Dkt. Tulia: Nyanda za Juu tumechoka kuwa washangiliaji na sisi tunataka treni ya umeme kama 'Wenzetu'

Dkt. Tulia: Nyanda za Juu tumechoka kuwa washangiliaji na sisi tunataka treni ya umeme kama 'Wenzetu'


Mbunge wa Mbeya Mjini Dr. Tulia amemtaka Waziri wa Ujenzi kuangalia namna ya kuiwezesha TAZARA kuwa na treni ya umeme.
Dr. Tulia amesema Tanzania ni moja na Wananchi wa pande zote wanahitaji maendeleo hivyo Kanda ya Nyanda za Juu Jusini wamechoka kuwa washangiliaji.

Kadhalika Dr Tulia amelalamikia Jiji la Mbeya kutopewa hadhi na Huduma stahiki kama ilivyo katika majiji mengine na badala yake Mbeya imekuwa kama Halmashauri.

Tulia amesema miundombinu ya Mbeya ni mibovu sana na miaka yote wamekuwa wakipewa bajeti ndogo isiyokidhi chochote.

Dr. Tulia alikuwa akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Ujenzi.

Source: Bungeni
Mimi sio mwanasiasa,lakini alichosema muheshimiwa Dr Tulia ni sahihi kabisa,maparachichi yanatoka Mbeya,Njombe,Songea,mahindi,chai,kahawa,ndizi,maharage,magimbi nk,lakini miundo mbinu toka uhuru hadi sasa kimya,na huku kodi ikitakiwa sana.Na vilevile ni mkoa uliokaribu na mipaka ya nchi mbili!Iweje iwe na miundo mbinu mibovu huku tunataka kodi?Waziri alione hili bila kigugumizi wala soni.Kazi iendelee.
 
Kadhalika Dr Tulia amelalamikia Jiji la Mbeya kutopewa hadhi na Huduma stahiki kama ilivyo katika majiji mengine na badala yake Mbeya imekuwa kama Halmashauri.

Tulia amesema miundombinu ya Mbeya ni mibovu sana na miaka yote wamekuwa wakipewa bajeti ndogo isiyokidhi chochote
Mfuatilie kaka yake Tulia kuanzia dakika ya 5-13
 
alikuwa wapi siku zote asiongee..anyamaze tuiponye nchi kwanza , angeongea kipindi cha awamu ya tano ndo tunemskiliza vizuri
 
.
FB_IMG_1620898147256.jpg
 

Mbunge wa Mbeya Mjini Dr. Tulia amemtaka Waziri wa Ujenzi kuangalia namna ya kuiwezesha TAZARA kuwa na treni ya umeme.
Dr. Tulia amesema Tanzania ni moja na Wananchi wa pande zote wanahitaji maendeleo hivyo Kanda ya Nyanda za Juu Jusini wamechoka kuwa washangiliaji.

Kadhalika Dr Tulia amelalamikia Jiji la Mbeya kutopewa hadhi na Huduma stahiki kama ilivyo katika majiji mengine na badala yake Mbeya imekuwa kama Halmashauri.

Tulia amesema miundombinu ya Mbeya ni mibovu sana na miaka yote wamekuwa wakipewa bajeti ndogo isiyokidhi chochote.

Dr. Tulia alikuwa akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Ujenzi.

Source: Bungeni
Pamoja na mimi kutoka kanda pendwa lakini Tulia kasema kweli.
 
Hayati Mwl. Nyerere alisema kuna watu tabia yao ni kudai tu, wanadai, wanadai hata bila ku reason, ni kudai na kudai hata bila kuangalia resources kama zinakidhi hayo wanayodai.

Sasa huyu tulidhani angekuwa mhubiri na mwelimishaji kwa wananchi kujifunza kuwa na subira, lakini ndiye huyo!!!
Msilete hizoo!
Ni Mwalimu aliyewekeza barabara mikoa ya Mbeya na Iringa.
Wengine wote wanapita tu utafikiri mikoa hiyo haipo duniani.
Barabara ya Tanzam ilijengwa 60's na kukarabatiwa miaka inayofuata.
Hii haiwiani na mikoa iliyozungushiwa barabara mpaka wanachoka wenyewe, hasa huko kwa mwendazake.
 

Mbunge wa Mbeya Mjini Dr. Tulia amemtaka Waziri wa Ujenzi kuangalia namna ya kuiwezesha TAZARA kuwa na treni ya umeme.
Dr. Tulia amesema Tanzania ni moja na Wananchi wa pande zote wanahitaji maendeleo hivyo Kanda ya Nyanda za Juu Jusini wamechoka kuwa washangiliaji.

Kadhalika Dr Tulia amelalamikia Jiji la Mbeya kutopewa hadhi na Huduma stahiki kama ilivyo katika majiji mengine na badala yake Mbeya imekuwa kama Halmashauri.

Tulia amesema miundombinu ya Mbeya ni mibovu sana na miaka yote wamekuwa wakipewa bajeti ndogo isiyokidhi chochote.

Dr. Tulia alikuwa akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Ujenzi.

Source: Bungeni
Wakati watu wanalalamika kuwa jiwe linapendelea kanda maalum hawa ndio walikuwa wanatunanga kwa kusema hata chato ni Tanzania na wote waliohoji wakahusishwa na Uchaga/Kilimanjaro. Leo ni nini kimemkuta tena
 

Mbunge wa Mbeya Mjini Dr. Tulia amemtaka Waziri wa Ujenzi kuangalia namna ya kuiwezesha TAZARA kuwa na treni ya umeme.
Dr. Tulia amesema Tanzania ni moja na Wananchi wa pande zote wanahitaji maendeleo hivyo Kanda ya Nyanda za Juu Jusini wamechoka kuwa washangiliaji.

Kadhalika Dr Tulia amelalamikia Jiji la Mbeya kutopewa hadhi na Huduma stahiki kama ilivyo katika majiji mengine na badala yake Mbeya imekuwa kama Halmashauri.

Tulia amesema miundombinu ya Mbeya ni mibovu sana na miaka yote wamekuwa wakipewa bajeti ndogo isiyokidhi chochote.

Dr. Tulia alikuwa akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Ujenzi.

Source: Bungeni
Asante Dr Tulia , at last Mbeya tumepata sauti ya kudai na sisi maendeleo ya Jiji kama ilivyo Mwanza, ARusha na hata Dar es salaam.

Kwa makusudi toka Awamu ya Pili, Tatu na Nne na Tano HAKUNA uwekezaji wa maana ulioingia Mbeya, si barabara , viwanda au hata huduma za kiwango cha kitaifa.
 
Wakati watu wanalalamika kuwa jiwe linapendelea kanda maalum hawa ndio walikuwa wanatunanga kwa kusema hata chato ni Tanzania na wote waliohoji wakahusishwa na Uchaga/Kilimanjaro. Leo ni nini kimemkuta tena
Ndio maana amesema " tumechoka kushangilia"
 
Asante Dr Tulia , at last Mbeya tumepata sauti ya kudai na sisi maendeleo ya Jiji kama ilivyo Mwanza, ARusha na hata Dar es salaam.

Kwa makusudi toka Awamu ya Pili, Tatu na Nne na Tano HAKUNA uwekezaji wa maana ulioingia Mbeya, si barabara , viwanda au hata huduma za kiwango cha kitaifa.
Ahsante bwashee

kny Dr Tulia
 

Mbunge wa Mbeya Mjini Dr. Tulia amemtaka Waziri wa Ujenzi kuangalia namna ya kuiwezesha TAZARA kuwa na treni ya umeme.
Dr. Tulia amesema Tanzania ni moja na Wananchi wa pande zote wanahitaji maendeleo hivyo Kanda ya Nyanda za Juu Jusini wamechoka kuwa washangiliaji.

Kadhalika Dr Tulia amelalamikia Jiji la Mbeya kutopewa hadhi na Huduma stahiki kama ilivyo katika majiji mengine na badala yake Mbeya imekuwa kama Halmashauri.

Tulia amesema miundombinu ya Mbeya ni mibovu sana na miaka yote wamekuwa wakipewa bajeti ndogo isiyokidhi chochote.

Dr. Tulia alikuwa akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Ujenzi.

Source: Bungeni
Salamu zimfikie Sugu ambaye alikuwa anazungusha tu makalio na kutukana watu mle jengoni.
 
Bora hata wangeililia watu wa kutoka Tanga, Kilimanjaro na Arusha! Ila siyo Nyanda za Juu Kusini! Maana hao wamejengewa treni ya kisasa kabisa ya TAZARA! Lakini wameshindwa kuishawishi Serikali kuiboresha ili iwe na tija.

Leo hii ukisafiri na treni ya TAZARA, utashuhudia tu magofu ya majengo kwenye stesheni zake, na huduma mbovu! Huku abiria na mizigo ikiwa ni ya kutosha tu.
Na je ya kati hakuna magofu na majengo kama vibanda umiza lakini wanajengewa treni ya umeme,kumbuka mikoa ya nyanda za juu kusini ndio zamani ikiitwa big 4 na sasa ni big 6, tunawalisha nyie wote, na tunalipa kodi zaidi hata ya hao ambao unawakingia kifua.
 
Back
Top Bottom