Dogo Edu wa Tamthilia ya Pazia ndiye muigizaji Bora kijana atakayekuja kushika Bongomovie

Dogo Edu wa Tamthilia ya Pazia ndiye muigizaji Bora kijana atakayekuja kushika Bongomovie

Ndio maana nikasema tamthiliya kuwa ndefu ni changamoto halafu mbaya zaidi series haina hata Full Script.

Mtunzi wa Huba kuna matukio anajichanganya na kuyafanya yasiwe na maana Kwa mtazamaji

Na ni kama anasahau characters wake katika episode za nyuma waliigiza nini.
 
Jua kali alijitahidi Sana mwanzoni katika upangiliaji wa visa vyake.

Ila kadri anavyoendelea anazidi kuharibu tu.
 
Mbona mtunzi wa huba amefeli sana.
Watunzi wa Huba ni wakenya ambao ni mwanahabari Rashid Abdallah, Zara Mwangi na kuna mwandishi mwingine alikuwaga anaitwa Ibrahim Chitayi wakishirikiana na waandishi wengine kutoka kenya na producer ni lulu hassan ambaye mmewe ni Rashid. Kiukweli Huba ndio baba wa tamthilia zote unazoziona kwenye tv hata Selina na kikubwa kinachoifanya Huba ikae hewani na Dstv kutoa pesa kubwa kwao ni idadi ya watazamaji wake na ule ndo moyo wa Dstv. Licha ya mapungufu machache wamekuwa wanapokea ushauri na kufanya marekebisho hasa director na mwandishi.
 
Huyu anayejisifia kwa lips nzuri mtoto wa kiume...tuletee mwingine
 
Hivi inakuaje kila tamthilia wanakua wanaonesha wapo kitandani na kuvaa nguo za kulalia?
Ila make ups na kope bado vimejaa usoni.
 
Back
Top Bottom