Dkt. Tulia aitetemesha Mbeya. Atua kijeshi na ndege ya Jeshi

Mkuu hapo kada mwenzangu nakukatalia. Mwezi October nilikuwa huko aisee Dkt Tulia hapendwi mno. Tena wanasema aliwatukana. Yaani status yake Dkt Tulia ni ngumu. Akae na vijana na wazee awasikilize. Kwa ufupi hali yake siyo njema. Mi ka Chawa wa Mama nilipita hiyo sehemu na huo ndiyo ukweli!
 
Unaweza kukuta hujanywa chai mpaka sasa umebakia uchawa

Sent from my Infinix X663 using JamiiForums mobile app
 
Wanasema aliwatukana akina nani? Aliwatukana kwa kusemaje? Aliwatukana akiwa wapi na akiwa anazungumza nini? Lini aliwatukana? Kwa sababu kama ni vijana na wazee hakuna kijiwe ambacho utakwenda cha vijana usikute wakimzungumzia vizuri Dr Tulia.kila kijiwe kimeguswa na kazi za Dr Tulia,kila kijana mwenye kushirikiana na wenzake kwa kuunda kikundi amepata msaada wa fedha taslimu kwa ajili ya kufanyia biashara.Dr Tulia amewapa vijana wengi sana bodaboda na bajaji bure kabisa ambazo kwa mwezi zinawaingizia Malaki ya pesa na hivyo kuondoa utegemezi wa kipato.

Hao unaosema sijuwi wazee hawawezi hata kukusikiliza ukimsema vibaya Dr Tulia maana wao wenyewe wanatambua kazi kubwa aliyoifanya Dr Tulia tangia amekuwa mbunge wao.amewasadia sana na kuwawezesha sana na amekuwa karibu nao sana na kuwasikiliza kila awapo jimboni kwake.

Hata kwa akina mama nako amefanya kazi kubwa sana amewasaidia kupitia mtu mmoja mmoja na kupitia vikundi vyao.amewapa mitaji inayowasaidia kufanya biashara na kujipatia kipato.
 
mbeya ni mji usiokuwa na miundombinu kabisa.
Hakuna mpango wa ujenzi wa mji.
Mitaa haipitiki.

Ni sahihi kabisa.

Kuna Boss mmoja aliwahi kusema kuna changamoto sana ya Town Planning jambo ambalo ni kikwazo kwenye kutimiza majukumu yake
 
Hivi unafahamu kuna idadi kubwa ya wagonjwa wanashikiliwa kwenye Mahospitali mbalimbali ya Serikali hapa nchini kwa kushindwa kulipa gharama za matibabu??hivi unafahamu kuna idadi kubwa ya maiti zimezuiwa kwenye mochwali mbalimbali za Serikali nchini kisa ndugu wa Marehemu hao wameshindwa kulipa gharama za matibabu??huyo Dr.Tulia kupokelewa kwa mbwembwe zozote zile kuna msaada gani kwa ndugu hao waliozuiliwa kwenye Mahospitali mbalimbali kwa kukosa Pesa ya kulipia gharama za matibabu??ifike kipindi uwe unatumia akili za kichwani na si za huko nyuma kwako
 
Kwa hiyo kushikiliwa kwa hao wagonjwa inaowaondolea vipi wanambeya nafasi na haki ya kumpokea mbunge wao wanayempenda na kumuunga mkono kutokana na uchapa kazi wake? Unayafahamu majukumu ya mbunge? Ni wapi katika majukumu ya mbunge ambapo mbunge kazi yake kwenda kuwalipia wagonjwa walioshindwa kulipa pesa za matibabu? Wewe umefanya juhudi gani kuwasaidia? Lini Dr Tulia amekuwa mbunge wa hospitali zinazoshikilia wagonjwa? Kwani Dr Tulia ni mbunge wa majimbo yote hapa Tanzania?

Acha ujinga wako hapa.timiza wajibu wako na siyo kupeleka lawama zako kusikohusika .
 
Dr Tulia ni moto wa kuotea mbali,.hakuna mwenye uwezo wala ubavu wa kuweza kupambana naye katika sanduku la kura.kwa sasa hata mkoa mzima wa Mbeya ukiwa ni jimbo moja la uchaguzi na Dr Tulia akigombea atapita na kushinda kwa kishindo kikubwa sana.
Sema katiba iliyopo ndiyo moto wa kuotea mbali.
 
Sema katiba iliyopo ndiyo moto wa kuotea mbali.
Hata ije katiba ya aina ipi bado Dr Tulia atapita na kushinda kwa kishindo kikuu. Kinachombeba Dr Tulia ni uchapa kazi wake na kuwa karibu ya wananchi pamoja na kuwasikiliza kwa unyenyekevu na kuwapatia majibu kwa wakati.
 
Uaskari wa mtu haupo katika mavazi bali katika mafunzo na utaalamu au ujuzi .kama huna mafunzo na hujahitimu mafunzo ya kijeshi huwezi ukawa mwanajeshi hata kama utavalishwa kombati za jeshi.
Unamjua mwanajeshi kamili Kada au unataja tu ?
 
Vipi leo umekuja na vitisho vipi maana si unakujaga na vitisho vyako utafikiri wewe ni Mungu. Embu andika vitisho vyako vya leo nivione
Nilisha malizana na wewe Mungu si mwanadam aseme uhongo , chukua hii, wala sio vitisho Mungu wangu yupo up to date sana, naludia kauli jirekebishe asema Bwana na sio ombi bali ni amri
 
Nilisha malizana na wewe Mungu si mwanadam aseme uhongo , chukua hii, wala sio vitisho Mungu wangu yupo up to date sana, naludia kauli jirekebishe asema Bwana na sio ombi bali ni amri
Bado hujasema yote . endelea kusema mpaka umalize .
 
Mimi ni bosi tayari sihitaji uteuzi na ni tajiri sana
Kwani lowasa hakuwa tajiri. Vipi kuhusu Abood au Rostam. Vipi kuhusu Truph au Hichilema. Uongozi ni utumishi kwa watu.wapo watu wengine wanahitajika katika serikali ili kuleta fikra mpya na siyo kwenda kutafuta pesa.ndio maana unakuta wengine wanaupeleka mshahara wao kwa watu wenye uhitaji.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…