Uchaguzi 2020 Dkt. Tulia bado unayo nafasi na muda wa kubadili Jimbo la kugombea

HUYU MAMA ANAPOTEZA MUDA MBEYA..NA HATA AKILAZIMISHA KUTANGAZWA ATAKUWA ONE TERM MP KWANI MWAKA 2025 HATAKUWA NA WA KUMTANGAZA ...BORA AENDE TUKUYU KWAO ATAKUA NA UHAKIKA WA KUWA MBUNGE MUDA MREFU KIDOGO
Hata mimi nashauri akagombee jimbo mojawapo la Rungwe kwao huko anaweza kuwa mbunge tena wa muda mrefu kama akina Ndugai. Asivutike na mbeya mjini kisa yupo mbunge wa upinzani, wala asiogope majimbo ya Rungwe kwao kwa sababu kuna wabunge wa CCM huko ndo ubunge kwake utanoga. Mbeya mjini ni pagumu kwa sababu watu wa pale wameshaelimika hata wamachinga mbeya mjini ni wajanja sio sawa na wakulima wa huko Rungwe. Ubunge wa kutegemea kudhurumu matokeo kwa ubabe sio mzuri kama ule wa kupigiwa kura na wanavijiji wa majimbo ya Rungwe. Mbeya mjini ni pagumu sana kwa CCM wakati huu.
 
hiyo video hapo,hao raia ndo wapiga kura wote wa Chadema.
ambao hawapo ni wengi zaidi ambao ndo wapiga kura wa Dr.tulia.
 
Mkuu naona umelewa ndo unatype Nani amekwambia Dodoma ndo shamba la Bibi jiheshimu
Dodoma wakiona kijana tu wanajaza kura, sijui wameathiriwa na rangi ya viwavi! [emoji2]
 
Ukabila unaingia kwa Kasi...na majitu fulani fulani..hii dhambi hiiiii!!
 
Dodoma ni makao makuu ya chama tawala na serikali Kuna watu huona Kama wakazi wa Dodoma ni Wajinga kuchagua CCM lakini sio kweli wakazi wa Dodoma wanajua kulipa fadhira kwa kile ambacho CCM imewatendea bila CCM huenda Dodoma ingekua na Hali mbaya Sana kwa sababu ni mkoa ambao ni nusu jangwa na umenyimwa Mali asili Kama mbuga za wanyama,madini na vitu vingine kwaio Dodoma na CCM Wana vinasaba
 
Tulia anaonekana kiongozi mzuri ila asidanganyike na wanaotaka kumtupa shimoni Mbeya , akienda huko Tukuyu au Chunya atadumu kwenye uongozi kama Mama Anne Makinda ......najua kuna wanaofaidika na pesa yake kumshawishi agombee Mbeya mjini wakijua hawezi kushinda labda aibe kura au ubabe .....hatafurahia kuona damu inamwagika ili yeye atangazwe na hata ikiwa hivyo ...atakaa hiyo miaka mitano tu !
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…