Dotnata afanya kufuru kwa kvuta "Hummer" la nguvu

Dotnata afanya kufuru kwa kvuta "Hummer" la nguvu

Mh! jamani msimshambulie sana ndiyo ubongo ulipofikia kutuletea habari kama hiii. Unakuta familia za watu wanakufa njaa wewe unafanya ubishoo ili watu wakujue. Ila kwa mdada sidhani kama ana ubavu huo na kama anao na amenunua mashauzi hayo. Glory be to God. Mungu amuondelee uvivu wa kufikiri maana Hammer is nothing compared to the life we have.

P
 
I was about to say bei ya Hummer used haipo hivyo what i know Hummer zina range from 60,000 - 75,000 US$ so bi dada asitake sifa za kijinga kanunua sawa asijitangaze kama kapigwa.

Ukweli hiyo aliyo nunua ni used na hakuna bongo Hummer yoyote iliyotoka kiwandani na mbongo akawa First user.

Hilo Hummer aseme kanunua used..2010 GM walibaki na Hummer 2200 na zote zilishaisha...lakini kwani Hummer Big deal? mbona yamezagaa jamani na used Hummers Na used Hummers Prices ranger zake ni $28000-$61 000 while brand new toka kiwandani ambayo hayapo tena sa ivi price range zake ni $129,399.00 for the open-top; the wagon $140,796.00, H1 Alpha was priced at $150,975.00...in that range so huyu aiswafanywe watoto wadogo
 
Mi naona ni jambo zuri, la kimaendeleo, linaonyesha jinsi sanaa ilivyo na faida, na inaonyesha jinsi mwanamke anavyoweza kuinvest kwenye kitu kikubwa na bila kuwa na ulimbikeni.

mtazamo wangu ni kuwa ameona uelekeo wa sinema za kitanzania utahitaj kitu kama kile, hongera dada.
kama nyie mko mahali Hammer sio dili, mwenzenu yuko mahali anaona kama ni dili ya biashara,
KAma ambavyo wewe unachofanya hapo sio dili kwake
 
Hivi kukodisha "Hummer" kwa masaa 24 ni TZS ngapi?

Nataka kutoka na nyumba ndogo wikiendi kwenda Loliondo kupata "kikombe"
 
Huyu Mama huwa anapenda cheap publicity kinoma na kila miaka inavyoenda huwa hakui
 
Kufuru iko wapi hapa? Kama ni bei kwani linauzwa shillingi ngapi?

Halafu hummer ni outdated cars, hazitengenezwi tena gari.
 
MSANII matawi ya juu katika tasnia ya filamu Bongo, Husna Mohamed Posh ‘Dotnata’ amefanya kufuru baada ya kutoa ‘burungutu’ kununua‘mkoko’ wa kifahari aina ya Hummer, Amani Jipya limeinyaka.

Akizungumza na gazeti hili muda mfupi baada ya kukamilisha taratibu mbalimbali za kuukomboa mkoko huo kutoka katika Bandari ya Dar es Salaam, Dotnata alisema kuwa ametumia kiasi cha shilingi za kibongo Milioni 270 kununua ‘mchuma’ huo kutoka katika tawi la kiwanda cha magari hayo huko Detroit, nchini Marekani.

“Kila mtu atasema lake lakini ni kweli nimenunua gari hili kutoka Marekani na nimetumia kiasi cha shilingi milioni 270 mpaka linafika hapa,” alisema Dotnata.Akiendelea zaidi, msanii huyo mwenye heshima kubwa ndani ya tasnia ya filamu za Kibongo alianika kuwa watu wasimuelewe vibaya kwa kununua gari hilo amefanya hivyo akiwa na lengo la kulikodisha kwenye kwenye sherehe mbalimbali za kitaifa na kimataifa ili kupunguza makali ya maisha na siyo kutanua nalo kwa matanuzi yasiyo na lazima.

“Leo natarajia kukamilisha usajili hivyo mwishoni mwa wiki hii litakuwa barabarani lakini sitalitumuia kwa matanuzi kama ambavyo watu wanaweza kufikiria, nimepanga kulikodisha kwenye sherehe na hafla mbalimbali za kitaifa na kimataifa ili linisaidie kujikwamua, ” alimaliza Dotnata



Kumbe saanaa inalipa .Du somewhere somehow we made wrong career choice.Anyway its never too late to change.Contacts school of piracy?😉
 
Hivi kukodisha "Hummer" kwa masaa 24 ni TZS ngapi?

Nataka kutoka na nyumba ndogo wikiendi kwenda Loliondo kupata "kikombe"[/QUOTE]

Dada katangaza biashara, mteja huyu kapatikana
 
Hapa kuna la kujifunza. Sina tatizo na mtu kuwa na gari, gari ni muhimu sana kiasi kwamba hata kama huna nyumba unaweza ukanunua kwanza gari na nyumba (kulingana na mazingira unayoishi) ikafuata baadae. Ila nina tatizo na gari ya gharama (or any other "toys") kubwa kiasi hicho. Gari kama hiyo inamfaidisha mtu mmoja tu, wakati kwa pesa hiyo hiyo unaweza ukajenga shule ambayo itafanya watu wapate maarifa/elimu, waalimu wapate ajira, na mwekezaji apate faida. Gari kama Hummer haileti pesa, bali inakula pesa ktk mafuta na vipuri. May be I don't know how it feels like to be a star....


Mkuu Kila mtu ana mipango yake...na mawazo yake duniani....huwezi mpangia mtu afanye nini na awaze nini...au kwa kuwa ni dotnata...mbona husema watu wanao kunywa pombe kuwa pesa hizo wengeweza save na kujenga shule,clinic etc wewe hapo una TV nyumbani...kwanini usinge peleka kwenye vituo vya yatima pesa hiyo?Eish watu kwa kushadadia pesa za wengine na kuzipangia matumizi kujifanya wana akili sana duuu...kashasema anafanyia biashara wewe usha conclude kuwa gari inakula pesa sio kuingiza pesa...enda uko daradala?

huyu si anapamba harusi na kucheza filamu?Huoni kuwa kweney sherehe anaweza chukua sherehe nzima na gari la wahusika wakuu likawa hammer lake?Hukuhusishwa kwenye mipango yake then tulia mkuu.
 
Mh! jamani msimshambulie sana ndiyo ubongo ulipofikia kutuletea habari kama hiii. Unakuta familia za watu wanakufa njaa wewe unafanya ubishoo ili watu wakujue. Ila kwa mdada sidhani kama ana ubavu huo na kama anao na amenunua mashauzi hayo. Glory be to God. Mungu amuondelee uvivu wa kufikiri maana Hammer is nothing compared to the life we have.

P

Caroline Danzi - Hata wewe? kweli unasema Dotnata kaaza biashara ya mapambo kitambo sana...na kuandaa dhifa mbali mbali kitambo sana..zaidi ya 5yrs..yuko kwenye biashara..kwanini asiweze?kwanin wewe unakataa kuwa dada hawezi...mbona anaweza kuimba anaweza kuandaaaa sherehe kwanini asiweze...ana matatizo yake...na penye sifa apewe though habari imetoka kwenye gazeti la amani na ameeleza malengo yake...hata akilitumia kwa matanuzi ni yeye...Do you have problem with that?
 
Kama tatizo ni la mwandishi kupamba habari kishamba, mumlaumu mwandishi, lakini kama mtu ameinvest hela yake akaanzisha/endeleza biashara yake nyie inawashangaza au inawauma nini?

Kama wewe tajiri sana, unamdharauje masikini? au kama wewe huna unaona ubaya gani mwenzio akiwa nacho?
Au mlitaka awaombe ushauri humu JF?
 
......Watanzania hao, Serikali ikinunua Mashangingi ya Bei mbaya wanachonga, Mtu binafsi akinunua Gari lake la kutembelea binafsi pia wanachonga, na amesema wazi ni kwa ajili ya matumizi ya Biashara zake. eeeeeeeehh. HAIHUU Jamani
 
Kwahiyo akinunua Hummer! Ndio Tunafanyaje?
Angenunua Escalede au Cadillac ingekuwa vipi? Nadhani ingekwa zaidi ya matangazo na habari wasanii wa kibongo wanapenda sifa za KIJINGA vitu vidogo tu Matangazo kila mtu ajue Gari kama hiyo sasa hivi Saudia ni Taxi

Kama nilivyoona hili ni tangazo la biashara maana amesema atakuwa analikodisha katika sherehe za kitaifa na kimataifa. Hakuna tatizo mtu kutangza biashara yake. Mimi nitakodi siku ya arusi yangu ya mke wa sita.
 
Iwe used iwe mpya haihusu mlioponda mmesahau km huyu ni mama wa decoration na catering services km atakupambia kumbi na chakula akaleta kuna ubaya gani kukukodishia usafiri?me nampa big up sana anapanua biashara yake khs kujenga shule sijui hospital pesa ni yake ndo muamuz aifanyie biashara gani ni mtazamo wangu
 
yaani huyu naye ni maarufu, mbona mimi simfahamu? na kama amenunua hiyo gari so what? kwa pesa gani? kuna watu wana mabilioni na mabilioni lakini hawanunui takataka kama hiyo, wanajenga nyumba, nyumba nyingi zingine hadi wanatunzia yatima, wengine wanalipia watoto yatima na wasiokuwa na uwezo ada za shule...sasa yeye kama ndo hivi, and so what? aende zake na pesa za mawazo hizo...gari kama hiyo si itachoka muda si mrefu, atakuwa amefaidika ni kutuzidi sisi wengine wenye magari ya kawaida tu? na tunafanya tangible things kibao kwa jamii?
 
msanii matawi ya juu katika tasnia ya filamu bongo, husna mohamed posh ‘dotnata’ amefanya kufuru baada ya kutoa ‘burungutu’ kununua‘mkoko’ wa kifahari aina ya hummer, amani jipya limeinyaka.

Akizungumza na gazeti hili muda mfupi baada ya kukamilisha taratibu mbalimbali za kuukomboa mkoko huo kutoka katika bandari ya dar es salaam, dotnata alisema kuwa ametumia kiasi cha shilingi za kibongo milioni 270 kununua ‘mchuma’ huo kutoka katika tawi la kiwanda cha magari hayo huko detroit, nchini marekani.

“kila mtu atasema lake lakini ni kweli nimenunua gari hili kutoka marekani na nimetumia kiasi cha shilingi milioni 270 mpaka linafika hapa,” alisema dotnata.

white%20h2%20white%20rims.jpg

akiendelea zaidi, msanii huyo mwenye heshima kubwa ndani ya tasnia ya filamu za kibongo alianika kuwa watu wasimuelewe vibaya kwa kununua gari hilo amefanya hivyo akiwa na lengo la kulikodisha kwenye kwenye sherehe mbalimbali za kitaifa na kimataifa ili kupunguza makali ya maisha na siyo kutanua nalo kwa matanuzi yasiyo na lazima.

“leo natarajia kukamilisha usajili hivyo mwishoni mwa wiki hii litakuwa barabarani lakini sitalitumuia kwa matanuzi kama ambavyo watu wanaweza kufikiria, nimepanga kulikodisha kwenye sherehe na hafla mbalimbali za kitaifa na kimataifa ili linisaidie kujikwamua, ” alimaliza dotnata

dotnata+3.jpg


so what?
 
Back
Top Bottom