Dodoma: Hofu yawakumba Wajumbe!

Dodoma: Hofu yawakumba Wajumbe!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Kufuatia kinachoendelea hapa Bungeni Dodoma,Wajumbe mbalimbali wameingiwa na hofu kuu juu ya mambo fulanifulani. Wajumbe hao-hasa wenye mafungamano na CCM wameonesha hofu juu ya usalama wao na uanachama wao ndani ya chama hicho kwakuwa viongozi wa chama husika wameanza kutumia 'ubabe' kuwadhibiti Wajumbe hao. Wajumbe hao wanadai kuwa kwasasa hawako huru ingawa wana mtazamo tofauti juu ya kilicholikwamisha Bunge kwasasa: kura ya SIRI au DHAHIRI?

"Wewe acha tu.Wengine tunatamani tujiuzulu na kurudi majimboni mwetu. Hapa tunalazimishana kama wanafunzi wa Shule za Msingi. Hatutuko huru kabisa ingawa baadhi yetu hatuoni tatizo la kura ya siri. Ndiyo tuliyoizoea katika kupata uamuzi mkubwa hapa nchini. Lakini,nani atajitokeza kusema hivyo hadharani?" alisema Mjumbe mmoja machachari kutoka Nyanda za Juu

"Wengine walijaribu kuonesha tofauti ya kimtazamo kwenye Party Caucus na wakaishia kutishwa na meza kuu. Hali hapa ni tete. Sisi tunang'ang'ania DHAHIRI;wengine wote SIRI. Kimahesabu,bado hakuna mshindi. Mvutano huu waweza kuendelea kwa muda mrefu bila ya upande mmoja kujirekebisha.Na kimsingi,msimamo wetu kama CCM ni butu na batili.Watanzania wataendelea kutuvumilia kwa muda gani?" aliongeza Mjumbe huyo aliyewahi kupokea vitisho vya kichama kwa misimamo yake

Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Dodoma)
 
Hofu gani unalenga mbona mimi siioni hiyo hofu labda huko kwenu bavicha.
 
Wacha tuendelee kuvuna tulichopanda...!! CCM ni adui mkubwa wa Taifa hili, tuendelee kumuomba mungu atunusuru na janga CCM!!!:help:
 
Kwenye vikao vya chama wameongea kwa kujiachia hakuna aliyetishwa njoo namlingine mkuu.
 
VUTA-NKUVUTE Pole kaka.Ila mbona mnaanza kurithishna nchi mapema kabla hata pepo hamjaiachia?Mmeshindwa kusubiri mpaka 2015?Naomba unijibu kwa kilicho ndani ya moyo wako kama hii ni sahihi.
 
Last edited by a moderator:
Kwenye vikao vya chama wameongea kwa kujiachia hakuna aliyetishwa njoo namlingine mkuu.

Mbona wewe hautumii akili kujibu au kuchangia hoja,mambo yako ni ushabiki tu wa ki-pumba-vu kwa nini?Hivi kwa akili yako unafikiri watu nje ya Bunge hawaoni wala hawasikii?Huwezi kumlazimisha punda kula Pilau wakati chakula chake ni nyasi.Acha ushabiki usiokuwa na mantiki kwa mambo yaliyo wazi.
 
Pole kaka.Ila mbona mnaanza kurithishna nchi mapema kabla hata pepo hamjaiachia?Mmeshindwa kusubiri mpaka 2015?Naomba unijibu kwa kilicho ndani ya moyo wako kama hii ni sahihi.
Kuchaguliwa kwa watoto vigogo kugombea Majimboni ni kioo tosha cha chama kukosa demokrasia. Watoto hao wanachaguliwa kwa kuwaogopa wazazi wao na kuepuka kuwaudhi.Basi.Si jambo jema hata kidogo

Mzee Tupatupa

 
Chadema ni janga sugu la wazawa inapasa kuikataa kwa kukemea.

Unawashwa eeeeh? sasa chadema inahusiana vipi na post yangu? Povu la nini? Nyie kila kitu mnafikiria chadema tu? Mkeo akikunyima nyumbani pia ni chadema siyo? pvmb%fff!!!Au na wewe ni mmoja wao?
Wewe ni mmoja wapo wa wale wa buku saba?
 
Unawashwa eeeeh? sasa chadema inahusiana vipi na post yangu? Povu la nini? Nyie kila kitu mnafikiria chadema tu? Mkeo akikunyima nyumbani pia ni chadema siyo? pvmb%fff!!!Au na wewe ni mmoja wao?
Wewe ni mmoja wapo wa wale wa buku saba?

Safi sana kwa majibu yako kiongozi,nakuunga mkono,haya vitabu saba hayatumii akili,muda wote ni ushabiki wa kiseng-e tuuuu.
 
Kuna watu kwa maslahi yao wanataka kulifikisha Taifa hili katika hali ya malumbano pasipo sababu za msingi... maswala ya kuleta itikadi za chama katika swala nyeti kama hili ni dhambi kubwa sana na ninaamini wale wote wanaoleta maslahi binafsi bilakuzingatia kwamba mbele yao taifa linawaangalia na kuwategemea aelewe wazi kwamba Wa Tz wa leo wameamuka sio mambumbumbu tena.. kwamba wanajua kupambanua hiki na kile... na mwenyezi Mungu yupo pamoja nao watendao haki na kulitakia jema taifa hili... wote wanaoleta maslahi binafsi kwa nia mbaya Mungu pia atawashughulikia pasipo shaka...kwa haki na kwa misingi ya demokrasia kwa swala lililoko mbele ya watanzania leo ni KATIBA hivyo basi kuifanya katiba hii isiwe na manung'uniko ..wengi wa wa TZ wanataka kura ya SIRI ... kwani kuna ubaya gani kukubali hili?
 
inasikisha sana hivi CCM wanashindwa kuwa na akili, hekima na busara? wao wanachaguliwa wa siri leo wanataka wazi hili swala litawagawa ccm wenyewe na dhambi hii haitakwisha
 
Kufuatia kinachoendelea hapa Bungeni Dodoma,Wajumbe mbalimbali wameingiwa na hofu kuu juu ya mambo fulanifulani. Wajumbe hao-hasa wenye mafungamano na CCM wameonesha hofu juu ya usalama wao na uanachama wao ndani ya chama hicho kwakuwa viongozi wa chama husika wameanza kutumia 'ubabe' kuwadhibiti Wajumbe hao. Wajumbe hao wanadai kuwa kwasasa hawako huru ingawa wana mtazamo tofauti juu ya kilicholikwamisha Bunge kwasasa: kura ya SIRI au DHAHIRI?

"Wewe acha tu.Wengine tunatamani tujiuzulu na kurudi majimboni mwetu. Hapa tunalazimishana kama wanafunzi wa Shule za Msingi. Hatutuko huru kabisa ingawa baadhi yetu hatuoni tatizo la kura ya siri. Ndiyo tuliyoizoea katika kupata uamuzi mkubwa hapa nchini. Lakini,nani atajitokeza kusema hivyo hadharani?" alisema Mjumbe mmoja machachari kutoka Nyanda za Juu

"Wengine walijaribu kuonesha tofauti ya kimtazamo kwenye Party Caucus na wakaishia kutishwa na meza kuu. Hali hapa ni tete. Sisi tunang'ang'ania DHAHIRI;wengine wote SIRI. Kimahesabu,bado hakuna mshindi. Mvutano huu waweza kuendelea kwa muda mrefu bila ya upande mmoja kujirekebisha.Na kimsingi,msimamo wetu kama CCM ni butu na batili.Watanzania wataendelea kutuvumilia kwa muda gani?" aliongeza Mjumbe huyo aliyewahi kupokea vitisho vya kichama kwa misimamo yake

Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Dodoma)

tupe source
 
inasikisha sana hivi CCM wanashindwa kuwa na akili, hekima na busara? wao wanachaguliwa wa siri leo wanataka wazi hili swala litawagawa ccm wenyewe na dhambi hii haitakwisha

Fuatilia kote dunia inapofikia kupata majibu ya issues kura inayopigwa ni ya wazi lakini inapofikia kuchagua kujaza nafasi kura inayopigwa ni ya siri hivyo tusichanganye vitu hivyo viwili ambavyo ni tofauti sans
 
CCM kama wanataka kura ya siri Dodoma je wako tayari sasa katika kila uchaguzi watu wasimame nyuma ya wagombea waone kama watapona ? Maana majimboni huwa wanapata kura za nguvu kwa msaada wa Tume na polisi . Leo inakuwaje wanataka uwazi ambao hawauwezi ?
 
Eee Mungu wa mbingu na nchi naomba jicho lako liangalie Dodoma na Sikio lako lielekeze hapo kwenye Bunge la Katiba,tazama kuna watu wanataka kutuharibia kuandikwa katiba itakayo tufaa sisi Watanzania tuliopo sasa na vizazi vijavyo kwa maslahi yao wenyewe ,sasa ukamhukumu kila atakaye tenda uovu huu na hukumu hii ikadumu mpaka kizazi cha nne cha uzao wake,siku zao zikawe chache,upanga,ukiwa na uharibifu vikawaandame usiku na mchana.

Kwa vile wamejitukuza sana wanaona wao ndo kila kitu eeeh Bwana kumbuka ulichomtendea Mfalme Nebukadreza mpaka alipokiri aliye juu ndiye anaye miliki na kutawala,mkono wako ukaunyoshee juu yao na familia zao mpaka watakapo jua wao ni wanadamu tu tena ni mavumbi na wewe ubaki kuheshimiwa mbinguni na duniani tena mkono wako ulionyooshwa mwanadamu hawezi kuurudisha nyuma,na atakayetoa wazo lake katika kuharibu mchakato huu hapo bungeni ahesabiwa sawa na yule aigusaye mboni ya jicho lako eeh Bwana na kuwa amesimama kinyume ya kila neno lililo jema mabaya yasiondoke hemani mwake siku zote za maisha yake ya kuishi duniani.
 
Ccm ni mkwamishaji wa wazi wa suala la katiba! Na kikwete ni mvurugaji namba moja!
 
Back
Top Bottom