida hata huko Canada, basi atueleze ni lini MNADHIMU wa kambi ya UPINZANI ya CANADA alishambuliwa kwa risasi wakati wa vikao vya BUNGE.
ilikuwa sio lazima ajibu mkuu sio kila kitu kinajibika. labda ni punguani au uzee unamuelemea.
 
CCTV cameras kufichwa na upande wenu ni evidence tosha....vipi zile footage za clauz Bashite aka Paul Makonda chupuchupu kuwakill vijana wa Shilawandu mulizikataa ....mungu anaona ...endelea kushabikia umwagaji wa damu za watu wa Yehova bila hatia!!
hawa mpaka yamkute mtu wa familia yake ndio huwa wana shtuka na kujiapiza
 
Slaa ni wa kupuuza tu hana maana kabisa, anatoa shukrani kwa rushwa waliyompa aisambaratishe chadema. Kisiasa aliishajiishia kitambo na ni sawa na garasha.

Swala la Lissu ngoma bado mbichi.

No stone will be left unturned, it's just a matter of time. The potential culprits will one day be brought before justice to account for their crime, regardless of their social status.
sijui kiingereza lakini like
 
Ilikuwa ni suala la muda ili hata watu wanaochelewa kusoma alama za nyakati kuweza hatimaye kuona ni namna gani daktari wetu alivyobadili gia angani kwa sababu tu hakupewa nafasi ya kugombea uongozi.

Hapa ndipo inapokuja ile dhana ya kuwa mwanasiasa na unafiki ni kama pete na kidole. Nani ataaminika tena?
 
Back
Top Bottom