Doctor yeyote humu naomba ushauri katika hili...

Sir_Mimi

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2013
Posts
7,171
Reaction score
15,760
Lisaa limoja lililopita hapa karibu na ofisi yangu kuna kijana alikuwa anakimbizwa akituhumiwa kwamba ni mwizi na raia wakaanza kumshambulia sasa akiwa amezungukwa na raia mimi nikaingia katikati yao kumuokoa.

Katika kusukumizana sukumizana nikaangushwa chini kwenye lami kisha nikamdhibiti kijana asiendelee kupigwa,baada ya kuwa watu wameshapoa kwa hasira nikamuacha kwenye mikono salama ila nikajikuta nimebaki na damu kwenye kiganja cha mkono wangu ambao nao umepata michubuko kwenye vidole viwili kwa juu,nimenawa maji na sabuni ila naomba ushauri wenu siwezi kupata madhara yoyote in case jamaa akawa ana tatizo?nawasilisha
 
Wewe ni mvulana wa mkoani? huku Dar kila mtu ana mind business zake, siku nyingine utakuja kufa, acha kiherehere na kuwashwa washwa.
Asante sana chief kwa ushauri wako!nayo pia ni maoni yako sikulaumu!
 
ha hahah ha,acha uwoga jamaa..upo salama,pia hongera kwa kuokoa maisha ya huyo kijana!
Nipo salama vipi kaka hali nimeshika damu ya mtu nisiyemjua?japo sina uhakika sana kama damu ilifika live kwenye michubuko wasiwasi wangu ni je niliponawa maji haiwezi kuingia kupitia kwenye maji.
 
mwizi anapigwa nawatu wengi ???? Weee mmoja ndo ukaingia kumsaidia ???? Akati huna uhakika kama kaiba ?? Wat if km kweli nimwizi kaiba ??? .

Sitaki kuamin kama ujasiri mkubwa ulonao wakumuokoa jamaa mikonon mwa makumi yawatu ,huo ujasiri umekupotea.

Dahhhhhh hapo bado sijaielewa vizuri.

Anyway ....Kama nikweli wasiwasi wako nisababu ya kumuokoa jamaaa Basi Umzm Wa afya .

Ila km umetumia maelezo mengine kuelezea wasiwasi mwingine ,,Basi nivema kutuliaa kisha baadae ukachukie vipimo... Kugasana nadamu yamtu nihatar sana.
 
Asante chief,sina sababu ya kuelezea tofauti ili kupata faraja kutoka kwenu.kweli ni mwizi na sikumuokoa peke yangu japo mimi ndiye nilienza ndo nikapata kampan kutoka kwa jamaa wengine watatu tukamuokoa.
 
Nenda kituo cha afya cha karibu upimwe alau Hiv kama huna upewe dawa kinga mara moja na kama unaweza kwenda naye hospitali naye apimwe kama hana maambukizi haina haja ya dawa
 

Katika Kiswahili sanifu kabisa hakuna neno ' Lisaa ' bali kuna neno Saa tu. Tuanzie hapo Kwanza!
 
Hongera sana komando kipensi, nenda upate tiba huyo kijana atakuwa ni salama wezi huwa hawapati magonjwa kama HIV
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…