Dodoma City vs Arusha City (The Battle of Tanzania Capital City vs EAC Capital City)

Ndio ulete dodoma imechangia nini ukiachana na mapato ya Halmashauri kwingine hoi taabani njaa na kula ubuyu
Unachekesha sana...Dodoma CC inashika nafasi ya pili both makusanyo ya Halmashauri na TRA

 
Mwanza ni ushago Kwa Dom,nyie tupisheni kabisaa
Dodoma inapendeza hongera. Wakati inaanzishwa CDA miaka ya 70 mwanzoni ilikuwa majengo ya ghorofa yasizidi ghorofa nne kwa kuwa kuna viashilia vya tetemeko pia na water table ipo juu.
Japan yenye matetemeko mengi duniani inajenga hata ghorofa 100 LAKINI chini yake kuna Spring na spring hizo ni aghali,je hayo majengo marefu yaliojengwa Idodomya yamezingatia hilo?
Na kama kuna uvumbuzi wa jambo hilo,kwa miji ya kisasa ulitakiwa nyumba zote zijengwe na serikali,harafu serikali iwauzie au iwapangishe watu ili kulinda ubora,viwango vya miundo mbinu.
Lakini kuruhusu vijumba substandard vioteshwe na kuchukua maeneo makubwa sio kitu sahihi.
 
Ni kweli zamani maghorofa marefu Dodoma yalikua hayajengwi kutokana na water table kuwa juu ..ila maendeleo ya sayansi+teknolojia ya ujenzi kwa sasa Dom yanajengwa marefu tu.
Na sifa mojawapo inayotofautisha Dom na miji mingine ni kuwa jamaa wa CDA/Jiji wako very strictly kwenye mipangomiji...yaani ukikosea kujenga hata kama ni ndani ya kiwanja chako hawachukui hata wiki kuja kuweka alama ya "X-BOMOA"(Udom waliwahi kufanya kosa hilo walijenga geti kubwa la chuo bila kuwashirikisha kwanza CDA/Jiji kilichotokea lilibomolewa lote..kwa sasa ndio wamejenga lingine baada ya kufuata utaratibu)Kabla hujajenga ramani zote za ujenzi wa nyumba huwa zinakaguliwa na kupitishwa kwanza.
Kwamfano maeneo ya nyuma ya gereza la Isanga kule mlimani kama unaelekea tanesco nyumba za makazi zinazotakiwa kujengwa ni maghorofa tu .
 
Mkuu inapendeza kuona majumba yenye mvuto,lakini mara nyingi wakandarasi ni kubana matumizi hasa majengo ya taasisi za umma.
Mwalimu Nyerere alizungumzia Dodoma ni ghorofa nne tu,na kama kuna technology imekuja nayo iwekwe wazi ili wananchi wafahamishwe,kwani kwenye basement ya ghorofa ndefu ndipo mitambo hiyo ipo,na huwa inafanyiwa repair or replacement. Nigefurahi kupewa jengo mmoja refu lenye nyenzo hiyo.asante sana .mkuu.
 
Una akili sawa sawa wewe? Unaleta data za miaka5 iliyopita kwanin?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…