Dola hutumia nadharia njama kututoa tusijadili mambo ya maana badala yake tujadili uzushi?

Dola hutumia nadharia njama kututoa tusijadili mambo ya maana badala yake tujadili uzushi?

Nadharia Njama (Consipirancy Theory) ni hali ya kuamini kwamba kuna taasisi au watu fulani wanahusika kufanya jambo fulani la siri kwa faida yao. Lakini pia inawezekana ikawa ni hoja fikirishi ya kutungwa dhidi ya kitu fulani lakini hoja yenyewe isiwe ya kweli.

Siku moja miaka ya themanini (1987) kulitokea habari kwamba kwenye eneo fulani kule Buguruni kuna mtu kageuka nyoka. Zama zile kulikuwa hakuna mitandao ya kijamii wala teknolojia ya kusafirisha habari kama ilivyo hivi sasa, lakini habari hiyo ilisambaa kwenye mji wa Dar es salaam kwa kasi ya ajabu sana. Ghafla mji mzima ukashikwa na taharuki na kukawa na heka heka kubwa sana ya watu kuelekea Kituo cha Polisi Buguruni kwenda kumuona huyo mtu aliyegeuka kuwa nyoka.

Habari hii haikuwa mwisho wa habari kama hizo kutokea katika taifa letu. Na aghalabu habari zenyewe huja wakati kama Taifa huwa tunakuwa kwenye hali fulani inayohitaji mjadala wa Kitaifa. Kwa waliosoma kwenye shule za umma za Dar es salaam miaka ya sabini na themanini, watakumbuka vurumai za wanafunzi kutimua mbio kisa wameambiwa kuna Mumiani au majini yanakuja kwenye shule yao. Kuna wakati shule hadi zililazimika kufungwa kwa kuwa waalimu hawakuwa na amani kwenda shule kufundisha na wazazi nao ,walikuwa na hofu ya watoto wao kunyonywa damu ama na Majini au Mumiani.

Lakini hebu tujiulize, hivi ile habari ya "Rama mla watu" iliishaje? Ilikuwaje Taifa zima likasombwa kwenda Samunge kwa Babu? Nani anajiuliza dalali alikubalije kuziuza nyumba za Lugumi kwa kuambiwa tu kuwa "mia tisa itapendeza zaidi" na Dokta Shika?

Au hizi habari huwa zinazushwa ili kutupumbaza tusijali na kujadili mambo ya msingi kwa Taifa letu??
Tume ya Mipango ambapo namba mbili wa sasa alikulia huko
 
Nadharia Njama (Consipirancy Theory) ni hali ya kuamini kwamba kuna taasisi au watu fulani wanahusika kufanya jambo fulani la siri kwa faida yao. Lakini pia inawezekana ikawa ni hoja fikirishi ya kutungwa dhidi ya kitu fulani lakini hoja yenyewe isiwe ya kweli.

Siku moja miaka ya themanini (1987) kulitokea habari kwamba kwenye eneo fulani kule Buguruni kuna mtu kageuka nyoka. Zama zile kulikuwa hakuna mitandao ya kijamii wala teknolojia ya kusafirisha habari kama ilivyo hivi sasa, lakini habari hiyo ilisambaa kwenye mji wa Dar es salaam kwa kasi ya ajabu sana. Ghafla mji mzima ukashikwa na taharuki na kukawa na heka heka kubwa sana ya watu kuelekea Kituo cha Polisi Buguruni kwenda kumuona huyo mtu aliyegeuka kuwa nyoka.

Habari hii haikuwa mwisho wa habari kama hizo kutokea katika taifa letu. Na aghalabu habari zenyewe huja wakati kama Taifa huwa tunakuwa kwenye hali fulani inayohitaji mjadala wa Kitaifa. Kwa waliosoma kwenye shule za umma za Dar es salaam miaka ya sabini na themanini, watakumbuka vurumai za wanafunzi kutimua mbio kisa wameambiwa kuna Mumiani au majini yanakuja kwenye shule yao. Kuna wakati shule hadi zililazimika kufungwa kwa kuwa waalimu hawakuwa na amani kwenda shule kufundisha na wazazi nao ,walikuwa na hofu ya watoto wao kunyonywa damu ama na Majini au Mumiani.

Lakini hebu tujiulize, hivi ile habari ya "Rama mla watu" iliishaje? Ilikuwaje Taifa zima likasombwa kwenda Samunge kwa Babu? Nani anajiuliza dalali alikubalije kuziuza nyumba za Lugumi kwa kuambiwa tu kuwa "mia tisa itapendeza zaidi" na Dokta Shika?

Au hizi habari huwa zinazushwa ili kutupumbaza tusijali na kujadili mambo ya msingi kwa Taifa letu??

Mijadala isiyokuwa na matendo haiwezi kuwa na tija.
 
Ndivyo ilivyo. Ripoti ya siejii na pisisibii zilipokelewa siku moja kabla ya ujio wa Kamala ili kupunguza attention. Baada ya mgeni kuondoka tukapigwa na mazingaombwe ya mawaziri wawili kubadilishana wizara
 
Habari nyingine za maana lakini zinakuja wakati mbaya. Kwa mfano habari ya mashoga. Sasa watu walioainishwa na CAG kwamba wameiba hela wote watasepa wakati sisi tunawatafuta mashoga.
Au,persistently,watu wanasema Magufuli ameuawa. Useless people,wale Kigogo na yule Veronica France,wanazungumza maneno yasiyokuwa na maana. Lakini we are not getting enough information to investigate it.
 
Hakuna kazi iliyo rahisi kama kulitawala fuvu la Mtanzania. wewe lijaze Simba Yanga halafu anzisha kauzushi kadogo mengine liachie fuvu hilo litajaza lenyewe.

Wewe njoo kwenye vijiwe vya kahawa vya huku Tandika usikie yanayojadiliwa mambo ya kipuuzi na propaganda za CUF.

Nyerere aliua elimu na sasa matokeo tunayaona mitaani.
Ulitaka watu wasijadili habari za michezo,Burudani n.k wajadili siasa tu? Wapi ipo hivyo duniani?
 
Nadharia Njama (Consipirancy Theory) ni hali ya kuamini kwamba kuna taasisi au watu fulani wanahusika kufanya jambo fulani la siri kwa faida yao. Lakini pia inawezekana ikawa ni hoja fikirishi ya kutungwa dhidi ya kitu fulani lakini hoja yenyewe isiwe ya kweli.

Siku moja miaka ya themanini (1987) kulitokea habari kwamba kwenye eneo fulani kule Buguruni kuna mtu kageuka nyoka. Zama zile kulikuwa hakuna mitandao ya kijamii wala teknolojia ya kusafirisha habari kama ilivyo hivi sasa, lakini habari hiyo ilisambaa kwenye mji wa Dar es salaam kwa kasi ya ajabu sana. Ghafla mji mzima ukashikwa na taharuki na kukawa na heka heka kubwa sana ya watu kuelekea Kituo cha Polisi Buguruni kwenda kumuona huyo mtu aliyegeuka kuwa nyoka.

Habari hii haikuwa mwisho wa habari kama hizo kutokea katika taifa letu. Na aghalabu habari zenyewe huja wakati kama Taifa huwa tunakuwa kwenye hali fulani inayohitaji mjadala wa Kitaifa. Kwa waliosoma kwenye shule za umma za Dar es salaam miaka ya sabini na themanini, watakumbuka vurumai za wanafunzi kutimua mbio kisa wameambiwa kuna Mumiani au majini yanakuja kwenye shule yao. Kuna wakati shule hadi zililazimika kufungwa kwa kuwa waalimu hawakuwa na amani kwenda shule kufundisha na wazazi nao ,walikuwa na hofu ya watoto wao kunyonywa damu ama na Majini au Mumiani.

Lakini hebu tujiulize, hivi ile habari ya "Rama mla watu" iliishaje? Ilikuwaje Taifa zima likasombwa kwenda Samunge kwa Babu? Nani anajiuliza dalali alikubalije kuziuza nyumba za Lugumi kwa kuambiwa tu kuwa "mia tisa itapendeza zaidi" na Dokta Shika?

Au hizi habari huwa zinazushwa ili kutupumbaza tusijali na kujadili mambo ya msingi kwa Taifa letu??
Mbona huzungumzii habari za hovyo za online TV. Moja imeandika "ailyemwua magufuli amepatikana"
 
Mbona huzungumzii habari za hovyo za online TV. Moja imeandika "ailyemwua magufuli amepatikana"
Huyo hana lengo la kuleta mjadala kukwepesha jambo, bali anafanya hivyo kwachota wajinga ili apate "Views" nyingi na labda wajinga hao watamuona yeye ni mwerevu, na mwisho wa siku wa-subscribe kwenye tovuti yake.
 

Brazil wenyewe wanapenda mpira ila huwezi kuwakuta wakijadili mpira siku nzima.

Kwetu ni too much, hebu angalia Kenya
Wenye kujadili mpira watajadili na wenye kujadili siasa muda wote watajadili ndio ipo hivyo.
 
Back
Top Bottom