Dola zimeadimika kwasababu wageni wanavuna fedha za miradi kuliko wazawa

Dola zimeadimika kwasababu wageni wanavuna fedha za miradi kuliko wazawa

kama ulikua hujui nikwambie tu kuwa hao wakandarasi wa bongo ni tia maji sana, wengi wao ni wezi na hawako punctual kwenye kazi zao, uvivu [kazi ya mwezi itakamilika ndani ya mwaka kwa visingizio vingi sana] - talking from experience.
Shida vikazi vya miamia ndo mnawapa wazawa kazi za mabilion mnawapa wachina unawaza nini wewe mwaga pesa.
 
Sababu kubwa ni kwamba there's 'No Balance of Trade.'
Bidhaa nyingi sana kama siyo bidhaa karibia zote tunaagiza kutoka nje ya nchi hii, wakati huo huo sisi hatuna bidhaa yoyote ile ya maana ambayo tunauza nje ya nchi hii.
Kuna ma IT wengi Tanzania ambao wanaweza kutengeneza software na kuuza duniani kote ila shida ni upokeaji wa fedha.
Tanzania ni jehanamu, unanunua software kwa paypal ila huwezi kupokea pesa kutoka paypal😁😁😁😁. Ukiangalia viongozi wanakula rushwa, wanafanya ufisadi wa kila namna ila wanaogopa paypal.
 
Shida vikazi vya miamia ndo mnawapa wazawa kazi za mabilion mnawapa wachina unawaza nini wewe mwaga pesa.
Makandarasi wa kibongo hawana exposure, dili nyingi wanapewa na mzee kaishia darasa la saba unategemea nini apo au na ilo pia hujui?
 
Yaani thread zingine na justification ni vitu viwili tofauti daaah. Kiswahili hiki, kina maneno mengi sana.
Mfabo mtoa thread unayesema dollar zimeadimika, wewe dollar unatumia za kazi gani? Ukinijibu hili nitakujibu pia.
 
Kuna ma IT wengi Tanzania ambao wanaweza kutengeneza software na kuuza duniani kote ila shida ni upokeaji wa fedha.
Tanzania ni jehanamu, unanunua software kwa paypal ila huwezi kupokea pesa kutoka paypal😁😁😁😁. Ukiangalia viongozi wanakula rushwa, wanafanya ufisadi wa kila namna ila wanaogopa paypal.
Muongo
 
Kila siku tunalia kuhusu kuadikika Kwa Dola licha ya juhudi za kukuza Uchumi lakini hakuna ambae anajadili jambo Hilo Kwa kuangalia sababu za msingi.

Mojawapo ya vitu vinavyosababisha kuadikika Kwa Dola Nchini no hizo hapa 👇

1. Kuwapa kazi za Ujenzi wakandarasi wa kigeni badala ya wazawa Kwa visingizio vya hawana uwezo na uzoefu(wageni hulipwa Kwa Dola)

2. Kuagiza bidhaa nyingi ambazo tunaweza Kuzalisha wenyewe ndani ya mwaka eg maziwa,ngano,Mafuta ya kula,sabuni,vyakula vya mifugo,mbegu nk

3. Kukwamisha uwekezaji kutoka Nje kutokana na mitizamo ya siasa za ujamaa(kusema Nchi imeuzwa Kwa Waarabu,kuwa na sera ambazo hazitabiriki,Urasimu wa Kiserikali na Rushwa) eg miradi ya Lindi LNG na Liganga imekwama kutokana na siasa uchwara.

---
WAGENI WAVUNA FEDHA ZA MIRADI KULIKO WAZAWA

SERIKALI imesema asilimia kubwa ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inawanufaisha wageni kutoka nje ya nchi kuliko wazawa.

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema bungeni Dodoma kuwa sababu kubwa inayochangia hali hiyo ni uwezo mdogo wa makandarasi wa ndani wa kifedha, mitambo na wataalamu hivyo inakuwa vigumu kwao kushindana kwenye zabuni za kazi na makandarasi kutoka nje hasa kampuni za Kichina.

Bashungwa amesema hayo akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2024/25 bungeni Dodoma jana. Alisema kwa mujibu wa takwimu za Bodi ya Usajili wa Makandarasi, kati ya miradi 36,839, wazawa walitekeleza miradi 35,351 sawa na asilimia 95.9 ya miradi hiyo.

Hata hivyo, Bashungwa amesema miradi iliyotekelezwa na wazawa ni midogomidogo yenye thamani ya Sh trilioni 23.749, sawa na asilimia 38.5 ya thamani ya miradi yote iliyosajiliwa na kutekelezwa katika kipindi hicho ambayo ni Sh trilioni 61.638.

“Hivyo, makandarasi wa nje ambao ni takribani asilimia 4.1 walitekeleza miradi michache yenye thamani kubwa (asilimia 61.5 ya thamani ya miradi yote),” amesema Bashungwa.

Kwa mujibu wake, kuna kampuni 14,800 za ndani za makandarasi, za ushauri wa wahandisi ni 252 na kampuni za wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi ni 461.

Chanzo: Habari Leo

My Take
Naunga mkono wazo la Bashungwa kuanza kuwaamini Wakandarasi Wazawa.Sheria hii isiishie Wizara ya Ujenzi pekee Bali Taasisi zote.Tanzania sio Mali ya Wachina pekee.
Tuhamie BRICS
 
Kila siku tunalia kuhusu kuadikika Kwa Dola licha ya juhudi za kukuza Uchumi lakini hakuna ambae anajadili jambo Hilo Kwa kuangalia sababu za msingi.

Mojawapo ya vitu vinavyosababisha kuadikika Kwa Dola Nchini no hizo hapa 👇

1. Kuwapa kazi za Ujenzi wakandarasi wa kigeni badala ya wazawa Kwa visingizio vya hawana uwezo na uzoefu(wageni hulipwa Kwa Dola)

2. Kuagiza bidhaa nyingi ambazo tunaweza Kuzalisha wenyewe ndani ya mwaka eg maziwa,ngano,Mafuta ya kula,sabuni,vyakula vya mifugo,mbegu nk

3. Kukwamisha uwekezaji kutoka Nje kutokana na mitizamo ya siasa za ujamaa(kusema Nchi imeuzwa Kwa Waarabu,kuwa na sera ambazo hazitabiriki,Urasimu wa Kiserikali na Rushwa) eg miradi ya Lindi LNG na Liganga imekwama kutokana na siasa uchwara.

---
WAGENI WAVUNA FEDHA ZA MIRADI KULIKO WAZAWA

SERIKALI imesema asilimia kubwa ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inawanufaisha wageni kutoka nje ya nchi kuliko wazawa.

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema bungeni Dodoma kuwa sababu kubwa inayochangia hali hiyo ni uwezo mdogo wa makandarasi wa ndani wa kifedha, mitambo na wataalamu hivyo inakuwa vigumu kwao kushindana kwenye zabuni za kazi na makandarasi kutoka nje hasa kampuni za Kichina.

Bashungwa amesema hayo akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2024/25 bungeni Dodoma jana. Alisema kwa mujibu wa takwimu za Bodi ya Usajili wa Makandarasi, kati ya miradi 36,839, wazawa walitekeleza miradi 35,351 sawa na asilimia 95.9 ya miradi hiyo.

Hata hivyo, Bashungwa amesema miradi iliyotekelezwa na wazawa ni midogomidogo yenye thamani ya Sh trilioni 23.749, sawa na asilimia 38.5 ya thamani ya miradi yote iliyosajiliwa na kutekelezwa katika kipindi hicho ambayo ni Sh trilioni 61.638.

“Hivyo, makandarasi wa nje ambao ni takribani asilimia 4.1 walitekeleza miradi michache yenye thamani kubwa (asilimia 61.5 ya thamani ya miradi yote),” amesema Bashungwa.

Kwa mujibu wake, kuna kampuni 14,800 za ndani za makandarasi, za ushauri wa wahandisi ni 252 na kampuni za wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi ni 461.

Chanzo: Habari Leo

My Take
Naunga mkono wazo la Bashungwa kuanza kuwaamini Wakandarasi Wazawa.Sheria hii isiishie Wizara ya Ujenzi pekee Bali Taasisi zote.Tanzania sio Mali ya Wachina pekee.
Sababu namba 2 Ndiyo ya msingi kunasababisha tusiwe wabunifu
 
Kuna kitu kinafichwa ....
Ni kwamba mradi wa ujenzi wa bwawa kufua umeme la Julius Nyerere zilikopwa hela kutoka nje kwa mfumo wa kibiashara ..
Yaani kulipa inakuwa na riba kubwa sana na kwa muda mfupi ..
Serikali inabidi kulipa deni hilo kwa haraka na ni kwa dollar..

Pia kuna miradi mikubwa sana inaendelea inayohitaji dollar nyingi sana kulipa nje ya nchi ..hasa ya ujenzi iliyoanzishwa miaka michache nyuma
 
Haya ndio madudu ya serikali ya CCM.
Kama nakosea niambie wapi
 
Kuna kitu kinafichwa ....
Ni kwamba mradi wa ujenzi wa bwawa kufua umeme la Julius Nyerere zilikopwa hela kutoka nje kwa mfumo wa kibiashara ..
Yaani kulipa inakuwa na riba kubwa sana na kwa muda mfupi ..
Serikali inabidi kulipa deni hilo kwa haraka na ni kwa dollar..

Pia kuna miradi mikubwa sana inaendelea inayohitaji dollar nyingi sana kulipa nje ya nchi ..hasa ya ujenzi iliyoanzishwa miaka michache nyuma
Kwani kukopa ni nini? Unakopa harafu unampa Mchina hapo unaingiliwa mara 2
 
Sawa kwa vile unashinda Jamii forum kusoma umbeya, ukitoka unaingia whatsApp kuangalia status, ukitoka hapo unaingia Youtube kuangalia video za Mwakatobe, ukitoka hapo unaingia tiktok na unamalizia facebook huwezi kuelewa ndiyo maana umeishia na jibu moja tu la muongo.
Mitandaoni kuna pesa nyingi sana shida mfumo wa upokeaji wa fedha. Kwa akili yako huwezi kuelewa kwasababu wewe ni msoma umbeya
 
Back
Top Bottom