Dkt. Wilbert Kleruu - Utata wa kifo chake, historia na maisha yake

Dkt. Wilbert Kleruu - Utata wa kifo chake, historia na maisha yake

Jamaa kukuzaba kibao mbele ya watoto wako na mke ni dharau kubwa mno.Usipotetea haki yako wakati huo basi wewe hata ukiishi miaka elfu hapa duniani huna faida yoyote. Kuna mambo mengine hayakubaliki kabisa.

I know one thing, ni kwamba Wahehe walimlilia sana Chief wao Adam Sapi, afanye kila awezalo kumuokoa Mwamwindi, asinyongwe. Sapi alijaribu kila njia kumuokoa Mwamwindi kwa kumbembeleza sana Mwalimu na Kawawa, lakini Mwalimu aliweka mguu chini. Infact yeye Sapi na Mwakawago, waliishia kwua wanasiasa very unpopular huko Iringa kwa sababu ya kushindwa kumuokoa Mwamwindi,

Chief Sapi, aliacha kabisa kwenda Iringa, na Mwakawago alishia hata kutokujenga nyumba kabisa huko Iringa, na hata ule ubunge aliokuwa akiupata ilikuwa ni kwa sababu ya kumuoa dada wa Sapi, ambapo Sapi alipofarikit tu ukawa mwisho wake wa ubunge na uwaziri.

Kwa maneno yake mwenyewe Mwalimu, kitendo cha kusaini kifo cha Mwamwindi, kilikuwa kikimtesa sana Mwalimu, aliyekua akitembea na Biblia kila mahali akimuomba Mungu amsamehe, kwa sababu ndiye aliyekwua the only mwananchi aliyenyongwa kwa saini yake.

Ahsante Wakuu.
 

Kwa maneno yake mwenyewe Mwalimu, kitendo cha kusaini kifo cha Mwamwindi, kilikuwa kikimtesa sana Mwalimu, aliyekua akitembea na Biblia kila mahali akimuomba Mungu amsamehe, kwa sababu ndiye aliyekwua the only mwananchi aliyenyongwa kwa saini yake.


Mkuu umekosea kidogo hapo kwenye data, tutasahihishana:

MAJADILIANO YA BUNGE
MKUTANO WA KUMI Kikao cha Pili – Tarehe 30 Januari, 2008


SWALI: MHE. MUDHIHIR M. MUDHIHIR (CCM, Mchinga) (K.n.y. MHE. RICHARD M. NDASSA, (CCM, Sumve)

"Je, kuanzia uongozi wa nchi wa Awamu ya Kwanza hadi Awamu hii ya Nne, ni watu wangapi wamekwishanyongwa na ni awamu gani iliyoridhia utekelezaji wa hukumu hiyo?"

JIBU: NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA, MHE. MATHIAS CHIKAWE (CCM, Nachingwea)

"Mheshimiwa Spika, jumla ya watu 82 wamenyongwa kuanzia awamu ya kwanza hadi awamu hii ya nne. Kati ya watu hao, 10 walinyongwa wakati wa awamu ya kwanza na 72 walinyongwa wakati wa awamu ya pili. Hakuna ambaye alinyongwa wakati wa awamu ya tatu na awamu ya nne."


Habari ndio hiyo!
 
wakati dr kleruu akiwahamisha wahehe toka vijiji vyao vya asili kwake kule marangu mambo yalikuwa tofauti, bado alikuwa anamiliki kihamba chake, na hakuhamia kwenye vijiji vya ujamaa. ni ule msemo maarufu kuwa WANASIASA HUWA WAANAHUBIRI UBORA WA KUNYWA MAJI KWA WAFUASI WAO, WAKATI WAO WANAKUNYWA DIVAI
 
  • Thanks
Reactions: amu
wakati dr kleruu akiwahamisha wahehe toka vijiji vyao vya asili kwake kule marangu mambo yalikuwa tofauti, bado alikuwa anamiliki kihamba chake, na hakuhamia kwenye vijiji vya ujamaa. ni ule msemo maarufu kuwa WANASIASA HUWA WAANAHUBIRI UBORA WA KUNYWA MAJI KWA WAFUASI WAO, WAKATI WAO WANAKUNYWA DIVAI

Kule Kili sidhani kama kulikua na vijiji vya ujamaa as such, au? Mwenye kujua anifahamishe, ni mikoa yote ili embrace hiyo doctrine ya vijiji vya ujamaa?
 
wakati dr kleruu akiwahamisha wahehe toka vijiji vyao vya asili kwake kule marangu mambo yalikuwa tofauti, bado alikuwa anamiliki kihamba chake, na hakuhamia kwenye vijiji vya ujamaa. ni ule msemo maarufu kuwa WANASIASA HUWA WAANAHUBIRI UBORA WA KUNYWA MAJI KWA WAFUASI WAO, WAKATI WAO WANAKUNYWA DIVAI

Mkuu ... vijiji vya ujamaa vilikuwa na kwa 'watu wa porini tu....' watu wasio na makazi ya kudumu... 🙂
 
Kule Kili sidhani kama kulikua na vijiji vya ujamaa as such, au? Mwenye kujua anifahamishe, ni mikoa yote ili embrace hiyo doctrine ya vijiji vya ujamaa?

Injinia,
Tatizo la Moshi lilikuwa ni overpopulation. Mwalimu aliwaambia wahamie Mwesi wenyewe wakasema Wamarekani walikwenda mwesini wakarudi.
Usingeweza kuanzisha vijiji vya ujamaa Moshi kwa sababu ardhi ilikuwa imeshachukuliwa/tumika yote.
 
Mkuu umekosea kidogo hapo kwenye data, tutasahihishana:

Kwa maneno yake Mwalimu alisaini kunyongwa kwa mwananchi mmoja tu, Mwamwindi na siku zote alikuua akitembea na Biblia akimuomba Mungu amsamehe, maana yake inaweza kua moja tu kuwa hivyo vifo vingine 9 katika awamu yake vilisainiwa na wengine, kwa maelekezo yake or else!

Masahihisho ni kitu kizuri sana, ila yafanyike pale kwenye makosa tu!
 
Du inaonekana hii issue inachanganya kidogo, kwa mtizamo wa haraka haraka unaweza kusema kuwa Mwamwindi ndiye alikuwa mwana mapinduzi hapa lakini ukiangalia pia issue ya mada sina uhakika wana sheria watasemaje, ni dhahiri kuwa hata kama angekuwa ameuwa kwa kutokukusudia mwelekeo wa siasa wa kipindi hicho kwa vyevyote ungemhukumu tu kwa kumuondoa mkuu wa Mkoa ( I am only speculating though). Pia ukifuatilia hizi post za wana JF waliochangia na kutoa maelezo ya huyu Dr Kleruu, kwa upande mwingine inaonekana kama hasa alikuwa mkereketwa wa ujamaa au alikuwa anatumia madaraka yake vibaya. Nafikiri angeweza kuwa na compromising solution ya kudeal na watu ambao walikuwa na mashamba makubwa zaidi ya hivo alivofanya kama maelezo ya Kithuku yanavyosema hapa:

GM,
Napenda nichangie kidogo kuhusu hiyo speculation yako. Hujakosea... kesi ya Mwamwindi ina mambo mengi ndani yake yanayoathiri matumizi sahihi ya principles of law. Siasa ilikuwa ni major consideration..pamoja na kuwa mahakama inatakiwa iwe huru kufuatana na separation of powers... kipindi kile tukumbuke kulikuwa na some kind of fussion baina ya ile mihimili mitatu mikuu ya serikali.. na chama kilikuwa ndiyo kimeshika hatamu na siyo bunge wala nini! Executive nayo ilikuwa imemeza nguvu ya bunge na hata mahakama!..Kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu kipindi hicho na ndiyo maana hata katiba ya nchi haikuwa na bill of rights kama tulivyo nayo sasa baada ya mageuzi ya kiuchumi na kisiasa.
 
DR Kleruu na Nyerere walihusika sana katika kuwatia umaskini wakulima wa mkoa wa Iringa kwa kuwageuza kutoka wakulima wakubwa na kuwa wakulima wadogo wa kilimo cha kujikimu.

Huko nyuma kabla ya sera vijiji vya ujamaa matajiri wa Iringa walikuwa ni wakulima.Walikuwa wakimiliki magari na matrekta mapya ya kisasa wakiwa huko huko vijijini.(sijwahi kuona wala kusikia kuwa wakulima kabla ya sra potofu ya vijiji vya ujamaa walikuwa wakinunua magari na matrekta ya mitumba au used kama siku hizi kutoka majalala ya wakulima wa ulaya au Japan).

Iringa ofisi za wauzaji magari na matrekta mapya zilikuwepo Iringa na show rooms zao zilikuwa na matrekta na magari mapya. Wateja wao wakubwa walikuwa ni wakulima.

Mfano Mwamwindi alikuwa ni tajiri mkulima wa kijijini aliyekuwa na magari na matrekta ya kulima kwenye mashamba yake makubwa na kuyakodisha kwa wengine wenye mashamba makubwa yanayohitaji kulima kwa trekta badala ya ng`ombe au jembe la mkono..

Mabasi ya abiria ya ndani ya Iringa na kuelekea hata safari za mbali kama kwenda Dar es salaam yalikuwa yakimilikiwa na wakulima waliokuwa wakiishi vijijini na sio mjini Iringa.Nyumba za kupangisha Iringa mjini nyingi zilikuwa zinamilikiwa na wakulima waishio vijijini wakilima mashama yao.

Hata wahindi walikuwa wakiwafuata vijijini wakulima kwenda kuwauzia bidhaa zikiwemo nguo (wahindi hao waliitwa guoguo sababu wakiuza nguo walikuwa wakisema guo guo bei rahisi ) wakijua soko lilikuweko vijijini.

Wakulima wa Iringa walishafikia kiwango cha kuwa wakulima wa Mashamba makubwa (ESTATES) ya mazao kama mahindi wakishindana na wagiriki waliokuwa na mashamba makubwa ya tumbaku.Kilimo cha mashamba makubwa ya waswahili ya kibiashara Iringa yalikuwepo kama ilivyo Kenya.

Nyerere akaleta vijiji vya ujamaa akanyang`anya mashamba makubwa akakatia watu ekari tatu tatu tu zingine akazifanya mashamba ya vijiji vya ujamaa.Toka hapo wakulima Iringa wakageuzwa kuwa wakulima wa kujikimu wa ekari tatu tatu toka wakulima wakubwa wa mashamba makubwa (Malungulu kwa lugha yao ya kihehe).

Sera za Nyerere na DR.Kleruu wake za kunyang`anya mashamba makubwa na kuyagawa zilikuwa za upendeleo kwani hazikugusa mashamba ya wagiriki au wazungu ambao walikuwa na mashamba makubwa wakilima au kufuga Iringa. Wengine wapo hadi leo na mashamba yao hayakuguswa mfano ni mwingereza PHILIPS Mwenye shamba la KIBEBE DAIRY FARM ambaye hadi leo yupo na hakuguswa na sera potofu za vijiji vya ujamaa.


Na Nyerere wakati ananyang`anya mashamba mashamba makubwa ili agawie watu wengine Iringa hakukuwa na tatizo la ardhi kama ilivyo Mkoa wa Kilimanjaro.Iringa ardhi ilikuwapo tele na hadi leo maeneo mengi yapo yasiyo na watu ambayo wangeweza kupeleka watu huko wakaanzishe vijiji vya ujamaa huko badala ya kupora ardhi za watu waliokwishawekeza mitaji yao na kuiendeleza kama Marehemu Mwamwindi.

Iringa ingeachwa bila kuingiliwa na sera mbovu za vijiji vya ujamaa sasa hivi ingekuwa na matajiri wengi wakulima wa mashamba makubwa wazawa kama ilivyo Kenya na Afrika ya KUSINI na umaskini uliokithiri ambao upo kila eneo ukipita Iringa usingekuwepo kwani wengi walishaanza kuwaiga wakulima wa mashamba makubwa ili nao wawe matajiri kwa kulima kisasa na kwa juhudi.Kilimo kilikuwa na heshima kubwa Iringa hadi kiliposhushwa heshima na nyang`anya nyang`anya ya mashamba.
 
  • Thanks
Reactions: amu
Kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu kipindi hicho na ndiyo maana hata katiba ya nchi haikuwa na bill of rights kama tulivyo nayo sasa baada ya mageuzi ya kiuchumi na kisiasa.

Strong point.
 
Kule Kili sidhani kama kulikua na vijiji vya ujamaa as such, au? Mwenye kujua anifahamishe, ni mikoa yote ili embrace hiyo doctrine ya vijiji vya ujamaa?

Moshi vijiji vya ujamaa vilianzishwa kule njia ya kuelekea Mabogini, kuna vijiji kule vya Mtakuja, Mvuleni, Newland, nk. Wakazi wa vijiji hivyo wengi wao ni wale waliokuwa manamba zamani kwenye mashamba ya miwa ya TPC, wa makabila ya wasafwa ambao waliletwa zamani na mkoloni, wakawa wanaishi kwenye mabanda ya TPC, vijiji vya ujamaa vilipoanzishwa wakapata ukombozi wakahamia huko. Hata hivyo bado waliendelea kutumika kwenye mashamba ya miwa, nadhani hadi leo wao ndio wakata miwa walio wengi kule. Vijiji vingine vya ujamaa kule Moshi vilianzishwa eneo la Kahe, anakotoka IGP Saidi Mwema, nako pia ni maeneo ya "mabondeni" ambako wachaga hawapendi kuishi ingawa huwa wanaenda kulima huko mahindi (ya biashara), wengi wanaoishi huko Kahe ni kabila "jipya" la wakahe, ambao lugha yao ni mchanganyiko wa kichaga, kipare, kikamba na kiluhya (reli ya Mombasa inapita hapo, kwa hiyo kuna watu wengi kutoka Kenya waliingia tangu wakati wa mjerumani). Vijiji hivyo vya Mtakuja, Mvuleni, Newland ndiko Zakia Meghji alipojichukulia ujiko mwaka 1990 alipokuwa Mkuu wa Wilaya ya Moshi Vijijini, palitokea Mafuriko nyumba nyingi zikazolewa na maji, Zakia Meghji akaweka kambi kule pamoja na vijana wa JKT wakawa wanawajengea upya wananchi nyumba zao zilizozolewa. Ilitangazwa sana kipindi kile hiyo habari kwenye magazeti na redio, na wapo kinamama wengi waliojifungua watoto kipindi kile wakaamua kuwapa majina ya Zakia kutokana na jinsi alivyokuwa anashinda nao na kulala hukohuko kwa zaidi ya mwezi mzima. Baada ya lile janga kuisha, ndipo rais Mzee Ruksa akampandisha Zakia cheo kuwa mkuu wa mkoa, na nyota yake ikazidi kung'ara tangu wakati huo hadi mwaka huu alipokumbwa na mzuka wa EPA!.
 
wakati dr kleruu akiwahamisha wahehe toka vijiji vyao vya asili kwake kule marangu mambo yalikuwa tofauti, bado alikuwa anamiliki kihamba chake, na hakuhamia kwenye vijiji vya ujamaa. ni ule msemo maarufu kuwa WANASIASA HUWA WAANAHUBIRI UBORA WA KUNYWA MAJI KWA WAFUASI WAO, WAKATI WAO WANAKUNYWA DIVAI

Havikuwepo vijiji vya ujamaa Uchagani .Labda Upareni.I stand to be corrected.
 
Na kama tukizungumzia Kilimanjaro kama mkoa, hata kule Mwanga kuna vijiji vya ujamaa vilianzishwa maeneo ya mabondeni, kama kuelekea ziwa Jipe, lakini huko nako hakukai wapare, kunakaa pia manamba wa zamani waliokuwa wanakata mkonge, nao pia waliletwa na wakoloni. Watu hao ni wa kabila la wanyamwanga (nadhani kutoka sehemu fulani ya Mbeya), na hadi leo hawachanganyiki na wapare, wanaishi mabondeni, na hata leo ukienda staili yao ya maisha ni kama ile ya wakati wa vijiji vya ujamaa.
 
Netanyau, ulichozungumza kimenigusa sana maana umegusa kitu ambacho nimekuwa nacho hadi hapa nilipo. Sera ile ilikuwa ni mbaya sana sisi tuliishi karibu na Kambi ya Jeshi Mafinga JKT, nakumbuka sana wanajeshi walikuwa wanakuja kumsumua baba maana naye mwanzoni alikataa kujiunga na Kijiji cha Ujamaa. Baada ya hap serikali ikaamua kutumia wanajeshi kutuhamisha kwa nguvu ikawa hivyo. Mali kibao ziliharibika kwa jua na mvua nyumba zilichomwa moto tukiwa watoto tuliingiwa na woga sana kuona hali ile Baba ambaye alikuwa ndiye tunaona ni mwenye nguvu hakufanya kitu mbele ya wanajeshi wa JKT. Alisukumwa huku na huku akitakiwa kuhama mara moja ifikapo jioni ile. Sisi kwa utoto wetu tukadhani ni vita maana wanajeshi na bunduki zao kwa raia asiye na hata mkuki. Tulikuwa tukilima mazao mbali mbali hata siku moja hatuwahi kuwaza kitu kiitwacho njaa lakini leo hii nchi imejibu. Baba alikuwa anamiliki mashamba makubwa huko Isimani kilomita kama 150 - 200 toka Mafinga nako mambo yakawa hayo hayo ya vijiji vya ujamaa. Umasikini tulijitakia. Tulikuwa na Irrigation scheme nzuri sana ambapo hata wakati wa kiangazi mazao yalikuwa yakilimwa lakini si leo. Umasikini huu kwa nchi hii viongozi wandamizi waliutaka.
 
Bila kuona haya nadhani katika hii issue Mwamwindi ndiye shujaa. Hakukubali ushenzi na uonevu usiokuwa na maana, hivyo alikuwa tayari kufa kuliko kuona uchafu huo.

Tanzania ya sasa inahitaji watu kama Mwamwindi ambao watasimama na kupigania haki zao na nchi yao. Tungekuwa na akina Mwamwindi wengi hapa Tanzania basi hata pesa za EPA zingerudi.
 
Netanyau, ulichozungumza kimenigusa sana maana umegusa kitu ambacho nimekuwa nacho hadi hapa nilipo. Sera ile ilikuwa ni mbaya sana sisi tuliishi karibu na Kambi ya Jeshi Mafinga JKT, nakumbuka sana wanajeshi walikuwa wanakuja kumsumua baba maana naye mwanzoni alikataa kujiunga na Kijiji cha Ujamaa. Baada ya hap serikali ikaamua kutumia wanajeshi kutuhamisha kwa nguvu ikawa hivyo. Mali kibao ziliharibika kwa jua na mvua nyumba zilichomwa moto tukiwa watoto tuliingiwa na woga sana kuona hali ile Baba ambaye alikuwa ndiye tunaona ni mwenye nguvu hakufanya kitu mbele ya wanajeshi wa JKT. Alisukumwa huku na huku akitakiwa kuhama mara moja ifikapo jioni ile. Sisi kwa utoto wetu tukadhani ni vita maana wanajeshi na bunduki zao kwa raia asiye na hata mkuki. Tulikuwa tukilima mazao mbali mbali hata siku moja hatuwahi kuwaza kitu kiitwacho njaa lakini leo hii nchi imejibu. Baba alikuwa anamiliki mashamba makubwa huko Isimani kilomita kama 150 - 200 toka Mafinga nako mambo yakawa hayo hayo ya vijiji vya ujamaa. Umasikini tulijitakia. Tulikuwa na Irrigation scheme nzuri sana ambapo hata wakati wa kiangazi mazao yalikuwa yakilimwa lakini si leo. Umasikini huu kwa nchi hii viongozi wandamizi waliutaka.

Asante kwa kutupa hali halisi.Pole sana.
 
Kwa maneno yake Mwalimu alisaini kunyongwa kwa mwananchi mmoja tu, Mwamwindi na siku zote alikuua akitembea na Biblia akimuomba Mungu amsamehe, maana yake inaweza kua moja tu kuwa hivyo vifo vingine 9 katika awamu yake vilisainiwa na wengine, kwa maelekezo yake or else!
Masahihisho ni kitu kizuri sana, ila yafanyike pale kwenye makosa tu!

Hapana Mkuu hicho kitu hakiwezekani. Mtu asaini death warrant on behalf of some body else? No way. Kuna kesi ambayo KAWAWA ALISAINI DEPORTATION ORDER kwa niaba ya Mwalimu kusudi Jamaa ahamishwe (it wa normal kipindi cha mzee ukipingana naye kupelekwa mafia au kwingineko for the rest of your life). Mahakama ilikataa kwamba hiyo order haikuwa valid kwa sababu kuna vitu huwezi kuvi-delagate. Hiyo kesi ukiihitaji naweza itafuta, ila naamini wanasheria wanaijua hiyo kesi maana ni famous sana kwenye administrative law.

Kuhusu number ya waliokufa kipindi cha mwalimu sina takwimu (ila namuamini Kuhani maana ameleta source) Kama watu walinyongwa ilikuwa ni kwa ORDER YA MWALIMU period. Hii ya apologetics wake kutaka tuamini kwamba Mwalimu alinyonga mtu mmoja tuu nadhani siyo sahihi kabisa. Kwani watu wakinyongwa wananchi tunataarifiwa? si mpaka ukutane na hizo kesi kwenye vitabu vya sheria au ukutane na aliyepoteza ndugu? I think so far Kuhani is the best sources kwamba Nyerere alinyonga watu Kumi.

After all kama Nyerere alikuwa anatembea na bible..kwa nini hakuifutilia mbali adhabu ya kifo? kama kweli alikuwa anaamini "sanctity of human life?"

Anyway tuendelee na mjadala.
 
Alhaj Mwamwindi aliua Desemba/1971 na mapema June/1972 kesi ilikuwa imekwishamalizika...Ni vipi kesi hii ya mauaji iliyohitaji uchunguzi wa muda mrefu iliendeshwa kihara haraka namna hiyo?Ni kweli kwamba Mwalimu alitia saini adhabu ya kifo kwa sababu tu kifo kilimuhusu rafiki yake?Mbona alikawia na hatimaye kumuacha huru Mama Liundi ambaye aliuawa watoto wake wawili kwa kuwatilia sumu kwenye chakula?(wakati hukumu ya mahakama ilikuwa ni adhabu ya kifo?)..

Cheki rekodi zako mzee,huyu mama ni kweli aliua watoto wake wakati Mwalimu akiwa rais lakini aliyemwachia huru alikuwa ni Mwinyi...na alisema kuwa huyu mama kishapata adhabu ya kutosha.
 
Masanja said:
Hapana Mkuu hicho kitu hakiwezekani. Mtu asaini death warrant on behalf of some body else? No way.

Masanja,

..unajua kuna watu wanafikiri kutoa visingizio vya ajabu-ajabu kama hivyo hapo juu wanamtetea, kumlinda, na kumuenzi, Baba wa Taifa.

..ku-suggest kwamba Mwalimu Nyerere alikasimisha mamlaka yake ya kusaini death-warrants kwa watu wengine ni kumtukana matusi makubwa kabisa.


Mwikimbi said:
wakati dr kleruu akiwahamisha wahehe toka vijiji vyao vya asili kwake kule marangu mambo yalikuwa tofauti, bado alikuwa anamiliki kihamba chake, na hakuhamia kwenye vijiji vya ujamaa. ni ule msemo maarufu kuwa WANASIASA HUWA WAANAHUBIRI UBORA WA KUNYWA MAJI KWA WAFUASI WAO, WAKATI WAO WANAKUNYWA DIVAI

Mwikimbi,

..Peter Kisumo, akiwa mkuu wa mkoa, ndiye aliyemshawishi Mwalimu kutokupeleka operesheni vijiji Kilimanjaro.

..kuna sababu nyingi tu zikiwemo za kihistoria, kisiasa, kijiografia, na hata kiuchumi, kwamba zoezi hilo lingeleta madhara makubwa, na lilikuwa halitekelezeki, katika maeneo mengi ya Kilimanjaro.

..Kithuku ameleta maelezo ya kina kuhusu maeneo ambayo vijiji vya ujamaa vilianzishwa Kilimanjaro. lakini utaona kwamba zoezi hilo lilitekelezwa ktk maeneo ambayo kiasili yamekuwa hayakaliwi na makabila makubwa ya Kilimanjaro--Wachaga na Wapare.
 
Back
Top Bottom