Dodoma: Uchaguzi wa Viongozi wa TLS umeingia Katika hali ya Sintofahamu, mfumo wa “Mjue Wakili” wagoma

Dodoma: Uchaguzi wa Viongozi wa TLS umeingia Katika hali ya Sintofahamu, mfumo wa “Mjue Wakili” wagoma

Abdul Said Naumanga

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2024
Posts
673
Reaction score
1,318
IMG_5407.png
Kutoka katika Ukumbi wa JKCC uliopo jijini Dodoma, mawakili wa Tanzania Bara wamekusanyika kwa ajili ya zoezi muhimu la kupiga kura kuchagua Rais, Makamu wa Rais, na viongozi wengine wa Chama cha Mawakili Tanzania bara(Tanganyika Law Society - TLS). Matokeo ya uchaguzi huu yanatarajiwa kutolewa leo mchana.​

IMG_5405.jpeg

Hata hivyo, hali ya sintofahamu imeibuka miongoni mwa wapiga kura kutokana na mfumo wa "Mjue Wakili" almaarufu kama E-Wakili kushindwa kufanya kazi. Hali hii imeleta wasiwasi kuhusu uwepo wa mamluki, mawakili wasio huisha (renew) leseni hasa mawakili wa serikali, ambao inaaminika wameletwa na baadhi ya wagombea ili kuhujumu wapinzani wao.

Ikumbukwe kuwa ni mawakili wa kujitegemea walio huisha lesini zao za uwakili pekee ndiyo wenye haki na ruhusa ya kupiga kura katika uchaguzi wa TLS, hivyo kutopatikana kwa mtandao wa E-Wakili kunaleta changamoto kubwa ya kuthibitisha uhalali wa wapiga kura.

Kwa taarifa zaidi nitawafahamisha wakuu.

PIA FATILIA: LIVE: Uchaguzi Wa Rais TLS: Nani Kuibuka Kidedea Urais TLS
 
Kuna nchi inaitwa Tanganyika? Mimi ninavyofahamu ni Tanzania Bara na Visiwani, Tanganyika iliishia 1964​
Ninachojuwa mimi kuna Tanganyika na Zanzibar.

Mzanzibar hata siku moja hawezi kujitambulisha ni wa visiwani, wanajitambulisha Wazanzibar.

Kwa nini TLS wanatumia jina la Tanganyika badala ya Tanzania bara?
 
Kutoka katika Ukumbi wa JKCC uliopo jijini Dodoma, mawakili wa Tanzania Bara wamekusanyika kwa ajili ya zoezi muhimu la kupiga kura kuchagua Rais, Makamu wa Rais, na viongozi wengine wa Chama cha Mawakili Tanzania bara(Tanganyika Law Society - TLS). Matokeo ya uchaguzi huu yanatarajiwa kutolewa leo mchana.​


Hata hivyo, hali ya sintofahamu imeibuka miongoni mwa wapiga kura kutokana na mfumo wa "Mjue Wakili" almaarufu kama E-Wakili kushindwa kufanya kazi. Hali hii imeleta wasiwasi kuhusu uwepo wa mamluki, mawakili wasio huisha (renew) leseni hasa mawakili wa serikali, ambao inaaminika wameletwa na baadhi ya wagombea ili kuhujumu wapinzani wao.

Ikumbukwe kuwa ni mawakili wa kujitegemea walio huisha lesini zao za uwakili pekee ndiyo wenye haki na ruhusa ya kupiga kura katika uchaguzi wa TLS, hivyo kutopatikana kwa mtandao wa E-Wakili kunaleta changamoto kubwa ya kuthibitisha uhalali wa wapiga kura.

Kwa taarifa zaidi nitawafahamisha wakuu.​
MaCCM ni majitu ya ovyo sana. Yanamuogopa Mwabukusi kuliko kitu chochote. Yamwache Mwabukusi aingie madarakani ainyooshe nchi.
 
Kama vigezo na masharti ya kupiga kura havijakidhi, si waahirishe hilo zoezi!?
Zoezi lenyewe lilisimama kwa zaidi ya saa zima kwa kisingizio kwamba Karatasi za kupigia kura ziliisha, sasa swali la kujiuliza ni je TLS walikua hawajui idadi kamili ya mamber wao ambao wapo na vigezo vya kupiga kura?🤔​
 
Me naona tuna wapa airtime hawa TLS Hawana msaada wowote wala umuhimu wowote .zaidi ya kutoa pro bono ambazo wana haribu kazi wana zifanya very shallow .yani ni bora uuze shamba umlipe wakili kuliko kwenda kuomba pro bono kwa hawa TLS uta haribiwa case yako wata ifanya ili mradi tu
 
Me naona tuna wapa airtime hawa TLS Hawana msaada wowote wala umuhimu wowote .zaidi ya kutoa pro bono ambazo wana haribu kazi wana zifanya very shallow .yani ni bora uuze shamba umlipe wakili kuliko kwenda kuomba pro bono kwa hawa TLS uta haribiwa case yako wata ifanya ili mradi tu
Mwabu alishasema TLS ni jeshi la kisheria, wananchi tunalalamika sana kuhusu mikataba mibovu, sasa tuna solve vipi hili suala bila kuipata TLS inayo wajibika.

NB: Simpigii kampeni mgombea yeyote, ila najaribu kukuonyesha umuhimu wa TLS nchini mbali na izo pro bono unazosema​
 
Zoezi lenyewe lilisimama kwa zaidi ya saa zima kwa kisingizio kwamba Karatasi za kupigia kura ziliisha, sasa swali la kujiuliza ni je TLS walikua hawajui idadi kamili ya mamber wao ambao wapo na vigezo vya kupiga kura?🤔​
Kuna wengine waliletwa kutoka Zanzibar, wamelipiwa tickets kabisa 😂, hawa ndio wanaleta taharuki
 
Kuna nchi inaitwa Tanganyika? Mimi ninavyofahamu ni Tanzania Bara na Visiwani, Tanganyika iliishia 1964​
Hivi huwa hauwasikilizi viongozi wa Zanzibar wanapohutubia mikutano yao?
Wanasema" serikari zetu mbili "

Hautakuja kusikia wakisema serikali ya Tanzania katika maswala yao.
Wanasema serikali ya mapinduzi ya Zanzibar.
 

Propaganda za uchaguzi wa TLS
 
Kutoka katika Ukumbi wa JKCC uliopo jijini Dodoma, mawakili wa Tanzania Bara wamekusanyika kwa ajili ya zoezi muhimu la kupiga kura kuchagua Rais, Makamu wa Rais, na viongozi wengine wa Chama cha Mawakili Tanzania bara(Tanganyika Law Society - TLS). Matokeo ya uchaguzi huu yanatarajiwa kutolewa leo mchana.​


Hata hivyo, hali ya sintofahamu imeibuka miongoni mwa wapiga kura kutokana na mfumo wa "Mjue Wakili" almaarufu kama E-Wakili kushindwa kufanya kazi. Hali hii imeleta wasiwasi kuhusu uwepo wa mamluki, mawakili wasio huisha (renew) leseni hasa mawakili wa serikali, ambao inaaminika wameletwa na baadhi ya wagombea ili kuhujumu wapinzani wao.

Ikumbukwe kuwa ni mawakili wa kujitegemea walio huisha lesini zao za uwakili pekee ndiyo wenye haki na ruhusa ya kupiga kura katika uchaguzi wa TLS, hivyo kutopatikana kwa mtandao wa E-Wakili kunaleta changamoto kubwa ya kuthibitisha uhalali wa wapiga kura.

Kwa taarifa zaidi nitawafahamisha wakuu.

PIA FATILIA: LIVE: Uchaguzi Wa Rais TLS: Nani Kuibuka Kidedea Urais TLS
Serikali inayowajumu wapiga kura wake
 
Back
Top Bottom