Donald Trump: Assad amekimbia nchi. Ni muda wa Putin na Zelensky kuachana na ukichaa unaoendelea; wakae chini wayamalize

Donald Trump: Assad amekimbia nchi. Ni muda wa Putin na Zelensky kuachana na ukichaa unaoendelea; wakae chini wayamalize

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Muda mfupi baada ya kuwepo kwa taarfa kuwa Bashar Al Assad amekimbia nchi na kwenda kusikojulikana, Rais mteule wa Marekani Donald Trump ametoa tamko

Trump amesema kuwa moja ya sabu ya Assad kuanguka ni kwa sababu hakupata msaada kutoka kwa Urusi na kuongeza kuwa ni muda muafaka sasa kwa Putin na Zelensky kukaa chini kumaliza tofauti zao

======================================================

Assad is gone. He has fled his country.His protector, Russia, Russia, Russia, led by Vladimir Putin, was not interested in protecting him any longer.

There was no reason for Russia to be there in the first place .They lost all interest in Syria because of Ukraine, where close to 600,000 Russian soldiers lay wounded or dead, in a war that should never have started, and could go on forever.

Russia and Iran are in a weakened state right now, one because of Ukraine and a bad economy, the other because of Israel and its fighting success.

Likewise, Zelenskyy and Ukraine would like to make a deal and stop the madness. They have ridiculously lost 400,000 soldiers, and many more civilians.

There should be an immediate ceasefire and negotiations should begin.

Too many lives are being so needlessly wasted, too many families destroyed, and if it keeps going, it can turn into something much bigger, and far worse.I know Vladimir well.

This is his time to act. China can help. The World is waiting!”



Putin.jpeg
 
Ni suala la muda tu, Ayatollah (Iran) na Putin (Russia) nao watatembea mbele. Kila jambo na muda wake.
 
Hakuna Rais humo,
Rais wa Marekani anatakiwa ku stand up kwa nguvu dhidi ya Russia aggression.
Mkuu, wewe ungeweza kupambana na ukuta wa zege la Mjerumani? Anachoweza kufanya Marekani ni kumbwekea tu kama mbwakoko.

Suala la kumbutua, hilo sahau kabisa. Kama ingewekana, JB na utawala wake wangeshafanya miaka 3 iliyopita. Lakini wanajua matokeo yake ni mabaya kuliko kumwacha ajiendee atakavyo.

Kwa bahati nzuri Putin anakuwaga na hesabu nzuri mno - anamwona Mmarekani anakoelekea kabla hata Beberu hajaanza kufanya maandalizi ya kuondoka.

Ni suala la muda tu, Ukreni inaenda kuwa chakula cha jioni cha Urusi - ama kwa maridhiano au makabiliano.
 
Ni suala la muda tu, Ayatollah (Iran) na Putin (Russia) nao watatembea mbele. Kila jambo na muda wake.
Mbona hutaji nchi za NATO na washirika wake kibao ambao viongozi na marais wao wameliwa vichwa kwa sababu ya SMO?

Give credit where it's due. Wapi Boris Johnson? Wapi Joe Biden na Kamala? Wapi nguvu na mabavu ya PM wa Ujerumani? Wapi vitisho vya Abrams na ATACAMS? Wapi afisa wao kindakindani, komredi T14 Armata ?
 
Mkuu, wewe ungeweza kupambana na ukuta wa zege la Mjerumani? Anachoweza kufanya Marekani ni kumbwekea tu kama mbwakoko.

Suala la kumbutua, hilo sahau kabisa. Kama ingewekana, JB na utawala wake wangeshafanya miaka 3 iliyopita. Lakini wanajua matokeo yake ni mabaya kuliko kumwacha ajiendee atakavyo.

Kwa bahati nzuri Putin anakuwaga na hesabu nzuri mno - anamwona Mmarekani anakoelekea kabla hata Beberu hajaanza kufanya maandalizi ya kuondoka.

Ni suala la muda tu, Ukreni inaenda kuwa chakula cha jioni cha Urusi - ama kwa maridhiano au makabiliano.
Hiyo vita kama sio West kujivuta vuta wakati inaanza huku Ukraine ikipambana kivyake kwa miezi kadhaa wakati huu Mrusi angeshakuwa ametepeta. Ilikuwa ni makosa makubwa kusikiliza vitisho vya Putin mwanzo wa vita.
 
Trump anafikiria kuendesha nchi na geopolitics zake ni kama kufanya biashara ya Hotel zake! Kila muda "deal", "deal", deal.... tu!🤣
 
Democrats ndo wana hiyo tabia
Siasa za Marekani zimebadilika sana, zamani Republicans ndio walikuwa wakali zaidi dhidi ya wakomunisti, Russia na madikteta kuliko Democrats. Marais kama Ronald Reagan walikuwa na uso wa kazi kweli kwa viongozi wa USSR.
 
Hiyo vita kama sio West kujivuta vuta wakati inaanza huku Ukraine ikipambana kivyake kwa miezi kadhaa wakati huu Mrusi angeshakuwa ametepeta. Ilikuwa ni makosa makubwa kusikiliza vitisho vya Putin mwanzo wa vita.
Siyo kwamba walitumia busara? Maana wangejiendea kichwa kichwa, wangemwagiwa tindikali ya Mrusi na kuguyuguzwa kwenye makombora yasiyo na majina.

Mkuu, usimdharau Mrusi hata kidogo. Jamaa ameweza kuikabili NATO yote (nchi karibu 100 kwa pamoja) bila mwenyewe kutikisika! Hilo huoni?

Hata Marekani yenyewe inashangaa jinsi Russia ilivyo imara mpaka sasa, na tena uchumi wake ukistawi kuliko kabla ya vita, na zaidi ya kiwango cha ukuaji wa uchumi wa Ulaya na Marekani kwa pamoja.

Unasemaje sasa kwamba angemalizwa kitambo - wakati awali ndipo alikuwa bado hajachomoa hata silaha moja?

Unachotakiwa kutambua ni kwamba Marekani na NATO safari hii wameshikwa pabaya, na aibu hii wataisimulia karne na karne. Heri mara mia hata ile ya Vietnam, Kyuba, na juzijuzi hapa kule Afghanistani.

Kubalini kwamba supapawa wenu ndiye wa mchongo!

Umesema, Ilikuwa ni makosa makubwa kusikiliza vitisho vya Putin mwanzo wa vita, kwa hiyo unamaanisha supapawa wenu anamwogopa nani sasa? Mbona?!
 
Marekani ni Taifa la kinafiki sana. Yeye na mdogo wake Israel wameshiriki kumuondoa Assad ili tu kuwakomoa Iran na Urusi!! Na wakati huo huo wamesahau huyo kibaraka wao waliymuunga mkono, aliwahi kuwa mwanachama mtiifu wa mtandao maarufu wa kigaidi, wa Al Qaida.
 
Back
Top Bottom