Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ww ndio utakua mpumbavu wa ubongoPumbavu.
Nimurudia mara nne ulichowakilisha , mkuu kwa kuwa umekwenda sana personal nasita kukuambia siwezi kukujibu. Kwa kuwa ninatakiwa kwenda persoal ili niwakilishe mawazo na muono wangu kwa ufasaha. Na kwa uelewa wangu huu uwanja sio sahihi.
Nashukuru nimekuelewa, umetumia maneno mengi kuwakilisha kilichomo akilini mwako. Naomba urudie mara nne uweze kujua umewakilisha nini ?. Nafarijika nimeupata ufahamu na uelewa wako kupitia kwa ulichowakilisha.
Haya mambo yanachochewa sana na JPM na spika huu ndio ukweli. John na Job katika action na matamko yao iwe kwa kujua au kutokujua, iwe kwa hasira au masihara wanawatia sana hamasa wafuasi wao ktk kuwa attack wanachadema. Niwazi maneno ya wanachedema yanachoma, hasa kwa serikali hii yenye mbwembwe lazima uumie. Lakini tusifike kuanza kujengeana fitina kiasi hiki, kama upinzani ni karaha kwanini tusipige marufu vyama vingi, hawa mabeberu tusiwaogope, tuwaache waendelee na democrasia yao. Yaani waafrika tunaumizana kipumbavu wakati uwezo wa kuamua mambo yetu tunao.Nianze Kwanza kwa Kutoa Pole zangu za dhati kabisa kwa Mheshimiwa Freeman Mbowe, Familia yake, Wapiga Kura wake, Wanachama wake wa CHADEMA, Wanasiasa mbalimbali, Wabunge na Sisi Watanzania wa kawaida tusioegemea upande wowote ule (Mzukulu) nikiwemo kwa kilichotokea. Naamini Mwenyezi Mungu ataupigania Uhai wake ila kwa waliohusika Maulana / Mola atawajibu kwa Adhabu Kali kabisa.
Jana nilipoziona tu zile Nondo Kali na zenye Mashiko za Mheshimiwa Tundu Lissu nilihisi kabisa kuwa ili kuwapoteza Watu na Kuyahamisha Mawazo yao katika Kukijadili au Kuyajadili yale aliyoyaandika ambayo yote ni mazuri basi ni lazima tu Spinning ya Hatari ingefanyika. Kilichofanyika ni kutaka Kufunika alichokifanya Lissu jana kuanzia leo Watanzania wote tujikite zaidi katika Kuzungumzia hili lililomkuta Mheshimiwa Freeman Mbowe.
Na Kiutaalam zaidi ili kuonyesha kuwa hawa Wahuni wanaolelewa vibaya na walijipanga ni kwamba itakuwa walijipanga tokea pale Taarifa za Mheshimiwa Tundu Lissu aliposema kuwa atazungumza na Watanzania hivyo hata Wao walishajipanga na walipoona Jana Mheshimiwa Tundu Lissu katoa Nondo ile Kabambe basi na Wao wakaamua Kulitekeleza hilo walilolitekeleza.
Kuna Mmoja namuheshimu sana humu ila sasa nitaanza Kumdharau amesema kuwa Mheshimiwa Mbowe Kavamiwa na Majambazi akiwa na Kimada aliyemnunua. Ameshindwa kujua ya kwamba Siku zote Mbinu za Kijasusi huwa zinaratibiwa vyema na Kimkakati zaidi kwa kuwahusisha Magenge ya Wahuni ili hata likija Kufanikiwa basi hao Majasusi wasijulikane moja kwa moja kama ni Wao.
Kwa hali ilivyo na kwa uelewa wangu mdogo sana wa Masuala ya Usalama ( Ujasusi ) ila wale wanaojua zaidi yangu hapa JF watanisaidia ni kwamba kwa Nyakati tuliopo na kwa Hofu ya Wapinzani na Agenda zao, na kwa Uchungu wa Kulikosa Jimbo la Hai ambalo wanalitaka na kwa kutaka Kuleta Hofu na Vitisho nitakuwa wa mwisho Kuamini kama katika hili Tukio la Mbowe hayo Mapanga hayakuwa na Sumu za Kijasusi.
Namalizia tu kwa kusema kama Tanzania ya sasa imefikia hapa ambapo Wanasiasa wanafanyiwa mambo haya mabaya halafu nchi ina Kiongozi Mkuu na ina Idara yake ya Usalama na mambo (matukio) haya yanatokea kila Kukicha ila wanayanyamazia basi huenda kwa Mwaka huu Tanzania ikawa na Vifo vingi vya Wanasiasa (hasa wa Upinzani) na Wanaharakati kuliko wale ambao labda CORONA ingewauwa au imewauwa.
Nawaombea LAANA mbaya sana na Kali mno kwa Mwenyezi Mungu hawa Wote wanaoyafanya haya na hasa huyo Mkubwa wao anayewatuma.
Day dreaming inaruhusiwaTulipofikia Tanzania hatuna tofauti na Rwanda!! Usalama hasa wa wanasiasa wa Upinzani upo shakani.. kuna mtu hataki kusikia akikosolewa!! Yeye yupo sahihi daima.
Pole au kebehi? Pumbav.Mkuu mbona nimetoa pole
Aliyekupa uthibitsho kuwa amekunywa ni nani? vipimo vya daktari labda au kelele na propaganda za wabunge wa CCM?Je Mheshimiwa. Pole tena. Kwa kwenda kunywa nje Na kulewa nje
Njooni kwenye box la kura tuwashindeMmh hizi si dalili nzuri kabisa kuelekea uchaguzi mkuu. Njia zote zimeshindikana sasa hii ya kuumizana ndio silaha yao ya mwisho iliyobaki. KUKICHWA KUTAMBAZUKA. WAKATI SI MILELE.
Jr[emoji769]