Dodoma: Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe avamiwa, apigwa na kujeruhiwa na watu wasiojulikana

Dodoma: Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe avamiwa, apigwa na kujeruhiwa na watu wasiojulikana

Freeman Mbowe kapoteza vingi sana katika kipindi cha miaka 5; biashara, marafiki na sasa wamemvunja mguu… binafsi sijawahi kusikia hata kauli moja ya Mbowe akimtusi mtu. Kinachosikitisha zaidi ni kwamba viongozi wa upinzani bungeni wanaishi kwenye makazi rasmi sio uchochoroni.

Nimeinukuu mahali.

Kwa mtazamo wangu naona nchi hii inatenegeneza uasi na ulipizaji kisasi ambao watawala watauita ugaidi toka watu wasiojulikana kuja wanaojulikana. Kwa kauli za Muloto ni wazi anawajua na anafurahi kilichomkuta Mbowe.

Tunaposema ubaguzi upo kila sehemu duniani hii ndiyo maana yake. Bora ubaguzi wa mzungu kuliko wa mtu mweusi. Mtu mweusi anakubagua, anakunyanyasa, anakufilisi, anakufunga kwa kesi za uwongo. Ukipona uko anaamua kukuvamia akuue ili upotee kabisa. Ssa wale watu maarufu wapase sauti.
 
Sure mkuu

Na kwa hali ya sasa ya CDM na mbowe ni ya kumuonea huruma zaidi kuliko haya

Lakini pia KUB hana ulinzi? Wako wapi wale walinzi wake??

Bado mtu ambaye haipendi CCM anaweza kabisa kufanya haya ili lawama ziende CCM, hii kitaalaamu wanaita 'third part' ambaye anafanya jambo akijua kabisa watalaumiwa watu fulani

Acha uongo, hakuna neno la kitaalamu linaitea "third part"
 
Wameanza ile Mbinu yao ya kujiteka kutafuta huruma ya Wapiga kura. Uzuri tuliokuwa Chadema tunaifahamu hii mbinu ya kutafuta kiki za kisiasa. Mbowe amejiteka. Acheni ujinga wenu wa kuyasumbua masikio yetu.
Na endeleeni kujiombea kujiteka, One day Alshab babu watawafanyia kweli mbwea nyie ambao hamjui madhara ya hiyo mbinu ya kisenge

Huna haja ya kutukana mkuu..... nikwambie tu kwa uwezo wa Jeshi letu kama Mbowe kajiumiza mwenyewe dakika sifuri wangekuwa washamkamata (nisichowapendea polisi wetu huwa hawana siri).....AMINI.......
 
It's where we can notice the big difference between black americans and africans, this is totally intolerable!
 
Ina maana pamoja na bandiko la Jana kuwa viongozi wa chadema ni wanunuaji wa machangudoa mwenyekiti nae kajeruhiwa na dada poa
 
Mnadhimu wa kambi ya upinzani bungeni mh Bulaya ameongea na waandishi wa habari na kusema Mbowe ana maumivu makali na kwa sasa wao kama chama wanajipanga kumhamishia Dsm kwa matibabu zaidi.

Maendeleo hayana vyama!
 
Si rahisi kuwatenga uvccm na ugaidi huu
 
Dah....ajabu sana[emoji2960]
tapatalk_1591687797247.jpg
 
Nianze Kwanza kwa Kutoa Pole zangu za dhati kabisa kwa Mheshimiwa Freeman Mbowe, Familia yake, Wapiga Kura wake, Wanachama wake wa CHADEMA, Wanasiasa mbalimbali, Wabunge na Sisi Watanzania wa kawaida tusioegemea upande wowote ule (Mzukulu) nikiwemo kwa kilichotokea. Naamini Mwenyezi Mungu ataupigania Uhai wake ila kwa waliohusika Maulana / Mola atawajibu kwa Adhabu Kali kabisa.

Jana nilipoziona tu zile Nondo Kali na zenye Mashiko za Mheshimiwa Tundu Lissu nilihisi kabisa kuwa ili kuwapoteza Watu na Kuyahamisha Mawazo yao katika Kukijadili au Kuyajadili yale aliyoyaandika ambayo yote ni mazuri basi ni lazima tu Spinning ya Hatari ingefanyika. Kilichofanyika ni kutaka Kufunika alichokifanya Lissu jana kuanzia leo Watanzania wote tujikite zaidi katika Kuzungumzia hili lililomkuta Mheshimiwa Freeman Mbowe.

Na Kiutaalam zaidi ili kuonyesha kuwa hawa Wahuni wanaolelewa vibaya na walijipanga ni kwamba itakuwa walijipanga tokea pale Taarifa za Mheshimiwa Tundu Lissu aliposema kuwa atazungumza na Watanzania hivyo hata Wao walishajipanga na walipoona Jana Mheshimiwa Tundu Lissu katoa Nondo ile Kabambe basi na Wao wakaamua Kulitekeleza hilo walilolitekeleza.

Kuna Mmoja namuheshimu sana humu ila sasa nitaanza Kumdharau amesema kuwa Mheshimiwa Mbowe Kavamiwa na Majambazi akiwa na Kimada aliyemnunua. Ameshindwa kujua ya kwamba Siku zote Mbinu za Kijasusi huwa zinaratibiwa vyema na Kimkakati zaidi kwa kuwahusisha Magenge ya Wahuni ili hata likija Kufanikiwa basi hao Majasusi wasijulikane moja kwa moja kama ni Wao.

Kwa hali ilivyo na kwa uelewa wangu mdogo sana wa Masuala ya Usalama ( Ujasusi ) ila wale wanaojua zaidi yangu hapa JF watanisaidia ni kwamba kwa Nyakati tuliopo na kwa Hofu ya Wapinzani na Agenda zao, na kwa Uchungu wa Kulikosa Jimbo la Hai ambalo wanalitaka na kwa kutaka Kuleta Hofu na Vitisho nitakuwa wa mwisho Kuamini kama katika hili Tukio la Mbowe hayo Mapanga hayakuwa na Sumu za Kijasusi.

Namalizia tu kwa kusema kama Tanzania ya sasa imefikia hapa ambapo Wanasiasa wanafanyiwa mambo haya mabaya halafu nchi ina Kiongozi Mkuu na ina Idara yake ya Usalama na mambo (matukio) haya yanatokea kila Kukicha ila wanayanyamazia basi huenda kwa Mwaka huu Tanzania ikawa na Vifo vingi vya Wanasiasa (hasa wa Upinzani) na Wanaharakati kuliko wale ambao labda CORONA ingewauwa au imewauwa.

Nawaombea LAANA mbaya sana na Kali mno kwa Mwenyezi Mungu hawa Wote wanaoyafanya haya na hasa huyo Mkubwa wao anayewatuma.
Acheni kujitekenya na kucheka wenyewe. Seriously Lisu awe Rais?
Nothing ktk hotuba yote kaonyesha uanaharakati tuu. Huwezi shida kwa style hiyo ya ku attack kila organ. Soon mtaanza kusema mmeibiwa kabla ya uchaguzi.
Vizuri kufikiria (ve+)
 
Mmh hizi si dalili nzuri kabisa kuelekea uchaguzi mkuu. Njia zote zimeshindikana sasa hii ya kuumizana ndio silaha yao ya mwisho iliyobaki. KUKICHWA KUTAMBAZUKA. WAKATI SI MILELE.

Jr[emoji769]
Hakuna kitu hapo ni kiki tu
Yaleyale ya Lisu , kapigwa kushoto kavimba kulia!
 
Ukimsikiliza Msigwa wajumbe wa kikao chao nyumbani kwa Mbowe ni wale wanaojulikana kama Wajumbe wa kamati ndogo ya kamati kuu. Pale amekosekana Reggy na Mrema tu!

Sasa walikuwa wakijadili hotuba ya Lissu au mkakati gani? Je hilo tukio kutokea immediately baada ya kikao haiwezekani kuwa tukio hilo ni maazimio ya kikao hicho?

Siasa hizi za kufungwa mapiopio na kulazwa zilikuwa ni michezo ya Lytonga Mrema enzi hizo. Ninachokiona mimi hawa vijana wa Mrema wa wakati huo Msigwa na Lema wamemwingiza kingi Bw Mbowe!

Nasisitiza the next victim ni Lissu

Ngoja muda utatuambia


Sent from my itel Prime 4 using JamiiForums mobile app
 
Mimi nina mashaka Inawezekana hizi ni njama ndani ya chama kumpoteza Mbowe ili kuwapokonya watu wa Kilimanjaro Chama chao.
 
Swali la kwanza kujiuliza hivi mbowe hana ulinzi ? nikajiuliza hapo nyumbani kwake walipomvamia pakoje mpaka kiongozi mkubwa wa upinzani kukung'utwa ? baadae nasikia hakuwa nyumbani.

Niseme tu kuwa Freeman Mbowe alikuwa anatafuta kupigwa vizuri ikiwezekana kutekwa kabisa , nimemshangaa kiongozi mkuu wa upinzani (Mbowe) wakati anajua kabisa hali ya siasa nchini tena kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu , yeye anaishi kijinga jinga tu , anatembea usiku bila intelijensia yoyote yaani yupo yupo tu , anatembea usiku bila mpango yani hana hata silaha yoyote kama vile nchi hii yakwako.

Yeye anajua kabisa kisiki kilichobaki katika upinzani ni yeye na anajua watu wasiojulikana wapo kazini masaa 24 , alafu anategemea miujiza ya mungu imshukie tena katika utawala huu .... sawa naweza kusema ukitafutwa kwa dhana maalum ya kukuua au kukujeruhi watakufuata popote lakini hiyo sio tija , tija ni unaishije katika makundi ya maadui zako , mawasilano yako yakoje?

Chakula chako kinaangaliwa vipi? safari zako zinafanyikaje? ratiba yako ya siku inaisha saa ngapi? ulinzi wako umeimarishwaje ? sio unaishi kwa kutegemea fair play utakufa ... na wapinzani wengine muwe makini nchi hii sio yenu .....
 
Seriously,unatembea usiku mnene na hauwezi kujihakikishia ulinzi wako?,,
Sawa na yule alikuwa akilalamika anafuatiliwa na watu kisha akashauliwa achukue tahadhari,yeye akachukulia poa,matokeo yake akashambuliwa,
Hii sio game,,be serious

Sioni hoja yako ni ipi hapa, tatizo ni kutembea usiku au tatizo ni usalama mdogo wa viongozi wa upinzani? Maana kama tatizo ni kutembea usiku, Lisu yeye alishambuliwa mchana kweupe.

Na kama suala ni viongozi wa upinzani kuhitaji ulinzi kwa ajili ya usalama wao, basi Lisu ameomba zaidi ya mara moja ahakikishiwe usalama wake, lakini hakuna aliye tayari kumpa huo ulinzi. Wakati mwingine ndugu jiepushe na kutetea uovu, kwa sababu za kuungaunga.
 
Back
Top Bottom