Dkt. Tulia anataka awe Spika wa Bunge lisiloweza kufanya chochote?

Dkt. Tulia anataka awe Spika wa Bunge lisiloweza kufanya chochote?

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Sijui kama ni unafiki, ulaghai, akili kidogo au tamaa, ambavyo huweza kumfanya mtu kuwa mtumwa wa ujinga.

Hivi karibuni, Naibu Spika Tulia, mbele ya Rais wakati Rais akiwaapisha mawaziri aliowateua, alitamka wazi kuwa Rais na Serikali, ni kila kitu. Na kwamba, japo Bunge linaweza kuishauri Serikali, lakini Serikali hailazimiki kufuata ushauri wa Bunge.

Kwa maneno haya, maana yake Bunge haliwezi kubadilisha chochote ambacho Rais au Serikali wanataka. Kiuhalisia, hii inamaanisha kuwa uwepo wa Bunge hauna maana. Kila kitu kinaweza kufanywa na Rais na Serikali. Kama ndivyo, kwanini pesa ya walipa kodi iendelee kuhudumia taasisi ambayo haina msaada wowote?

Kama bunge haliwezi kubadilisha chochote ambacho Serikali na Rais wanataka, si aheri Bunge lisingekuwepo, na hiyo pesa inayopotea, Serikali na Rais wakaitumia kuwaletea wananchi huduma muhimu?

Kioja zaidi ni pale Samia aliyesema Bunge si chochote mbele ya Rais na Serikali, anagombea uongozi wa taasisi ambayo, kitafsiri, haina maana yoyote! Kama Bunge halina maana yoyote mbele ya Rais na Serikali, anataka uongozi kwenye chombo kama hicho kwaajili ya nini? Ni uroho na tamaa ya mapato binafsi au kuna kitu kingine?
 
... anachokitafuta sio kuwatumikia wananchi; wala sio kulipeleka taifa mbele. Kinachomsukuma kugombea ni tamaa ya mshahara mnono, posho, marupurupu, na stahili za Spika na ile kinga ya kutoshtakiwa popote sasa na baada ya kustaafu. Hayo ndio ya muhimu kwake, mengine geresha tu.

Muulize ana agenda gani ya kugombea uspika kama atakujibu kitu cha maana! Ambaye bado hajawastukia hawa jamaa akapimwe akili! Huyo yuko kwenye usingizi wa pono.
 
... anachokitafuta sio kuwatumikia wananchi; wala sio kulipeleka taifa mbele. Kinachomsukuma kugombea ni tamaa ya mshahara mnono, posho, marupurupu, na stahili za Spika na ile kinga ya kutoshtakiwa popote sasa na baada ya kustaafu. Hayo ndio ya muhimu kwake, mengine geresha tu...
Kwa kutegemea watu kama hawa, nchi itaendelea kuwa mkia japo Mungu hakuifanya iwe hivyo.
 
Umasikini wa nchi nyingi za Kiafrika ni wa kujitakia, tunakusanya pesa nyingi kupitia kodi na vyanzo vingine lakini namna tunavyo tumia hizo pesa ndio kichekesho kabisa; kama unavyo sema, hivi tunayo sababu hata 1 ya sisi kua na BUNGE!?

(Kwa matamshi ya naibu spika) Kama usemavyo, binafsi siuoni kabisa umuhimu wa bunge, bunge lingevunjwa halafu tutafute namna nyingine ya kuwapata mawaziri, tukivunja bunge tuta sevu pesa nyingi sana ambazo kimsingi tunazitumia kwasababu zisizo na maana yoyote.
 
Yeye mwenyewe ameshajiona mbwa mbele ya chatu, hafai tena kwenye nafasi hiyo, aendelee na mapambio yake kwa chifu hangaya.
 
Hivi karibuni, Naibu Spika Tulia, mbele ya Rais wakati Rais akiwaapisha mawaziri aliowateua, alitamka wazi kuwa Rais na Serikali, ni kila kitu. Na kwamba, japo Bunge linaweza kuishauri Serikali, lakini Serikali hailazimiki kufuata ushauri wa Bunge.

Kwa maneno haya, maana yake Bunge haliwezi kubadilisha chochote ambacho Rais au Serikali wanataka. Kiuhalisia, hii inamaanisha kuwa uwepo wa Bunge hauna maana.

Kila kitu kinaweza kufanywa na Rais na Serikali. Kama ndivyo, kwanini pesa ya walipa kodi iendelee kuhudumia taasisi ambayo haina msaada wowote?
 
Mambo ya CCM hayo ,hayanishughulishi kabsaa,wakichaguana wakiraruana ,wakitishana,wakiuwana ni yao ,inakuwaje unashobokea watu wasio na faida kwa raia?

Huyasoma nione uzuzu wao namna wanavyozuzuana wakijitekenya wenyewe wakicheka wenyewe. Na zaidi kuona watu wazima wanavyodanganyana, maana liccm linaposema kuwambia wenzake tumeshinda,

ujuwe wanaomsikiliza wametoa macho wakidanganywa, sasa kama ni chama cha wadanganyana ,kuna maendeleo ya nchi hapo? 10% inayofikia trilions
 
Kauli ya Tulia ilikuwa ni kielelezo tu cha wengi waliopo huko CCM, hata akitokea mwingine akachaguliwa bado nae atakuwa na mtazamo kama huo wa Tulia.

Naona kama Tulia aliitoa ile kauli makusudi ili ajipigie kampeni ya uspika, akijua fika Rais ndie mwenye nafasi kubwa ya kumuweka pale mtu atakaemtaka.
 
Kodi ya watanzania inayokusanywa kwa kiwango kikubwa kinawahudumia baadhi ya watu na taasisi ambazo ziko kinyume na viapo vyao kwa mujibu wa katiba, hawasaidii wananchi nabadala yake nikinyume chake''
 
Sijui kama ni unafiki, ulaghai, akili kidogo au tamaa, ambavyo huweza kumfanya mtu kuwa mtumwa wa ujinga.

Hivi karibuni, Naibu Spika Tulia, mbele ya Rais wakati Rais akiwaapisha mawaziri aliowateua, alitamka wazi kuwa Rais na Serikali, ni kila kitu. Na kwamba, japo Bunge linaweza kuishauri Serikali, lakini Serikali hailazimiki kufuata ushauri wa Bunge.

Kwa maneno haya, maana yake Bunge haliwezi kubadilisha chochote ambacho Rais au Serikali wanataka. Kiuhalisia, hii inamaanisha kuwa uwepo wa Bunge hauna maana. Kila kitu kinaweza kufanywa na Rais na Serikali. Kama ndivyo, kwanini pesa ya walipa kodi iendelee kuhudumia taasisi ambayo haina msaada wowote?

Kama bunge haliwezi kubadilisha chochote ambacho Serikali na Rais wanataka, si aheri Bunge lisingekuwepo, na hiyo pesa inayopotea, Serikali na Rais wakaitumia kuwaletea wananchi huduma muhimu?

Kioja zaidi ni pale Samia aliyesema Bunge si chochote mbele ya Rais na Serikali, anagombea uongozi wa taasisi ambayo, kitafsiri, haina maana yoyote! Kama Bunge halina maana yoyote mbele ya Rais na Serikali, anataka uongozi kwenye chombo kama hicho kwaajili ya nini? Ni uroho na tamaa ya mapato binafsi au kuna kitu kingine?
Wanasiasa wanaonekana ni wasomi wanaozikataa taaluma zao. Au taaluma zao zimewakataa. Ukweli kawao ni kama giza tu. Tatizo kubwa llipo kwetu tuanaowaimbia mapambio
 
Anataka kuongeza urefu wa kamba yake ili apate eneo kubwa zaidi la ulaji
 
Hilo Bunge wangevunja na kuwapa Ofisi pale Ikulu itakuwa rahisi ku-rubber stamp maamuzi ya Serikali / watawala
 
Back
Top Bottom