Dr. Biteko anastahili kupewa nafasi yakuongoza nchi; ana hofu ya Mungu na anaheshimu mawazo, utu na maoni ya wasiompenda na wanaompenda

Resilience

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2023
Posts
1,096
Reaction score
4,948
Katika siasa za Tanzania Dr. Biteko na Majaliwa wanayo nafasi kubwa yakuongoza nchi yetu. Ni viongozi wanaoamini kwenye mabadilishano ya hoja, mabadiliko na mchuano wa fikra.

Wote wana mapungufu yakibinadamu lakini wana mengi mazuri kuliko mabaya. Mwenyenzi Mungu awaepushe na tamaaaaa
 
ARE YOU THOSE ARE THE TRUE COLOURS OF HIM? PEOPLE SPEAK AT PEOPLE NOT TO PEOPLE
 
Mtasababisha wampe sumu bure
 
Hofu ya Mungu ndio upuuzi gani kwenye uongozi wa taifa. Wapi ulisikia Churchill, Washington, Mandela, Anwar Saddat, Deng Xiaoping au kiongozi mwingine aliyefanya makubwa anasifiwa kuwa na hofu ya Mungu.

Hofu yake ya kuchomwa moto wa milele sisi inatuhusu nini? Kwani atheists kina Kiranga hawaruhusiwi kugombea?
 
Too sad hawatopewa nafasi hizo, why? Chama walichopo hakina falsafa hizo
 
Wananchi tunamwamini Mungu hivyo tunahitaji kiongozi wa imani yetu.

Katafute nchi yako isiyoamini katika Mungu.

In GOD WE TRUST
 
Sahihi, kama nchi hatuchagui mchungaji, padri au imamu kuwa kiongozi wetu. Sisi hata kama akiwa mpagani au atheist kama sio fisadi na mpindisha haki anatufaa sana.
Mwenyenzi Mungu amekataza kuua, hawa watu wawili wanaweza kupambana na mauaji ya watu wanaodai haki
 
Kama siyo kigezo jiulize kwanini kila kiongozi lazima aape?
Ni mojawapo ya mambo yasiyo na mashiko tuliyorithi kutoka kwa wakoloni wetu Wazungu, lakini pia niliwahi kumsikia Nyerere akisema kuapa sio lazima iwe kwa vitabu vya kidini, hata kuapa kwa Katiba kwa wasioamini Mungu inafaa.
 
Ngoja tumu assess kwanza mama msituchanganye...
 
Thibitisha maneno yako kwa mifano..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…