Dodoma: Kofia mbili kuchomoza mabadiliko CCM

Dodoma: Kofia mbili kuchomoza mabadiliko CCM

Nikuulize wewe kwenu ni wapi.

Mfano, Kilimanjaro, ofisi ya Mkoa ipo Moshi Mjini.

Wilaya ya Moshi, ofisi ipo Moshi Mjini, Arusha Road

Kata ya Kibosho Magharibi, ofisi ipo Mawaleni, Kibosho

Tawi la Manushi Sinde,ofisi ipo Manushi Sinde.

Balozi/Mjumbe kwake kuna bendera na hapo ndipo ilipo ofisi ya shina.

Upo?
VITUKO CCM:
Kata anayoishi Mwenyekiti wa ccm Mkoa wa Kilimanjaro haina Ofisi ya ccm ya Tawi Hata moja wala haina Ofisi ya ccm kata.

Pili kata anayotokea mbunge wa ccm jimbo la Moshi mjini kule Kilimanjaro Hakuna Ofisi ya ccm Kata.

Ni Lini uliwahi kusikia kuna sherehe ya uzinduzi wa Ofisi ya ccm kata?
 
VITUKO CCM:
Kata anayoishi Mwenyekiti wa ccm Mkoa wa Kilimanjaro haina Ofisi ya ccm ya Tawi Hata moja wala haina Ofisi ya ccm kata.

Pili kata anayotokea mbunge wa ccm jimbo la Moshi mjini kule Kilimanjaro Hakuna Ofisi ya ccm Kata.

Ni Lini uliwahi kusikia kuna sherehe ya uzinduzi wa Ofisi ya ccm kata?
Kilimanjaro watu hawataki kuiona CCM hata kwa macho tu achilia mbali ofisi
 
CCM chama tawala hakina uwezo wa kuandaa kabrasha lenye maelekezo muhimu ya kufanyiwa kazi na makatibu wake wa mikoa na kuwafikishia walitumie kupitia njia mbalimbali za mawasiliano? Wanataka waje ndani ya vikao ili wasikie kwa masikio yao.Daah!
 
CCM chama tawala hakina uwezo wa kuandaa kabrasha lenye maelekezo muhimu ya kufanyiwa kazi na makatibu wake wa mikoa na kuwafikishia walitumie kupitia njia mbalimbali za mawasiliano? Wanataka waje ndani ya vikao ili hasikie kwa masikio yao.Daah!
Hawawezi kusikia kwenye tv au kuona?
 
Wanataka kurudisha ajira 170 wamesahau mishahara kipindi hicho walikuwa wanachangisha kutoka kwa wahindi na waburushi. Wenye akili kubwa ambao waliiwezesha CCM kuwa na fedha za kujiendesha wenyewe waliona hizo ajira ni za kujidurufu. Umaarufu wa kutaka kujipendekeza kwa watu huwa tabia yake ni kukulipa kwa kitambo kidogo sana.
 
Kofia mbili tuseme kuanzia Mwenyekiti wa CCM Taifa asiwe pia Rais wa nchi siyo !! ama ?

Kama hivi ndivyo basi haya yatakuwa mabadiliko makubwa mno ndani ya chama chetu, sijui yamesukumwa na nini? yaani why now ?
Mkuu Fuso, wana maana kuwa mgombea Rais wa CCM itakapo tokea amechaguliwa kuwa RAIS wa Nchi basi ile siku anaapishwa tu apewe na cheo/nadaraka yake ya kuwa Mwenyekiti wa Chama cha CCM, maana kwa utaratibu wa sasa, Rais anayemaliza muda wake huwa amebakiza miaka 2 ya uwenyekiti wake na hivyo kulazimika kujiuzuru mwaka mmoja kabla na kumkabidhi kofia hiyo Rais Mteule awe na kofia mbili akisubili kukabidhiwa rasmi na Mkutano Mkuu wa Chama.

Kwa maoni yangu, muda umefika sasa wakutenganisha kofia mbili. Ukizingatia kuwa Kazi za Rais ni nyingi sana na hasa ukizingatia kuwa leo shughuli za SERIKALI ZA MITAA (LOCAL GOVERMENT) kwa asilimia kubwa inashughulikiwa na CENTRAL GOVERMENT jambo ambalo zamani hai
kuwa hivyo. CCM isiogope kutenganisha kofia mbili. Tuna iomba sana ITENGANISHE KOFIA MBILI KWA MAENDELEO YA NCHI NA WATU WAKE.
 
Haiwezi kuwa Mkuu, Rais kutokuwa Mwenyekiti wa Chama maana yake unajenga chama ndani ya Chama, unajenga kundi lenye nguvu ndani ya chama, unajenga mazingira ya watu kukosa 'heshima na hofu' juu ya Rais maana wanajua hana 'meno' kwenye chama.

Hii ndiyo ilileta changamoto pale South Africa, Zuma alikosa power na akaacha kuogopwa na hatimaye akina Rampho wakamtumia Chairperson ku'push agenda ya kumuondoa Zuma.

Ndani ya Chama, Mwenyekiti anayo nguvu kubwa sana. I bet CCM hawatofanya hili kosa.
Mkuu kwa hiyo leo Ramphosa ana kofia mbili?
 
Ili ccm ibakie salama kofia mbili zitenganishwe. Mwenyekiti asiwe na nguvu kuliko wanachama
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Mkuu Fuso, wana maana kuwa mgombea Rais wa CCM itakapo tokea amechaguliwa kuwa RAIS wa Nchi basi ile siku anaapishwa tu apewe na cheo/nadaraka yake ya kuwa Mwenyekiti wa Chama cha CCM, maana kwa utaratibu wa sasa, Rais anayemaliza muda wake huwa amebakiza miaka 2 ya uwenyekiti wake na hivyo kulazimika kujiuzuru mwaka mmoja kabla na kumkabidhi kofia hiyo Rais Mteule awe na kofia mbili akisubili kukabidhiwa rasmi na Mkutano Mkuu wa Chama.

Kwa maoni yangu, muda umefika sasa wakutenganisha kofia mbili. Ukizingatia kuwa Kazi za Rais ni nyingi sana na hasa ukizingatia kuwa leo shughuli za SERIKALI ZA MITAA (LOCAL GOVERMENT) kwa asilimia kubwa inashughulikiwa na CENTRAL GOVERMENT jambo ambalo zamani hai
kuwa hivyo. CCM isiogope kutenganisha kofia mbili. Tuna iomba sana ITENGANISHE KOFIA MBILI KWA MAENDELEO YA NCHI NA WATU WAKE.
Kama Katiba ya nchi yetu ilivyo ni ngumu kubadilishwa na Rais aliyeko madarakani vivyo hivyo kwa mwenyekiti wa CCM taifa ilivyo ngumu kukubali hoja ya kutenganisha uwenyekiti wake na Urais.

Mwalimu alituachia mzigo mkubwa mno, nafikiri kabla hajaamua kung'atuka angetupatia katiba mpya kwanza..hii kitu itatusesa sana..wengi watakufa, watakuwa vilema, watqfirisika hadi katiba mpya inaoatikana.

Vita bado ni mbichi.
 
Kama Katiba ya nchi yetu ilivyo ni ngumu kubadilishwa na Rais aliyeko madarakani vivyo hivyo kwa mwenyekiti wa CCM taifa ilivyo ngumu kukubali hoja ya kutenganisha uwenyekiti wake na Urais.

Mwalimu alituachia mzigo mkubwa mno, nafikiri kabla hajaamua kung'atuka angetupatia katiba mpya kwanza..hii kitu itatusesa sana..wengi watakufa, watakuwa vilema, watqfirisika hadi katiba mpya inaoatikana.

Vita bado ni mbichi.
Mkuu ni kweli Mwalimu ametuacha njia panda, maana alisema kwa sasa Rais ana kofia mbili lakini kuna hatari kama inaweza kupata Rais katili na akawa na kofia mbili, nchi itapata shida, hivyo ni vyema tukafikiria namna ya kuondoa kofia mbili
 
Kama Katiba ya nchi yetu ilivyo ni ngumu kubadilishwa na Rais aliyeko madarakani vivyo hivyo kwa mwenyekiti wa CCM taifa ilivyo ngumu kukubali hoja ya kutenganisha uwenyekiti wake na Urais.

Mwalimu alituachia mzigo mkubwa mno, nafikiri kabla hajaamua kung'atuka angetupatia katiba mpya kwanza..hii kitu itatusesa sana..wengi watakufa, watakuwa vilema, watqfirisika hadi katiba mpya inaoatikana.

Vita bado ni mbichi.
Mkuu ni kweli Mwalimu ametuacha njia panda, maana alisema kwa sasa Rais ana kofia mbili lakini kuna hatari kama inaweza kupata Rais katili na akawa na kofia mbili, nchi itapata shida, hivyo ni vyema tukafikiria namna ya kuondoa kofia mbili
 
  • Thanks
Reactions: Ame
CCM imeitisha mkutano mkuu maalumu kufanya marekebisho ya katiba yake kwa kuwapa majukumu wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), kuwarejesha kwenye NEC makatibu wa mikoa na kofia mbili kwa nafasi za uongozi wa juu.

Haya ni mabadiliko ya 17 kufanyika ndani ya chama hicho kilichoanzishwa mwaka 1977 baada ya kuunganishwa kwa vyama vya Tanganyika African National Union (Tanu) cha iliyokuwa Tanganyika, na Afro-Shiraz cha Zanzibar.

Mabadiliko ya mwisho yalifanyika mwaka 2017 yaliyoendana na kuwapunguza wajumbe wengi kwenye vikao vya juu vya chama sababu kubwa ikitajwa ni gharama ingawa kulikuwa na nyingine zilizotajwa nyuma ya pazia.

Hata hivyo, mkutano huu unaotarajiwa kufanyika Aprili mosi pia kuna wana-CCM watatu wenye kesi ya ukosefu wa maadili mbele ya chama na Kamati Kuu imeagiza waitwe kujieleza, akiwamo Humphrey Polepole aliyekuwa mbunge wa kuteuliwa na Rais na sasa ameteuliwa Balozi wa Tanzania nchini Malawi.

Mkutano mkuu maalumu wa mwaka 2017 uliowafukuza uanachama wana-CCM 12 na wengine kuonywa, pia ulimpa onyo Dk Emmanuel Nchimbi ambaye baadaye aliteuliwa kuwa balozi wa Tanzania nchini Brazil, wengine ni wabunge Josephat Gwajima (Kawe) na Jerry Silaa (Ukonga). Huenda mkutano huu unakuzungumzia hatma ya wana-CCM hao.

Taarifa ya mwisho ya CCM iliyotolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka ilisema Kamati Kuu iliagiza wabunge hao waitwe kujieleza kutokana na dosari na mienendo yao.

Mabadiliko ya katiba
Mabadiliko ya katiba ya mwisho yaliwaondoa ujumbe wa Nec makatibu wa CCM wa mikoa waliokuwa wakiingia kwa nafasi zao na kuwaacha wenyeviti wa CCM wa mikoa kuendela kuwa wa-NEC.

Hata hivyo, taarifa za ndani za CCM zilisema kuondolewa kwa makatibu hao kumetengeneza udhaifu wa utekelezaji wa maagizo yanayotolewa na Nec, kwa kuwa baadhi ya wenyeviti hawayafikishi kwa makatibu wao, huyafikisha kwa kuchelewa au kwa tafsiri isiyo sahihi.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, makatibu wa mikoa ambao ndio watendaji wa chama kwenye maeneo yao, mara kadhaa wameshindwa kutekeleza maagizo ya NEC na kudhoofisha shughuli za chama kwa kuwa hawakuyapata kwa usahihi au hayakufika kabisa.

Kuondolewa NEC
Chanzo chetu kilisema makatibu hao waliondolewa baada ya wajumbe wa NEC ya kumtafuta mgombea urais wa CCM iliyofanyika Septemba 21, 2015, kuimba “tuna imani na Lowassa” wakati Mwenyekiti wa CCM kwa wakati huo Jakaya Kikwete akiingia ukumbini.

Kipindi hicho kilikuwa cha mchakato ndani ya CCM wa kumtafuta mgombea urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 na jina la Edward Lowassa lilikuwa limekatwa na vikao vya mwanzo.

Chanzo chetu kilisema makatibu wa mikoa wanahesabika ni watumishi wa chama, lakini kwa wakati huo hakuna aliyesimama kumtetea mwenyekiti kwa kuupinga wimbo huo.

Wa-NEC kupewa majukumu
Kwa mujibu wa chanzo chetu, wajumbe wa Nec hasa wa wanaowakilisha mikoa wamekuwa wakilalamika hawana majukumu ya kufanya baada ya vikao wanavyohudhuria vya Nec na kamati za siasa za mikoa yao.

Mabadiliko haya yanakwenda kuwapa majukumu wa-Nec kwa kuwanganisha na wajumbe wa mitaa ili waongeze nguvu kuratibu kazi za chama kwenye mashina ya maeneo yao.

Kofia mbili
Kwa mujibu wa chanzo chetu CCM inatarajia kurejesha mfumo wa uongozi wa kofia mbili kwa zile nafasi nyeti, ili wahusika waingie kwa nafasi zao.

Mfano, Rais anapochaguliwa kushika uongozi wa nchi vile vile awe mwenyekiti wa chama kwa nafasi yake badala ya kwenda kuchaguliwa tena ndani ya chama.

Hali ilivyo sasa, uchaguzi ndani ya CCM na ule wa nchi unafanyika tofauti, hivyo, kiongozi anayeondoka kwenye nafasi ya urais anabaki kuwa mwenyekiti wa chama hadi uchaguzi utakapofanyika mwaka mmoja baadaye.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, hiyo imekuwa ikiwalazimu wenyeviti hao kujiuzulu nyadhifa hizo ili kumpa nafasi aliye madarakani kuongoza Serikali na chama.

Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa (marehemu) alijiuzulu uenyekiti wa chama na kumuachia Jakaya Kikwete aliyekuwa amechukua uongozi wa nchi na Kikwete alipoondoka madarakani alijiuzulu uenyekiti na kumuchia John Magufuli (marehemu).

Kwa mujibu wa chanzo chetu hilo linategemea na hiari ya mtu na wakati mwingine imekuwa ngumu katika utendaji wa kazi za Rais pale anapoingia kwenye vikao vya chama kama mwalikwa akisubiri muda wa uchaguzi.

Kauli ya Shaka
Katibu mwenezi wa CCM, Shaka alisema sababu ya kufanya marekebisho ya katiba ni kuongeza kasi ya ufanisi wa kazi za chama na utekelezaji wa maamuzi ya vikao vya chama.

Shaka alisema pia lengo lingine ni kuongeza na kuimarisha udhibiti wa chama na viongozi wake wanaochaguliwa na kuongoza kusimamia utekelezaji wa ilani ya CCM kupiti Serikali za mitaa.

Mabadiliko yapunguza ajira
Mabadiliko hayo yaliondoka na ajira zaidi ya 170, hasa makatibu wasaidizi wa mikoa na wilaya na wenye vyeo visivyotambulika katika katiba waliokuwa wakilipwa mishahara, huku ikiondoa mzigo wa posho, ikielezwa kuwa kazi zao zitafanywa na makatibu wa jumuiya. Katika mlolongo huo, wamo makatibu wasaidizi wa mikoa ambao idadi yake ni 32 na wilaya 139, walipoteza ajira zao.

Mabadiliko mengine ni kupunguza wajumbe waliokuwa na kofia mbili kama vile wabunge na wajumbe wa Nec, isipokuwa tu pale ambapo wanalazimika kwa mujibu wa nafasi zao.

Chanzo: Mwananchi
Mtu anaweza kuwaza, wanawarudisha hao kwakua ni wateuliwa kwahiyo wanauwezo wa kupewa maelekezo na wakayatekeleza kwakua wakikataa wanatenguliwa teuzi zao...Mungu saidia nchi yangu...:"CCM dhaifu itazaa serikali dhaifu" wosia wa baba!
 
Kama Katiba ya nchi yetu ilivyo ni ngumu kubadilishwa na Rais aliyeko madarakani vivyo hivyo kwa mwenyekiti wa CCM taifa ilivyo ngumu kukubali hoja ya kutenganisha uwenyekiti wake na Urais.

Mwalimu alituachia mzigo mkubwa mno, nafikiri kabla hajaamua kung'atuka angetupatia katiba mpya kwanza..hii kitu itatusesa sana..wengi watakufa, watakuwa vilema, watqfirisika hadi katiba mpya inaoatikana.

Vita bado ni mbichi.
Kwahili nakubaliana na wewe...Mwl alikuwa na dhamira njema ili nchi isijeikaingia mikononi mwa maadui na viongozi wakashindwa kudhibiti raia wengi ambao ni masikini na ambao hawana uelewa wakutosha, tatizo ni akina sisi maslahi binafsi kupitia kichaka cha maslahi ya taifa. Kuna watu historia itawahukumu kwakujali mambo yao binafsi kuliko ya wananchi
 
Kofia mbili tatizo lake ni kuwa inaondoa wengi kwenye maamuzi na kufanya wachache kudhibiti wenzao huku wao wakiweza kusukuma agenda zao binafsi. Sijui kwanini watanzania tunakuwa wabinafsi hivi!
 
Haiwezi kuwa Mkuu, Rais kutokuwa Mwenyekiti wa Chama maana yake unajenga chama ndani ya Chama, unajenga kundi lenye nguvu ndani ya chama, unajenga mazingira ya watu kukosa 'heshima na hofu' juu ya Rais maana wanajua hana 'meno' kwenye chama.

Hii ndiyo ilileta changamoto pale South Africa, Zuma alikosa power na akaacha kuogopwa na hatimaye akina Rampho wakamtumia Chairperson ku'push agenda ya kumuondoa Zuma.

Ndani ya Chama, Mwenyekiti anayo nguvu kubwa sana. I bet CCM hawatofanya hili kosa.
Ni vizuri kusoma na kuelewa ndipo tuandike au tujibu. Hakuna kokote paliposemwa kuondolewa kofia mbili. Kofia mbili zinarudi, lakini kutegemea nafasi. Sasa hivi mwenyekiti wa chama (taifa) hatapigiwa kura tena. Atakuwa mwenyekiti kwa sababu ya nafasi yake. Ina maana raisi akimaliza muda wake, akifariki, au kuacha uraisi kwa sababu yoyote, yule anayechukuwa nafasi yake anakuwa automatically mwenyekiti wa chama (taifa) bila kuita kikao cha kumchagua/kumuidhinisha.
 
Hilo ndio dhumuni kubwa ili fomu ya kugombea 2025 ichapishwe moja tu!! Yule bibi anaweweseka ndani na nje ya chama chake.
Kofia mbili tuseme kuanzia Mwenyekiti wa CCM Taifa asiwe pia Rais wa nchi siyo !! ama ?
 
Back
Top Bottom