Dodoma City vs Arusha City (The Battle of Tanzania Capital City vs EAC Capital City)

Hiv unaelewa ulichokiandika au magazeti tu .. kasome upya uje uandike before sijakuaibisha
Umwaibishe nani wewe kenge, umekariri GDP shuleni unataka kufanya watu majuha humu. Seychelles wana high GDP kwa hiyo hata Equatorial Guinea wana high GDP lakini watu maskini sana. Ndio nyinyi Mwanza huko. Kajifunze kwanza namna wanavyo calculate GDP. China wana GDP mara tatu ya nchi kama Japan na German lakini umeshawahi kuona Mjapan machinga Kariakoo? nenda kasome..
 
Hiv unaelewa ulichokiandika au magazeti tu .. kasome upya uje uandike before sijakuaibisha
Labda wasukuma standard ya maisha yenu iko wakati ukweli unajulikana maskini wengi sana sasa sijui hiyo GDP yako imechangia nini katika maisha ya wana Mwanza. Nyinyi na wahaya ndio mko kila sehemu sababu ya ugumu wa kazi Mwanza. GDP nyokooo
 
Labda wasukuma standard ya maisha yenu iko wakati ukweli unajulikana maskini wengi sana sasa sijui hiyo GDP yako imechangia nini katika maisha ya wana Mwanza. Nyinyi na wahaya ndio mko kila sehemu sababu ya ugumu wa kazi Mwanza. GDP nyokooo
Mbona umepaniki broo?! Kwo asiseme ukweli...sasa hata kwa hali ya kawaida kati ya dodoma na Mwanza watu wake ni wapi wanaongoza kuwa omba omba Tanzania?
 
Mkuu kuna International flight gani na kwa abiria wa wapi iwe na route kutoka ulaya kwenda Dodoma?..embassies zote zaidi ya mia mbili zilipewa plots bure kujenga ofisi za balozi zao zaidi ya miaka mitano iliyopita huko dom je kuna hata moja imeanza hata kujenga msingi?..dodoma itachukua miaka mingi sana kufikia levels za hiyo miji mingine ya dsm, arusha, mwanza kwa maendeleo jumuishi..tuache siasa kwenye mambo serious
 
Mkuu unajisumbua tu kubishana na hao haters wa jiji la Dodoma wengine hawajawahi hata kufika au wengine walikatisha tu barabarani wakati wanasafiri kwenda mikoani ndiomana wanakubishia kishabiki.Kwa sisi ambao tumewahi kuishi na kufanya kazi Dodoma Jiji tunajua ukweli kwamba kwa sasa Tanzania hii hakuna Jiji linalokaribia Dodoma kwenye vigezo vya ubora wa mipango miji,ubora wa miundombinu,uwekezaji mkubwa wa serikali na private,ukuaji wa mji.Hizo ni facts ndiomana unaona jamaa wanaokoteza okoteza tu porojo za mtaani😀😀😀
 
Wewe ndio unachekesha kabisa ...ngoja nikusaidie kukupa facts👇👇
-Mradi wa Msalato International Airport bado haujakamilika..uwanja wa ndege unaotumika ni ule wa zamani katikati ya Jiji
-Ubalozi mdogo wa Ujerumani tayari ushahamia Dodoma
-Mashirika mengi ya kimataifa tayari yashaweka ofisi zao Dodoma kwamfano WFP,FAO,SAVE THE CHILDREN,WHO,EGPAF n.k
Ikumbukwe mchakato wa kuhamia Dodoma ni process sio suala la sikumoja .
Kwa kulinganisha vigezo vya ubora wa mipangomiji,miundombinu,huduma za kijamii,uwekezaji wa serikali,ukuaji wa mji basi Dodoma inashika nafasi ya pili baada ya Dar huo ndio ukweli.Kitu pekee inachozidiwa Dom na Mwanza ni population(hilo halina ubishi) na inachozidiwa na Arusha ni uwekezaji kwenye sekta ya utalii
 
Soma title ya thread tunalinganisha majiji ya Dodoma na Arusha sio mkoa wa Dodoma na Arusha...👇👇

 
Yale yale ya Songwe International Airport zinaishia kutua Precision na Air Tanzania
 
..mkuu mm siongei siasa...unasema ubalozi mdogo wa Germany umehamia dom..umehamia wapi?kwenye plot yao waliyopewa zaidi ya miaka saba iliyopita?.kuna embassy gani zinazoshindwa kujenga jengo lao kwa zaidi ya miaka saba?.nchi zote za nje zina plots dom zaidi ya 7yrs but hakuna aliyeweka hata msingi na tatizo sio pesa.!.dom imeanza kupewa pesa na Gov toka enzi za CDA but mji umeshindwa kukua!

..huo mtaa wenye mashirika mengi ya kimataifa hapo dom ni upi?tutajie ili tukahakiki hizo office zao!..ukitaka kujua mji unakua kwa kasi na kuwa kimataifa kama unavyosema angalia hata bei za plots kwenye mji husika..hapo dom tena mjini viwanja vingi unapata kwa bei ya chini ya 10m tena survyed plot..wakati hiyo miji mingine ya arusha, mwanza,dsm huwezi kupata kiwanja chenye hati katikati ya mji kwa hiyo bei na bado hiyo miji inakua...ni ukweli kuwa ukuaji wa dom ni mdogo sana kulinganisha na pesa zilizokuwa invested hapo..hizo pesa zingekuwa invested miji mingine kama arusha, mwanza, dsm basi tungekuwa na Johannesburg au hata nairobi ndani ya Tz.
 
100%
 
I totally agree
 
Mkuu unajitahidi kubadili badili topics kuhamisha magoli baada ya kupewa facts tupu.Soma title ya thread inahusu DomCity vs ArushaCity sio Dom vs Nairobi au Dom vs Johannesburg.
Suala la ujenzi wa balozi ni mchakato na kuna vitu vingi wanaangalia sio suala la sikumoja ....leo hii nchini Israel ni ubalozi mmoja tu wa Marekani uliohamia Jerusalem balozi zingine zote bado zipo Tel Aviv.
Narudia tena Dom City kwa sasa is far away kulinganisha na Arusha au Mwanza kwenye ukuaji wa majiji ...ukibisha basi unabisha kwa hisia na kiushabiki .
Majiji mengine yote ya Tanzania ukitoa Dodoma yanakabiliwa na changamoto zilezile zinazofanana kwamfano ubovu wa mipangomiji(Dodoma jiji imepimwa eneo lote zaidi ya asilimia 90),ubovu wa miundombinu(Dodoma inaongoza kwa mtandao mpana wa barabara za lami ndani ya CBD),uwekezaji mdogo wa serikali(Dodoma wanapendelewa sana hilo halina ubishi).
Sijaona changamoto yoyote ambayo iko valid kuhusu ukuaji wa Dom City zaidi ya porojo
 
Hili swala la Dodoma kupangiliwa ni la miaka nenda rudi lakini hii bado haijawah fanya Dodoma kuizidi Arusha au Mwanza labda kwa title ya kupangwa tu ila kimaendeleo vipi
 
Mkuu maeneno gani nitapata kiwanja ya town dom chini ya mil 10 nisaidie tafadhari
 
Mkuu maeneno gani nitapata kiwanja ya town dom chini ya mil 10 nisaidie tafadhari

..mkuu vimejaa tele ingia hii link hapa chini utakuta bei ndogo sana na vina hati..hiki hapa kwenye link ni 5m ila ukiongea vizuri hata 3m utauziwa!

 
Hili swala la Dodoma kupangiliwa ni la miaka nenda rudi lakini hii bado haijawah fanya Dodoma kuizidi Arusha au Mwanza labda kwa title ya kupangwa tu ila kimaendeleo vipi
kupangiliwa vizuri mipangomiji jiji la Dodoma hiyo ndio top advantage iliyo nayo Dom kulinganisha na miji mengine nikupe mifano miwili tu👇👇
-Kutokana na ubora wa mipangomiji na miundombinu ya jiji la Dodoma ...Dodoma ndio jiji pekee Tanzania ambalo ikitokea ajali ya moto magari ya zimamoto yanafika chap kwa haraka na kwenye exact location.Nakumbuka kipindi fulani ilitokea ajali ya nyumba kuwaka moto maeneo ya Area A yaani ilichukua dakika chache sana gari ya zimamoto kutoka Zimamoto Makao Makuu kule Makole pamoja na gari la zimamoto kutoka Airport kufika na kuzima moto kwa haraka.Ingekuwa vichochoro kama vya miji mingine yenye makazi uchwara na mipangomiji ya hovyo hali ingekua mbaya sana
-Mfano wa pili ni kuhusu usalama wa raia.Kutokana na Dodoma kupangiliwa vizuri mipango miji na miundombinu ni nadra sana kusikia matukio ya ujambazi ndani ya jiji la Dodoma.Kwa namna mji ulivyopangwa ni ngumu sana majambazi kukimbia nje ya mji tofauti ni miji mingine mfano Dar ambapo majambazi wanaiba benki na bado wanafanikiwa kutoroka kupitia vichochoro vya uswahilini.Sikumbuki mara ya mwisho lini nimesikia tukio la ujambazi au wizi mkubwa ndani ya Dom City
 

mkuu dom ilikuwa designated kama mji mkuu wa Tz toka mwaka 1974 na hakuna any conflict since then..kulinganisha Jerusalem mji wenye conflict kati ya Israel&Palestina na Dodoma ambayo haijawahi kuwa na conflict ni kutofahamu mambo ya kuwa capital city...mchakato wa Dodoma kuwa mji mkuu ulianza hiyo 1974 na hadi leo miaka zaidi ya 49 hakuna embassy iliyojenga dom!..Abuja ilikuwa designated kama capital ya Nigeria 1991 na embassy zote zilishahamia Abuja kutoka Lagos...je utahitaji mchakato wa miaka mingapi dom kuwa na embassy?miaka mia moja?

..ukuaji upi huo wa dom wenye kushinda arusha, mwanza, dsm?.dom imeanza kuwa capital toka 1974 na pesa nyingi kuwekwa na Gov ila imeshindwa kukua...mfano wa Johannesburg na nairobi nimeutoa kwa maana ya kama pesa zilizowekezwa dom miaka yote na Gov zingewekezwa hiyo miji mingine basi tungekuwa tumefika levels za Johannesburg na nairobi
 
Huko ambako sio planned mara ya mwisho umesikia lini [emoji53]
 
mkuu sasa kuna vitu gani vya kuiba dom?.suala la uhalifu halihusiani na mpangilio wa mji...majiji makubwa yaliyopangiliwa kama new York, London, etc kuna uhalifu sababu kuna vitu vyenye thamani vya kuiba..sasa kama mji hauna ukuaji vibaka wataenda kufanya nini?..

..pia ujue hata mji wa dsm ulipangwa vizuri na mkoloni ni vile tu kuna fursa na ukuaji wa haraka ndio leo unauona hauna mpangilio..the same inaweza kuja kutokea kwa dom ukisha-grow na kuwa na fursa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…