Donald Trump apatikana na hatia ya makosa yote 34 katika kesi ya kughushi nyaraka na kutaka kuficha kuhusu hela alizomlipa pornstar ili akae kimya

So?

Huyo jaji hawezi tu kujitungia hukumu zake anazotaka yeye.

Kuna miongozo ya kisheria.

Licha ya hivyo, ngoma bado mbichi na ikibidi itaenda mpaka kwenye mahakama ya upeo.
Mimi nazungumzia "scenario" kwamba ikiwa Dolad Trump atahukumiwa itakuwaje kuhusiana na kampeni ya uchaguzi wa November na hapohapo kutekeleza jukumu la mahakama kuzingatia sheria kufuata mkondo wake.

Pia kwa wazee wa baraza kufikia uamuzi wa kwamba Trump ana hatia ya mashtaka yote 34 hiyo yatoa mwanya kwa upande wa Trump kukata rufaa ambayo yaweza kushinda.

Ni ukweli usofichika kwamba hii kesi ina mkono wa kisiasa.
 
Trump hakuonewa kabisa na wala siy hisia; ni sheria imetumika kama kawaida. Kumbuka kuwa makosa haya haya yamesababisha watu wengine wafungwe jela kabisa.

Concern yangu ilikuwa ni madai yako kuwa Trump angekuwa madarakani kusingetokea vita huko Ukraine na Gaza. Statement hiyo ndiyo imenifanya niwe na concern sana na nitakuja kukutafuta nikujulie hali. Siwezi kupumzika nikiwa na wasiwasi na well being ya ndugu yangu wa karibu kama wewe.
 
Trump ameshakutwa na hatia. Hivyo, anasubiri kusomewa hukumu July.

Sheria za New York au pengine USA zipoje? Atakata rufaa kabla ya hukumu au ni baada?

Tunaombeni maarifa Wakuu..
 
Hii ni kesi uchwara.

Hukumu itatenguliwa kwenye rufaa.

Natumaini tutairejea hii mada siku ya siku ikiwadia.
 
Badili kichwa cha habari, usitulishe matango pori

Kumlipa mtu asitoe siri yako ya kulala nae sio kesi mahala popote duniani
Donald Trump apatikana na hatia ya kughushi nyaraka.
 
Trump ana mengi tu ya siri na hili ni moja tu. Tusisahau sheria haingalii wewe ni nani. Uzurinwa sheria kama uou have a clean hand kwa wenzetu hujulikana tu, ni suala la muda.
 
Trump ameshakutwa na hatia. Hivyo, anasubiri kusomewa hukumu July.

Sheria za Manhattan zipoje? Atakata rufaa kabla ya hukumu au hata kesho?

Tunaombeni maarifa Wakuu..
Hakuna sheria za Manhattan 🤣.

Wengi mnaochangia hapa hata hamna uelewa mdogo wa mambo ya msingi.
 
Trump ameshakutwa na hatia. Hivyo, anasubiri kusomewa hukumu July.

Sheria za Manhattan zipoje? Atakata rufaa kabla ya hukumu au hata kesho?

Tunaombeni maarifa Wakuu..
Kwa kumkuta na hatia kwa mashtaka yote 34, hiyo yatoa mwanya kwa mawakili wake kukata rufaa ambayo yaweza kupunguza hatua hizo na kisha hukumu nzima kuangaliwa upya.
 
Trump ana mengi tu ya siri na hili ni moja tu. Tusisahau sheria haingalii wewe ni nani. Uzurinwa sheria kama uou have a clean hand kwa wenzetu hujulikana tu, ni suala la muda.
Lakini ukumbuke kwamba kesi hii na kukutwa na hatia kisha hukumu hakutamzuia Donald Trump kugombea uraisi kwenye uchaguzi mwezi Novemba.
 
Hakuna sheria za Manhattan 🤣.

Wengi mnaochangia hapa hata hamna uelewa mdogo wa mambo ya msingi.
Weye umefahamu vipi uwezo wa hao wengi kwamba wana uelewa mdogo wa mambo ya msingi?
 
Wamarekani waje wajifunze Tanzania. Eti kumkopa mwanamke ngono Ni kosa??? Au kuhonga Ni kosa? Watu wako bungeni kwasababu ya hongo, Kuna wanawake wamekalia vyeo kisa rushwa ya ngono.
Eti mcheza picha za ngono. Huku Africa watu wenye heshima na madaraka wanashiriki kabisa.
Aisee Ni ngumu Sana kuishi marekani.
Nadhani hata punyeto marekani Ni kosa na MTU unafungwa jela kabisa.
 
Tatizo kubwa la Trump ni majivuno na kiburi chake.

Kilichomponza Trump ni ego yake. Kosa la kwanza la kumlipa mwanamke afiche siri siyo siyo crime, na vile vile kudanganya (siyo kugushi) kwenye document za kibiashara siyo crime. Hili la kudanganya linakuwa crime tu kama lilifanyika ili kuficha kosa jingine. Sasa hapo kwenye ufichaji wa kosa jingine ndipo ego ya trump ilipompoza kwani iliwezekana kabisa kumlipa huyo mwanamke bila kuhusisha na uchaguzi ila akagtumia njia za kuwadharau waliokuwa wanamsaidia, na ndio waliomtosa.

Ukifuatia kosa la documents liliko mahakama ya Miami, nayo utagundua pia kuwa ni ego yake ndiyo iliyomletea matatizo. Idara ya kumbukumbu ilimwomba makaratasi matatu tu: (a) Barua aliyoachiwa na Obama (b) Barua aliyoandikiwa na Kim Jong Il (c) ramani iliyokuwa inatumika kuonyesha njia ya Hurricane Dorian. Lakini yeye kwa ego yake akawasumbua kwa zaidi ya mwaka mzima mpaka wakatumia amri ya mahakama na mwishowe kuvamia nyumbani kwa na kukuta document nyingi za serikali ambazo hakutakiwa kuwa nazo ambazo alikuwa anajitahidi sana kuzificha.

Baada ya kujikuta kuwa kosa lake dogo la ego limezaa tatizo kubwa kisheria, yeye anageuza kuwa la kisiasa na majuzi tu anasema kuwa Biden aliamuru FBI watumie deadly force kumkamata na kusahahu kuwa issue ilikuwa ni idara ya nyaraka za serikali.
 
You really believe that? Ila Marekani safari hii wako between a rock and a hard place, mchague Trump mhalifu, au Biden muungaji mkono mauaji Gaza. Wengi hawatapiga kura kwa sababu wataona ni choice between two devils you know.


Nimependa neneo "You know"
 
Mkuu, hii kesi leo wazee wa baraza wamemtia hatiani Donald Trump kwa makosa yote 34 ya kughushi nyaraka kuhusiana na pesa alozitoa kwa yule mwanamke zinoitwa "Hush Money".

Hivyo akiwa madarakani akawezesha nyaraka kughushiwa yaani kuchakachua na kurekebisha mahesabu kwamba fedha alozilipa ama ni ndogo au hakikuwepo kabisa,

Hivyo hii kesi yahusu Hush Money au Hush Money Trial.

NB
Hizi fedha za hash au Hush Money ni zile fedha unozilipa kwa mchepuko ili asije kutoa siri/taarifa zako nje au kumfunga mdomo pale siri au taarifa hizo zinapoleta dhahama kwako au familia yakop na mstakabali mzima wa maisha yako.
 
I hope it backfires on them big time in November.

1. He is not going to jail.

2. He is still running for president [and now I’m voting for him].
Kwanini alitaka Ku rig uchaguzi aliyoshindwa
 
Hakuna sheria za Manhattan 🤣.

Wengi mnaochangia hapa hata hamna uelewa mdogo wa mambo ya msingi.
Unaumiza kichwa bure wengi wako brainwashed na bbc, ukiangalia taarifa za habari lazima uwe walking zombie,The World Need Trump Now for better future.
 
Demokrasia ya Marekani ishakufa.

Marekani hawana tena uhalali wa kuzikoromea nchi zingine kuhusu demokrasia.
Lakini, miongoni mwa principles muhimu za demokrasia ni pamoja na Rule of Law. Hakuna aliye juu ya sheria.

Wanademokrasia wanaweza kutumia tukio hilohilo kama kielelezo kuwa demokrasia ya Marekani ni imara sana na ndio maana hata mtu ambaye ameshawahi kuwa rais wa nchi ameweza kushtakiwa na kukutwa na hatia.

Kuna nchi ambazo marais wana kinga za maisha za kutoshtakiwa kwa makosa yoyote. Hakuna anayefikiria hata kupeleka kesi ya jinai mahakamani dhidi yao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…