Dodoma hapakaliki, Watu wa Jiji wanafunga biashara za Watu kisa Service Levy

Dodoma hapakaliki, Watu wa Jiji wanafunga biashara za Watu kisa Service Levy

Naona wameamua kudhibiti wafanya biashara wachache tu wawepo
Kama mnavyoambiwa msizaane na wazungu
Hapo kuna watu wakubwa nyuma ya biashara hizo
Wanataka muwaachie mji labda mkalime
Halafu wako na mgambo wao wamevaa kijani ndo wako wanafunga makufuli. Loh.

Sent from my Infinix X669 using JamiiForums mobile app
 
Mshika Kibubu Mkuu alishasema " kama hatuendani na wanavyotaka tuhamie Burundi"

Ni wakati sasa wakufunga biashara na kutimkia Burundi.
Yani wanaweza kufunga line nzima ya maduka. Barabara yote kushoto na kulia wanafunga maduka . Wakikukuta na mteja wanawatoa nje wewe mwenye duka na mteja wako. Alafu wanatia kufuli.

Sent from my Infinix X669 using JamiiForums mobile app
 
Serikali ya Tanzania inaongozwa na wasomi waliowekwa madarakani na wachawi, waganga pori na wasoma viganja ambao karibia wote ni TABULARASA.... Ukiona msomi anashiriki SHIRKI ujue alienda shule kama stages za ukuaji na siyo kuelimika

Kimsingi tunaishi kama mazombi ndani ya nchi huru inayopeperusha bendera yake kwa furaha huku wananchi WAKIHAHA
Hatarii mnooo

Sent from my Infinix X669 using JamiiForums mobile app
 
Wiki iliyopita ilikuwa hapa Mwanza wilaya ya Misungwi,wafanya biashara walifanya mgomo kwa siku nzima,hawakufungua biashara zao..Wakilalamikia service levy ni kubwa na hawajapewa elimu juu ya hiyo kitu✍
 
Back
Top Bottom