Dodoma: Achomwa moto kwa tuhuma za mauaji

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Athuman Malesa (22) mkazi wa Kijiji cha Kaloleni wilayani Chemba mkoani Dodoma, ameuawa na watu wenye hasira kali kwa kuchomwa moto, akituhumiwa kwa mauaji na kufanya vitendo vya ukatili ikiwemo ubakaji na kulawiti watoto.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Olboloti wilayani Chemba Shabani Maslahi Maslahi amethibitisha kifo hicho.

Amesema hatua hiyo imetokana na kundi la vijana maarufu 'Maronjoo' ambao huishi na mifugo porini kufanya vitendo vya uhalifu na kuua.

Marehemu akiwa na wenzake walisakwa na wananchi wenye hasira kali kisha kuuawa ofisi ya kijiji cha Olboloti huku wengine wakishikiliwa na Jeshi la Polisi

Wanaoshikiliwa na Polisi ni Sefu Malekela (23), na Alhaji Hamad (21) wote wakazi wa Kijiji cha Kaloleni.
 
Ukiona wananchi wanakimbilia njia hii ya kujichukulia sheria mikononi, maana yake serikali na vyombo vyake vya ulinzi havitimizi majukumu yake ipasavyo kwenye maeneo husika.
 
Wananchi wenye hasira kali hawajawahi kuonyesha hasira zao kwa watembelea GXR
 
Imekaa vizuri kama shutuma ni za kweli...justice served quick ni Good Justice ⚖️ 🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…