Pre GE2025 Dkt. Willibrod Slaa aachiwa huru, DPP hana nia ya kuendelea na kesi

Pre GE2025 Dkt. Willibrod Slaa aachiwa huru, DPP hana nia ya kuendelea na kesi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
You can say that again

But slaa alizusha bahati mbaya aligusa live wire

Sasa hivi atatulia
Ukweli ni upi? Na kiza Bisgye wa UGANDA Je kagisa waya upi? Mbowe aliitwa GAIDI na baadae kufutiwa mashitaka kwa kugusa waya up? Mzee kibao naye aligusa waya???
Tuache uchawa
 
Ukweli ni upi? Na kiza Bisgye wa UGANDA Je kagisa waya upi? Mbowe aliitwa GAIDI na baadae kufutiwa mashitaka kwa kugusa waya up? Mzee kibao naye aligusa waya???
Tuache uchawa
Usilinganishe mbowe au kiza na kitu cha ajabu
 
Wakati wa kutungwa kwa KATIBA MPYA ILIYO BORA, tuangazie kazi na mamlaka ya huyu DPP..naona ni kama yanatumika vibaya
 
Slaa kaachiwa sababu za kufuta kesi hatujui.
Wamemfix,akileta nyodo tena wanampelelekea moto wa volcano.
Aachane na siasa.
 
Dpp hana nia ya kuendelea na kesi hii haina tofauti na wale jamaa waliokaa Germany kuigawa Afrika na kuitawala.
 
Dr.Slaa moto ni ule ule🔥
Dk. Slaa ana moto gani wa kutisha mtu? Kama ana moto mbona kipindi cha Jiwe aliufyata? Akakubali hadi kumtumikia Jiwe kwa namna alivyotaka Jiwe?

Ushauri wangu kwa Rais Samia na Serikali yake, huyu Mzee ashughulikiwe kwa namna yoyote inavyofaa pale atakapojifanya mjuaji na kutoiheshimu Serikali iliyopo madarakani. Hata ikibidi kufia jela sawa tu!
 
Walidhani kwa kumuweka Dr. Slaa korokoroni wangemsaidia mtu wao ashinde uenyekiti wa Chadema!! Wameambulia patupu😳🤪

Nanye Go, Allen Kilewella, Tlaatlaah, Erythrocyte, imhotep, na Ile timu kamili:

Gknr00nXQAA56h7.jpeg


Mnakwitwa huku!
 
Sasa alishikwa kwanini kama hana kesi!! Yaani mpaka mahakama ni machawa
Hujaambiwa hana kesi, kesi ipo ila hakuna haja ya kuendelea nayo kwa sasa, itappfika muda hata kesho watesi wake wakitaka kuendelea nayo anarudi rumande. Ila sasa hawapo na mahakama imeona impe tu muda akaendelee na shughuli yake.
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam imemuachilia huru Dkt. Wilbord Slaa baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini DPP kueleza kuwa hana nia ya kuendelea na shauri hilo.

Shauri Na.993 la mwaka 2025 lilidai Dkt. Slaa ameshtakiwa kwa kuchapisha taarifa za uongo kupitia ukurasa wa X (zamani Twitter).

Leo February 27,2025, Wakili wa Serikali Mwandamizi Job Mrema amewasilisha nia ya DPP mbele ya Hakimu Mfawidhi Franco Kiswaga .

Wakili Mrema ameieleza Mahakama kuwa DPP ameamua kutoaendelea na shauri hilo kwa mujibu wa kifungu cha 91 (1) cha mwenendo wa makosa ya jinai.


Source: Millard Ayo, TBC
Hii nchi inahitaji mabadiliko makubwa yaani serikali inaamua kumuweka mtu ndani kwa miezi miwili bila kosa halafu inakuachia bila fidia yoyote. Hii sio sawa . Watanzania bado hatujapata uhuru. Tunacho ambiwa ni uhuru sio uhuru ni hiari ya kutawaliwa kikolone na watu weusi wezetu.
 
Back
Top Bottom