Dkt. Tulia aitetemesha Mbeya. Atua kijeshi na ndege ya Jeshi

Dkt. Tulia aitetemesha Mbeya. Atua kijeshi na ndege ya Jeshi

Ndugu zangu watanzania,

Haijapata kutokea ,haijapata kuonekana kwa mapokezi makubwa aliyoyapata mh Dkt Tulia Acksoni Mwansasu mbunge wa Mbeya mjini,speaker wa Bunge na Rais wa umoja wa mabunge Duniani ni mapokezi ya kishindo,ni mapokezi ya karne,ni mapokezi ya kihistoria ni mapokezi yaliyovunja rekodi,ni mapokezi yaliyoitetemesha na kulisimamisha Jiji la mbeya.watu wamehudhuria haijapata kutokea,mafuriko ya watu wamemiminika haijapata kuonekana.

Kwa hakika Dr Tulia ni mpango wa Mungu mwenyewe,anapendwa na kuheshimika na wanambeya ni haijapata kutokea ,anakubalika na kuungwa mkono ni haijapata kushuhudiwa ,itachukuwa miaka mingi sana kwa kiongozi yeyote yule kupata mapokezi aliyoyapata leo hii Dr Tulia.mtoto wa Mbeya kapokelewa kishujaa Mithili ya wanajeshi waliotoka vitani na kurejea na ushindi wa kukomboa ardhi ya nchi na Taifa lao iliyokuwa imeporwa.

Kapokelewa na watu wa rika zote na makundi yote kuanzia viongozi wa dini, serikali,mila,vijana,akina mama,wazee n.k.kishindo chake kimeteka jiji la Mbeya, kwa hakika ujio wake tokea angani aliko kuwa akiingia na ndege ya jeshi kumefanya jiji lote kulipuka kwa shangwe, nderemo na vifijo ambayo haijawahi kutokea.

Rai yangu kwa upinzani na mtu yeyote yule asithubutu kuchukua Fomu ya ubunge kugombea ubunge jimbo la Mbeya mjini maana kwa hali iliyopo kwa sasa na kwa namna Dkt. Tulia anavyopendwa na kukubalika kwa hakika itakuwa ni kupoteza muda na fedha kushindana na Rais wa IPU Dkt. Tulia Acksoni mwansasu katika sanduku la kura.

Dr Tulia siyo mtu wa kawaida ,ana nguvu fulani ndani yake isiyo ya kawaida na ya ajabu sana yenye kuonyesha uwepo wa Mungu ndani yake hasa kwa kuzingatia ukweli kuwa Dr Tulia ni mcha Mungu mkubwa na mwenye kumtegemea na kumtumainia Mungu kwa kila jambo.upepo wa Dr Tulia ni mkali na wenye mvumo wa kipekee sana,ni mtu mwenye ushawishi wa hali ya juu sana. Kwa hakika kaiteka mioyo ya wana Mbeya na kutembea mioyoni mwao.

Ni faraja kwa wana Mbeya ni fahari kwa wana nyanda za juu kusini na ni Nembo kwa wana mbeya. ameuheshimisha mkoa ,amelipa hadhi jiji,amewafanya wana Mbeya watembee kifua mbele na kwa kujiamini .na kila mtu anaona anastahili kuringa na kujivunia Dr Tulia kwa kuwa ni Mbeya ndio iliyompeleka Bungeni Dr Tulia na ni Mbeya ndio iliyotoa Rais wa umoja wa mabunge Duniani kati ya nchi zaidi ya 180 wanachama wa IPU Duniani kwote.

ndio maana wana Mbeya wamefanya mapokezi ya kishindo na ya heshima kubwa sana kumpatia mtoto wao na dada yao na mbunge wao Dkt Tulia Acksoni mwansasu kwa ushindi na heshima ya kipekee aliyolipatia jiji la Mbeya.kila mmoja anajiona kuwa kupitia kura yake ya ndio kwa Dkt Tulia Taifa limepata heshima ya kutoa Rais wa IPU na mwanamke wa kwanza kutoka Barani Afrika kushinda na kushika urais wa IPU.

Kazi iendelee mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
Mpango wa mungu nil ile mitume iliyokufa
 
Bila picha huo ni UCHAWA NA UNAFIKI
NA MNAFIKI NA MUONGO WACHOMWE MOTO
 
Ukiwa umevuta mibangi yako na kulewa gongo zako ulisema kuwa hawezi kushinda urais wa IPU. Lakini ukiwa na macho yako uliona alivyoshinda kwa kishindoo kilichoitetemesha Dunia nzima ,na matokeo yake ukakimbia na kuhamisha magoli.kwa hiyo hata haya unauoyazungumza hapa hata wewe unafahamu kuwa Dr Tulia ndio chaguo la wana Mbeya na ndiye anayekwenda kuzoa kura zote jijini Mbeya. Wewe andaa tu mibangi yako ili ukawage unavuta kupunguza maumivu.
Sijawahi kuzungumzia juu ya yeye kuwa Rais wa IPU. Naona umechanganya mafaili,hizi ni dalili za wenda wazimu.
 
Acha uongo wako hapa wewe.Dr Tulia ni kipenzi cha wanambeya ndio maana watu wamemiminika kwa kishindo kumlaki na kumpokea mtoto wao kipenzi aliyewaheshimisha na kulipatia heshima Taifa
Broo umeonwa kwenye. Loli la ngombe bhna hayo ni kwel lakin
 
Sijawahi kuzungumzia juu ya yeye kuwa Rais wa IPU. Naona umechanganya mafaili,hizi ni dalili za wenda wazimu.
Huwezi ukakumbuka na wala kichwa chako hakiwezi kutunza kumbukumbu,kwa kuwa ulishaathiriwa na moshi wa bangi unazovuta bila kipimo na kunywa migongo kama Mwendawazimu 😄😄😄
 
Broo umeonwa kwenye. Loli la ngombe bhna hayo ni kwel lakin
Hakuna aliyebebwa wala kushurutishwa kwenda bali watu walienda kwa hiyari yao na upendo wao kwa Dr Tulia.lakin pia ukiona watu wanakubali kupanda magari na kusafiri umbali mrefu kuja kukusikiliza au kumuona kiongozi fulani basi ujuwe kuwa wana imani kubwa sana na huyo kiongo, wanamkubali na kumuunga mkono na ndio maana wanakuwa wapo tayari kuacha shughuli zao ili wakamlaki na kujumuika naye.
 
Huwezi kujua maana umejifanya mtumwa kwa viongozi Ili wakutoe kimaisha. Ila ni bonge la aibu kuishi kwa kujipendekeza.
Mimi naishi kwa jasho langu mwenyewe na siyo kupitia kujipendekeza. Naongea ukweli na wala sioni aibu kumpongeza na kumtia moyo anaye fanya vizuri kazi yake
 
Huwezi ukakumbuka na wala kichwa chako hakiwezi kutunza kumbukumbu,kwa kuwa ulishaathiriwa na moshi wa bangi unazovuta bila kipimo na kunywa migongo kama Mwendawazimu [emoji1][emoji1][emoji1]
Luka uwezo wako ni mdogo sana. Mimi sikujadili kuhusu hiyo nafasi ya Rais wa IPU kwani kwangu mimi ni irrelevant kabisa ndiyo maana sikulijadili. Usilazimishe mambo kwani wewe ni mshabiki kama walivyo washabiki wa Simba na Yanga tu. Nimekudharau sana. Ndiyo maana unajitoa ufahamu kila siku kujaza mabandiko ambayo hayana maudhui zaidi ya ushabiki na unazi. Mimi siko huko kabisa.
 
Mimi naishi kwa jasho langu mwenyewe na siyo kupitia kujipendekeza. Naongea ukweli na wala sioni aibu kumpongeza na kumtia moyo anaye fanya vizuri kazi yake
Hakuna anayeishi kwa jasho lake akawa na tabia za kike hivi.
 
Luka uwezo wako ni mdogo sana. Mimi sikujadili kuhusu hiyo nafasi ya Rais wa IPU kwani kwangu mimi ni irrelevant kabisa ndiyo maana sikulijadili. Usilazimishe mambo kwani wewe ni mshabiki kama walivyo washabiki wa Simba na Yanga tu. Nimekudharau sana. Ndiyo maana unajitoa ufahamu kila siku kujaza mabandiko ambayo hayana maudhui zaidi ya ushabiki na unazi. Mimi siko huko kabisa.
Kwa hiyo wewe kwa mibangi yako unaona kwamba mimatusi yako unayoporomosha humu jukwaani muda wote ndio yana maudhui? Kweli mibangi imekuharibu sana akili na kukupa upofu wa akili na macho. Wewe endelea tu na matibabu yako ya magonjwa ya akili 😄😄😄
 
Back
Top Bottom