Dodoma: Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe avamiwa, apigwa na kujeruhiwa na watu wasiojulikana

Dodoma: Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe avamiwa, apigwa na kujeruhiwa na watu wasiojulikana

Utawala huu umekuwa wa kishenzi sana, tulipofikia hakuna tofauti na ule utawala dhalimu wa Dikteta Nduli Idd Amin. Magufuli atambue tu kwamba hata yeye hatoishi milele, na huenda kifo chake kikawa ni SHEREHE KWA WENGI.
 
Daaa pole kamanda wetu japo Kuna mropokaji anae snitch kasema ulikunywa ulanzi mpak ukazima du sijui ni mdudu gani ameingia kwenye kichwa cha Li jua likaliii
 
June 9, 2020
Julius Nyerere international airport
Dar es Salaam, Tanzania

Freeman Aikaeli Mbowe asafirishwa kwa ndege na kuwasili ktk uwanja wa ndege wa Julius Julius Nyerere International Airport jijini Dar es Salaam ili kupata matibabu ya ziada ktk hospitali kubwa baada ya kushmbuliwa na watu wasiojulikana katika makazi yake rasmi mjini Dodoma Tanzania

 
Nimurudia mara nne ulichowakilisha , mkuu kwa kuwa umekwenda sana personal nasita kukuambia siwezi kukujibu. Kwa kuwa ninatakiwa kwenda persoal ili niwakilishe mawazo na muono wangu kwa ufasaha. Na kwa uelewa wangu huu uwanja sio sahihi.

Nashukuru nimekuelewa, umetumia maneno mengi kuwakilisha kilichomo akilini mwako. Naomba urudie mara nne uweze kujua umewakilisha nini ?. Nafarijika nimeupata ufahamu na uelewa wako kupitia kwa ulichowakilisha.

Huu ni mjadala wa wazi ndugu....

Kama una la kusema, usisite. Zungumza (andika) tu. Nitakusoma...

Mimi niliona tuwekane sawa tu ili kama wasomi, japo hili ni jukwaa la siasa, lakini wakati mwingine tujadili mambo ktk uhalisia wake...

Niliona kuwa mnajibishana na yule ndugu mambo ya kufikirika zaidi badala ya reality...
 
Nianze Kwanza kwa Kutoa Pole zangu za dhati kabisa kwa Mheshimiwa Freeman Mbowe, Familia yake, Wapiga Kura wake, Wanachama wake wa CHADEMA, Wanasiasa mbalimbali, Wabunge na Sisi Watanzania wa kawaida tusioegemea upande wowote ule (Mzukulu) nikiwemo kwa kilichotokea. Naamini Mwenyezi Mungu ataupigania Uhai wake ila kwa waliohusika Maulana / Mola atawajibu kwa Adhabu Kali kabisa.

Jana nilipoziona tu zile Nondo Kali na zenye Mashiko za Mheshimiwa Tundu Lissu nilihisi kabisa kuwa ili kuwapoteza Watu na Kuyahamisha Mawazo yao katika Kukijadili au Kuyajadili yale aliyoyaandika ambayo yote ni mazuri basi ni lazima tu Spinning ya Hatari ingefanyika. Kilichofanyika ni kutaka Kufunika alichokifanya Lissu jana kuanzia leo Watanzania wote tujikite zaidi katika Kuzungumzia hili lililomkuta Mheshimiwa Freeman Mbowe.

Na Kiutaalam zaidi ili kuonyesha kuwa hawa Wahuni wanaolelewa vibaya na walijipanga ni kwamba itakuwa walijipanga tokea pale Taarifa za Mheshimiwa Tundu Lissu aliposema kuwa atazungumza na Watanzania hivyo hata Wao walishajipanga na walipoona Jana Mheshimiwa Tundu Lissu katoa Nondo ile Kabambe basi na Wao wakaamua Kulitekeleza hilo walilolitekeleza.

Kuna Mmoja namuheshimu sana humu ila sasa nitaanza Kumdharau amesema kuwa Mheshimiwa Mbowe Kavamiwa na Majambazi akiwa na Kimada aliyemnunua. Ameshindwa kujua ya kwamba Siku zote Mbinu za Kijasusi huwa zinaratibiwa vyema na Kimkakati zaidi kwa kuwahusisha Magenge ya Wahuni ili hata likija Kufanikiwa basi hao Majasusi wasijulikane moja kwa moja kama ni Wao.

Kwa hali ilivyo na kwa uelewa wangu mdogo sana wa Masuala ya Usalama ( Ujasusi ) ila wale wanaojua zaidi yangu hapa JF watanisaidia ni kwamba kwa Nyakati tuliopo na kwa Hofu ya Wapinzani na Agenda zao, na kwa Uchungu wa Kulikosa Jimbo la Hai ambalo wanalitaka na kwa kutaka Kuleta Hofu na Vitisho nitakuwa wa mwisho Kuamini kama katika hili Tukio la Mbowe hayo Mapanga hayakuwa na Sumu za Kijasusi.

Namalizia tu kwa kusema kama Tanzania ya sasa imefikia hapa ambapo Wanasiasa wanafanyiwa mambo haya mabaya halafu nchi ina Kiongozi Mkuu na ina Idara yake ya Usalama na mambo (matukio) haya yanatokea kila Kukicha ila wanayanyamazia basi huenda kwa Mwaka huu Tanzania ikawa na Vifo vingi vya Wanasiasa (hasa wa Upinzani) na Wanaharakati kuliko wale ambao labda CORONA ingewauwa au imewauwa.

Nawaombea LAANA mbaya sana na Kali mno kwa Mwenyezi Mungu hawa Wote wanaoyafanya haya na hasa huyo Mkubwa wao anayewatuma.
Haya mambo yanachochewa sana na JPM na spika huu ndio ukweli. John na Job katika action na matamko yao iwe kwa kujua au kutokujua, iwe kwa hasira au masihara wanawatia sana hamasa wafuasi wao ktk kuwa attack wanachadema. Niwazi maneno ya wanachedema yanachoma, hasa kwa serikali hii yenye mbwembwe lazima uumie. Lakini tusifike kuanza kujengeana fitina kiasi hiki, kama upinzani ni karaha kwanini tusipige marufu vyama vingi, hawa mabeberu tusiwaogope, tuwaache waendelee na democrasia yao. Yaani waafrika tunaumizana kipumbavu wakati uwezo wa kuamua mambo yetu tunao.
 
Tulipofikia Tanzania hatuna tofauti na Rwanda!! Usalama hasa wa wanasiasa wa Upinzani upo shakani.. kuna mtu hataki kusikia akikosolewa!! Yeye yupo sahihi daima.
Day dreaming inaruhusiwa
 
.
IMG-20200609-WA0015.jpg
 
Kwanza nitoe pole kwa kuumia kwa Mheshimiwa Mbowe. I wish him speedy recovery.

Huwa naumizwa sana na contradictions within contradictions. Naumizwa Pia na chuki za kijinga ambazo watu kutokana na kiki za kisiasa wanapenda kuzipanda.

Napenda kujua tu je Wale wabunge walioenda kujiweka Quarantini, wamekubaliana wenyewe kimya kimya kuwa CORONA imekwisha?

Je Mheshimiwa. Pole tena. Kwa kwenda kunywa nje Na kulewa nje. Sorry Kunywa, ni thibitisho kuwa corona schon lange vorbei ist?

Je is that simple, kipindi hiki, mtu wa upinzani na CHADEMA atume watu wampige Mwenyekiti wa CHadema kwa kisa cha kumpunguzia nguvu ya kufanya kampeni? Is it logical? Huwa ninapata tabu sana na namna ya kufikiri kwa nyie watu wa humu. Are you really ok upstairs.

Kuna wakati mtu huonekana Makini pale ambapo ananyamaza katika issues kama hizi.
 
Mmh hizi si dalili nzuri kabisa kuelekea uchaguzi mkuu. Njia zote zimeshindikana sasa hii ya kuumizana ndio silaha yao ya mwisho iliyobaki. KUKICHWA KUTAMBAZUKA. WAKATI SI MILELE.

Jr[emoji769]
Njooni kwenye box la kura tuwashinde
 
Dr. Mashinji kaandika maneno haya twita.

"Kuteleza na kuanguka ni kitu cha kawaida kutokea duniani. Si kuvunjika tu wengine hata wamepoteza maisha.

Tujitahidi kuwa makini tunapopanda ngazi hata kama ni mbili tu!"- Dr. Vincent Mashinji.

IMG_20200610_131307.jpg
 
Bila kufaulu mtihani wa kumdhihaki na kumzalilisha Mbowe,hawawezi pata uteuzi.

Kujiuzulu CHADEMA huwa ni kufaulu/kutengeneza coursework tu, ila kuishambulia CHADEMA na hasa Mbowe, huwa ndio kufaulu final examination(UE) ambayo ina asilimia kubwa ya marks zote almost 60%.

Mashinji kaanza UE hivyo msimshangae akimaliza paper yake hii vizuri na kufaulu,basi mwalimu wake, Dr. ...... (jina linahifadhiwa) atampatia uteuzi kulingana na ufaulu wake.
 
Dah Mbowe amekua dhahabu kwa CCM, yaani ukitaka Mwenyekiti wao akuone kwenye uteuzi wewe mtaje Mbowe, utaonekana kama vile umeviunja amri sijui ya Kwanza ile...Usilitaje bure jina la bwana MUNGU wako.....
 
Back
Top Bottom