Dkt. Yahaya Nawanda apandishwa Kizimbani kwa Tuhuma za Ulawiti, aachiwa kwa dhamana

Dkt. Yahaya Nawanda apandishwa Kizimbani kwa Tuhuma za Ulawiti, aachiwa kwa dhamana

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Ameburuzwa kwenye Mahakama ya Mkoa wa Mwanza akikabiliwa na kosa moja la Ulawiti

Amepandishwa leo July 9 baada ya makelele mengi ya wadau kutaka haki itendeke

Bado haijajulikana kama ataswekwa Rumande au atapata dhamana.

====

Aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Yahaya Nawanda, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Mwanza na kusomewa shitaka moja la kumwingilia kinyume na maumbile Tumsiime Ngemela (21) katika eneo la Rock City Mall jijini Mwanza.

Mshtakiwa huyo amefikishwa katika mahakama hiyo mapema leo Julai 9, 2024 na kusomewa shitaka hilo ambalo anadaiwa kulitenda Juni 2, 2024 katika eneo hilo kinyume na kifungu cha sheria cha 154 kifungu kidogo (a) cha kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2022

Mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza, Erick Maley, Waendesha mashtaka wa kesi hiyo ambao ni Wakili wa serikali Magreth Mwaseba na Martha Mtiti waliitaja kesi hiyo kuwa ni kesi namba 1883 ya mwaka 2024.

Hatahivyo mshtakiwa alikana shtaka hilo na yuko nje ya dhamana baada ya kukamilisha masharti aliyokuwa amewekewa ambayo ni kuwa mtumishi wa serikali pamoja na bondi ya mali isiyohamishika yenye thamani ya Sh 5 milioni.

Baada ya kukamilisha masharti hayo, Mshtakiwa yupo nje ya dhamana hadi Julai 16, 2024 ambapo kesi hiyo itaanza kusikilizwa kwa hoja za awali huku upande wa mlalamikaji ukitakiwa kwenda na mashahidi.

Pia soma
 
Ameburuzwa kwenye Mahakama ya Mkoa wa Mwanza akikabiliwa na kosa moja la Ulawiti
Wacha haki itendeke. Swali langu, Je, ikithibitika ni kweli Nawanda alimlawiti yule binti, zile pesa milioni 10 alizopewa binti atazirudisha au zitakuwa zake au??

Wanasheria mtusaidie hapa. Maana binti aliulizwa ulipewa kiasi gani na Nawanda. Akajibu, alipewa milioni 10 cash. Anazo na hajazitumia hata shilingi.
 
Wacha haki itendeke. Swali langu, Je, ikithibitika ni kweli Nawanda alimlawiti yule binti, zile pesa milioni 10 alizopewa binti atazirudisha au zitakuwa zake au??

Wanasheria mtusaidie hapa. Maana binti aliulizwa ulipewa kiasi gani na Nawanda. Akajibu, alipewa milioni 10 cash. Anazo na hajazitumia hata shilingi.
Hio si ni hongo ya kumziba mdomo muhanga, na kama hazijadaiwa ni haki ya binti
 
Wacha haki itendeke. Swali langu, Je, ikithibitika ni kweli Nawanda alimlawiti yule binti, zile pesa milioni 10 alizopewa binti atazirudisha au zitakuwa zake au??

Wanasheria mtusaidie hapa. Maana binti aliulizwa ulipewa kiasi gani na Nawanda. Akajibu, alipewa milioni 10 cash. Anazo na hajazitumia hata shilingi.
Wanasheria watatusaidia hapa
 
Ameburuzwa kwenye Mahakama ya Mkoa wa Mwanza akikabiliwa na kosa moja la Ulawiti

Amepandishwa leo July 9 baada ya makelele mengi ya wadau kutaka haki itendeke

Bado haijajulikana kama ataswekwa Rumande au atapata dhamana.
ATAPATA DHAMANNA AS LONG AS IT IS BAILLABLE, WAMESHAPANGA KILA KITU NA HAKIMU KESHAPATA CHAKE (MOST PROBABLY, INGAWA NI VIGUMU KUWATAKA MLUNGULA)
 
Wacha haki itendeke. Swali langu, Je, ikithibitika ni kweli Nawanda alimlawiti yule binti, zile pesa milioni 10 alizopewa binti atazirudisha au zitakuwa zake au??

Wanasheria mtusaidie hapa. Maana binti aliulizwa ulipewa kiasi gani na Nawanda. Akajibu, alipewa milioni 10 cash. Anazo na hajazitumia hata shilingi.
Atumie kushonea marinda mkuu hiyo kitu sio mchezo
 
Back
Top Bottom