Dodoma City vs Arusha City (The Battle of Tanzania Capital City vs EAC Capital City)

Dodoma itabaki kuwa kama ilivyo Washington USA hata namba 5 haiwezi kuwepo ngoja wamalize kuuza viwanja
Washington Kuna viwanda? Washington ni ya tatu Kwa Ukubwa? Hapa ndipo mnapojifariji.Dom inajengwa tofauti na hiyo Miji mingine Kuna industrial areas
 
Dodoma after the majengo ya serikali are completed will be back to its normal state of dormantism

Nisamehewe kwa lugha
Ndio kwanza ita Take off, uwekezaji unaofanywa Dom sio majengo tuu Hadi miundombinu
 
Arusha haina mpinzani bongo ukitoa Dar! Mwanza yenyewe labda kwa population lakini kama Arusha jiji ikiongezewa manispaa chache tutaongea mengine.

Kwanza Arumeru iwe manispaa na ina sifa.
 
Arusha haina mpinzani bongo ukitoa Dar! Mwanza yenyewe labda kwa population lakini kama Arusha jiji ikiongezewa manispaa chache tutaongea mengine.

Kwanza Arumeru iwe manispaa na ina sifa.
haina mpinzani kwa vigezo vipi mkuu ....Dom washaikalisha Arusha kitambo.Kigezo pekee Arusha inachozidi Dom ni sekta ya utalii na mahoteli basi... lakini vigezo vingine kama ubora wa miundombinu,ubora wa mipangomiji, ubora wa huduma za kijamii,uwekezaji mkubwa wa serikali n.k Arusha haifiki hata robo kwa Dom City huo ndio ukweli
 
Dodoma wanapendelewa sana yaani👇
-National Hospital MIREMBE
-Zonal Referral Hospital B.W. MKAPA
-National Military Hospital
-Regional Referral Hospital
-na kuna ile nyingine Uhuru Hospital ipo Chamwino
Uhuru ni hospital ndogo,Kuna Hospital ya mama na mtoto yenye hadhi ya Kitaifa inajengwa.
 
Nasimama na Arusha.. dodoma bado Ina safari ndefu kuipata Arusha ndo ipambane na mwanza.....hata hyo population inayotajwa dodoma imehusisha Hadi vijiji vya hombolo huko na chipogolo ...proper city population ya dodoma not more than 450k ...
Dodoma inaipita arusha kwa sasa
 
Mi ni wa kanda ya kaskazini ila nisiwe mwongo ranking ipo hivi???
1. Dar es salaam.
2.Dodoma.
3.Arusha na Mwanza ziko sawa tu zimepishana padogo
4. Miaka 10 plus Dodoma inaweza kaa sawa na Dar....
Kinachoibeba Dar ni bandari na viwanda vingi...
 
Mi ni wa kanda ya kaskazini ila nisiwe mwongo ranking ipo hivi???
1. Dar es salaam.
2.Dodoma.
3.Arusha na Mwanza ziko sawa tu zimepishana padogo
4. Miaka 10 plus Dodoma inaweza kaa sawa na Dar....
Kinachoibeba Dar ni bandari na viwanda vingi...
Exactly.....tatizo wengi humu wanachangia kiushabiki sio kiuhalisia.
 
Mi ni wa kanda ya kaskazini ila nisiwe mwongo ranking ipo hivi???
1. Dar es salaam.
2.Dodoma.
3.Arusha na Mwanza ziko sawa tu zimepishana padogo
4. Miaka 10 plus Dodoma inaweza kaa sawa na Dar....
Kinachoibeba Dar ni bandari na viwanda vingi...
Dodoma ni mji wa Serikali na Serikali imeshahamishia Wizara na Idara zake 90% na Ofisi zinaelekea kukamilka kwa 90% hivyo speed ya ujenzi wa Ofisi za Kiserikali uko 90% hakutakuwa na miradi mingi iliyobaki ya Serikali.
Kama utafuatilia mapato ya Jiji la Dodoma kipindi Serikali inahamia yalifika hadi Bilioni 70 na kuzipita Halmashauri za Dar kwa sababu ya uuzaji wa viwanja, kwa sasa mapato yameshuka hadi Bilioni 30 kwa maana ya 50% na yataendelea kushuka kwa sababu niliyoonesha hapo juu.
Ushauri wangu kwa sasa Jiji waangalie njia mpya ya kuingiza mapato bila kutegemea ujio wa Serikali hapa Dodoma kama vile uwekezaji wa miradi mbalimbali kama Jiji la Dar,Arusha na Mwanza wanavyofanya.
Wananchi wa Dodoma watumie vyema fursa za Serikali kuwepo hapo kuwekeza maana naona speed ya Wafanyabiashara wa hapa Dodoma kuwekeza iko chini kulinganisha na majiji ya Dar,Mwanza na Arusha ambao yanajiendesha yenyewe bila kutegemea Serikali na ndio maana mapato yao yanapanda hayashuki.​
NAWASILISHA.
IN GOD WE TRUST
 
Endelea kujifariji 😂😂

View: https://youtube.com/watch?v=n_tLJ3MtVa0&si=8cDDyrz_oAQgYYct
 

View: https://twitter.com/mamanafanikisha/status/1698990293591187707?t=hqEcZeai0ToJ7KB9-laKMw&s=19
 
Mchakato wa kuhamia Dodoma ni endelevu kumbuka mambo ni dynamic ...hizo wizara nyingine mpya zinaanzishwa kulingana na mahitaji husika mfano waziri wa uwekezaji,juzijuzi uchukuzi na ujenzi zimetenganishwa kuwa wizara zinazojitegemea,bado kuna taasisi na idara za serikali zinaanzishwa kilasiku.Bado kuna taasisi nyingine za serikali zimepewa muda ziwe zimehamia Dom mfano NIMR n.k
 
Umeandika vizuri ila hapo kwenye kasoro/mapungufu tukurekebishe kidogo
-Ukisafiri barabara ya Iringa eneo la Jiji linaishia Mpunguzi na pale mbele kidogo Nkulabi...kuanzia Mlowa hadi njia yote ya Iringa ni maeneo ya wilaya za Chamwino na Mpwapwa
-Barabara ya ring road ikikamilika nadhani ndio itakua muarobaini wa foleni ya magari kwa barabara ya Dom-Moro
-Dom imezungukwa na mabwawa kama Dabalo,Hombolo,Farkwa,Bahi,Zuzu (kwa Pinda) n.k
-Ni kweli hamasa ya utalii Dodoma ipo chini sana lakini cha kushangaza Dodoma ni mojawapo ya mikoa yenye vivutio vingi vya utalii kwamfano pori la akiba swagaswaga,hifadhi ya misitu asili ya chenene,mapango na michoro kondoa irangi,chemchemi ya majimoto kondoa,hifadhi ya akiba mkungunero,hifadhi ya milima ya rubeho-mpwapwa,hifadhi ya Kolo-kondoa,mahandaki ya wapigania uhuru wa afrika kusini yaliyopo Kongwa,historia ya makabila asili ya Dodoma kama Wagogo,Wanguu,Warangi,Wasandawe,Waburunge,Wasagara,Wakaguru,Wanyambwa n.k
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…