Z kali
Member
- May 25, 2022
- 86
- 159
Nawasalimu nyote,
Ni baba angu mkubwa kabisa, ni mstaafu mpya kutoka serikalini ana mwaka ivi na miezi kadhaa uraiani.
Akiwa kazini alioa na kupata watoto wanne, mambo yalikuwa POA tu amani na furaha, watoto wamekuwa na washaolewa/kuoa
Mwaka Jana mzee akamaliza mda wa utumishi wake na kusitaafu kwa amani kabisa. Sasa mwaka huu mwazoni, nazan January mzee akataka kuongeza mke wa pili, na ikawa ivo, akajipatia dogodogo Kama yule wa mzee (hayati) Mrema, M/Mungu amlaze pema, ili amliwaze na kumrudisha utotoni Kama sio ujanani.
Siku zikapita mitala ikaendelea kama ilivoamrishwa. Aisee! mwez huu mwanzoni mzee alipata maradhi, kwenda hospital hana damu, kaongezewa chupa 4 na maji ya kutosha, hali mbaya, hamna nafuu, wakichek vipimo ugonjwa hauonekani, labda kalogwa, Mara itakuwa katupiwa jini, Mara ivi Mara vile.
Kwa bahati mwanae kaja majuzi Kati, yy anaishi mkoa mwingne, akashauri mzee acheki HIV/AIDS, na ikawa ivo na kwa bahati mbaya mzee kakutwa na maambukizi ya HIV.
Wakaitwa wake zake wote wawili nao ikabidi kupimwa HIV/AIDS na kwa bahati mbaya tena mke mdogo (dogodogo) anakutwa na maambukizi na bahati nzuri kwa mke mkubwa Yuko salama.
Sasa baada ya purukushani za hapa na pale, ikaonekana bi mdogo ndo kampa mzee ngoma, baada ya kubanwa bi mdogo akakiri ni kweli Yuko na maambukizi MIAKA MITANO Sasa na anatumia dozi, mzee aligoma kuamini first time aisee, ilikuwa noma Sana ila now kakubali matokeo na ameanza kutumia dozi rasmi.
Mzee alisitaafu vizuri kabisa ila mtaa hauna hurama, Ugonjwa upo wakuu, tuchukue tahadhari.
Assalam alaekum
Tujiandae na maswali 100 ya SENSA kesho
Ni baba angu mkubwa kabisa, ni mstaafu mpya kutoka serikalini ana mwaka ivi na miezi kadhaa uraiani.
Akiwa kazini alioa na kupata watoto wanne, mambo yalikuwa POA tu amani na furaha, watoto wamekuwa na washaolewa/kuoa
Mwaka Jana mzee akamaliza mda wa utumishi wake na kusitaafu kwa amani kabisa. Sasa mwaka huu mwazoni, nazan January mzee akataka kuongeza mke wa pili, na ikawa ivo, akajipatia dogodogo Kama yule wa mzee (hayati) Mrema, M/Mungu amlaze pema, ili amliwaze na kumrudisha utotoni Kama sio ujanani.
Siku zikapita mitala ikaendelea kama ilivoamrishwa. Aisee! mwez huu mwanzoni mzee alipata maradhi, kwenda hospital hana damu, kaongezewa chupa 4 na maji ya kutosha, hali mbaya, hamna nafuu, wakichek vipimo ugonjwa hauonekani, labda kalogwa, Mara itakuwa katupiwa jini, Mara ivi Mara vile.
Kwa bahati mwanae kaja majuzi Kati, yy anaishi mkoa mwingne, akashauri mzee acheki HIV/AIDS, na ikawa ivo na kwa bahati mbaya mzee kakutwa na maambukizi ya HIV.
Wakaitwa wake zake wote wawili nao ikabidi kupimwa HIV/AIDS na kwa bahati mbaya tena mke mdogo (dogodogo) anakutwa na maambukizi na bahati nzuri kwa mke mkubwa Yuko salama.
Sasa baada ya purukushani za hapa na pale, ikaonekana bi mdogo ndo kampa mzee ngoma, baada ya kubanwa bi mdogo akakiri ni kweli Yuko na maambukizi MIAKA MITANO Sasa na anatumia dozi, mzee aligoma kuamini first time aisee, ilikuwa noma Sana ila now kakubali matokeo na ameanza kutumia dozi rasmi.
Mzee alisitaafu vizuri kabisa ila mtaa hauna hurama, Ugonjwa upo wakuu, tuchukue tahadhari.
Assalam alaekum
Tujiandae na maswali 100 ya SENSA kesho