Dkt. Tulia Ackson alilenga nini kupotosha kuwa mhimili mmoja ni mkubwa kuliko miingine? Alijikosha, alijipendekeza?

Dkt. Tulia Ackson alilenga nini kupotosha kuwa mhimili mmoja ni mkubwa kuliko miingine? Alijikosha, alijipendekeza?

Katiba inasema Rais ni Mkuu wa nchi. Sura ya pili, ibara ya 33, kifungu cha kwanza.

Which means Rais yuko juu ya kila kitu na kila mtu, anaweza kumtaka hata mkeo kinguvu, kama chifu wa makabila. Tulia Ackson yuko sahihi.

Mkenge mwingine huu aliotuingiza Nyerere, u-chifu wa kwao.

Siku ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere mwaka jana mwanae Makongoro alisema babu yake alikuwa chifu, na bibi yake (aliyemzaa Mwalimu) alitakwa kuolewa kinguvu na chifu Burito, kijiji cha mwanamke kikasema binti hataki, Chifu Burito akasema anhaa, nakata huduma zote za kijamii kwenda Busegwe, Busegwe wakaambiana kijiji is bigger than kibinti kimoja, wakamwachia, binti Mgaya akaja kuchukuliwa mzega mzega kwenda Butiama, akamzaa Mwalimu kinguvu. Some serious stuff but typical Makongoro, he was laughing like a drunken sailor.

Ndo huu Urais wa ki-chifu aliotuletea Mwalimu. And he had brass set, anadiriki kusema angetaka angeweza kuwa dikteta, katiba inamruhusu. Mbona hukuibadilisha? Miaka 29. Baba wa Taifa uchwara wa dunia ya tatu.

Kuendelea kumpa lawama mtu aliyepita miaka 50 iliyopita ni kukosa akili. Nchi gani ambayo Ina rais mtendaji kama TZ ambaye hana mamlaka sawa na rais wetu?
 
Alishawahi kumkosea MAMA kwa hiyo anatafuta namna ya kuweka mambo sawa
Kuendelea kumpa lawama mtu aliyepita miaka 50 iliyopita ni kukosa akili. Nchi gani ambayo Ina rais mtendaji kama TZ ambaye hana mamlaka sawa na rais wetu?
 
Kuendelea kumpa lawama mtu aliyepita miaka 50 iliyopita ni kukosa akili. Nchi gani ambayo Ina rais mtendaji kama TZ ambaye hana mamlaka sawa na rais wetu?
Kujaribu kujisahaulisha historia ndio upunguani mkubwa zaidi. Taifa hili by and large limekuwa brainwashed and bamboozled na fikra za Nyerere, watu wanafanya vitu kwa sababu Nyerere alisema.
Sasa tunajaribu kuwaamsheni kwa kuwaambia Nyerere hakuwa nabii, bali nae alikuwa na fikra potofu katika baadhi ya maeneo. Tunaonyesha tatizo lilipoanzia ili kusudi tusije kurudia makosa tutakapo andika katiba mpya - tusimwache mtu mmoja na vibaraka wake kumi ishirini waamue mustakabali wa nchi kama Nyerere na kina Kawawa wake.

Nchi zote za kidemokrasia kamili ya mihimili zina Rais ambae hana mamlaka juu ya mihimili mingine.

Hapa kwetu "Rais ni Mkuu wa nchi," kosa! Tulia Ackson - Job Ndugai anaevaa gauni - yuko sahihi.
 
Nadhani si muhimu kujadili kuwa nani ni mkubwa kuliko nani bali la msingi ni kwamba hakuna aliyejuu ya katiba na sheria, ndio maana pamoja na huyo rais kuwa ndio mkuu wa nchi ila alipatikana kwa kupitia hiyo hiyo katiba na ataondoka katika huo ukuu kupitia hiyo hiyo katiba.

Kwahiyo suala la nani mkubwa kuliko mwengine sio point ya msingi sasa kama Tulia alikusudia rais ni mkubwa hadi kuwa juu ya katiba na sheria basi hilo ndio la kujadili.
 
Hata kwa katiba ya sasa serikali inatakiwa ipate kibali cha kukusanya kodi yoyote kutoka bungeni na bunge ndilo linatakiwa liridhie mipango yote ya serikali. Bahati mbaya sana bunge letu limekuwa la kugonga muhuri tu mambo ya serikali badala ya kuwa msimamizi na muwajibishaji wa serikali.

Katiba ya JMT, 1977
136.-(1) Fedha hazitatolewa kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali kwa ajili ya matumizi ila kwa mujibu wa masharti yafuatayo:- (a) fedha hizo ziwe kwa ajili ya matumizi ambayo yameidhinishwa yatokane na fedha zilizomo katika Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali na idhini hiyo iwe imetolewa na Katiba hii au sheria nyingine yoyote; (b) fedha hizo ziwe kwa ajili ya matumizi ambayo yameidhinishwa ama na sheria ya Matumizi ya Serikali iliyotungwa mahsusi na Bunge au sheria iliyotungwa kwa mujibu wa masharti ya ibara ya 140 ya Katiba hii.

138.-(1) Hakuna kodi ya aina yoyote itakayotozwa isipokuwa kwa mujibu wa Sheria iliyotungwa na Bunge au kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa kisheria na uliotiliwa nguvu kisheria na sheria iliyotungwa na Bunge.
Mkuu nakuelewa sana nini katiba inasema na pia uko haja kuangalia practice iko kwenye groud.

Unakumbuka Katibu Mkuu Jairo wakati mmoja alikwenda bungeni na mafungu na kukaa mezani wa waheshimiwa Dodoma ili siku bajeti ikija kusomwa wabunge wawe "washaelewa".

Kwa bunge la watu ambao mchakato wao wa kuingia haukuwa safi, watu wameweka rehani nyumba ili wapate hela ya kampeni, usitegemee kama washawekwa "sawa", wanaweza kupindua meza kwa kuigomea bajeti ya pendekezo la bajeti iwapo serikali imeleta bungeni.
Na katika hili, siwalau CCM pekee, hata wale walio nje ya bunge nao mchakato wa kupata wagombea na wao una bahasha za kutosha, Watanzania ni walewale.

Ila kuna Watanzania wachache sana waadilifu ambao wanaweza kusimamia maslahi ya wananchi, suala ni gumu sana kwao kupenye kwenye michakato hii ya vyama vya siasa.
hata wakiruhusu mgombea binafsi ni wachache sana wenye mtaji wa kugharamia kampeni.
Sheria ya vyama vya siasa imeweka cut point ya "bei" gani mgombea atumie, ila hajasema hiyo hela mgombea atatoa wapi na hamna mechanism ya kumbana mgombea kama "wapambe" wake watatumia nyuma ya pazia na ikawa ngumu ku-trace mtiririko wa hizo fedha.
 
Back
Top Bottom