Dr. Elly: Siyo kila mtu anatakiwa avae maski bali wanaohudumia wagonjwa na wanaohisi wameathirika

Dr. Elly: Siyo kila mtu anatakiwa avae maski bali wanaohudumia wagonjwa na wanaohisi wameathirika

Asante kwa hii, kiukweli elimu kuhusu Corona na jinsi ya kujinginga inahitajika sana!

P
Dah...tatizo mambo ya kitaalaam yanatolewa na wanasiasa....
Kuna tofauti kubwa sana kati ya kusambaza na kuambukiza... Bado elimu kubwa inahitajika...kwanini tuvae mask...tunawe mikono...tutumie sanitaiza...

Sent using Beretta ARX 160
 
Nimecheka sana bwashee!
Ha haaaa,niko kanda pendwa huku mkuu. Ila tujitahidi kupaza taarifa kwa wananchi.

Nadhani moja ya madhara ya kuvigeuza vyombo vya habari kuwa vituo vya propaganda za serikali ni hili.
Siku hizi watu hawaangalii tena hata taarifa za habari sababu wanajua watakutana na flai ova, standadi geji, mandege, tumbua/teua nk.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mpaka watangazaji kwenye tv wamevaa mask, habari hazisikilizwi Bali tunaangalia mask zao. Studio kwa nini zisipulizwe dawa? Ulimbukeni?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mjadala wa jinsi ya kujikinga na virusi vya Corona unaendelea muda katika luninga ya Channel Ten.

Mtaalamu Dr Elly Josephat kutoka MAT anasema kuvaa maski kwa mujibu wa maagizo ya WHO ni kwa wale wanaohudumia waathirika na wale wanajishuku au kuhisi kuwa wameathirika.

Na kuna jinsi ya kuvaa hizi maski, kama wewe unamhudumia muathirika ule upande wenye rangi ya blue ambao ndio una dawa unakuwa nje na kama wewe ni muathirika upande wenye rangi ya blue unakuwa ndani ili pumzi au sauti inapotoka tu inakutana na dawa kinga.

Source: Channel Ten
Mi kinachonikera ni watu kuvaa kidevuni, mfano Mbatia jana, alivyokua anaongea na waandishi wa habari, huku amevaa kidevuni, huo ni ulimbukeni tu, ni kama dr kumkuta nje au kwenye studio akihojiwa huku ametundika stethoscope mabegani.
Mbona hawatembei na syringe kwenye corido za hospitali!

Pia kwenye ishu ya corona, kumzuia mtu kuvaa mask hata kama ni kitambaa kuziba pua na mdomo, huku una msisitiza akipiga chafya ajizipe mdomo kwa kitambaa kuepusha kusambaza vijidudu ni kujichanganya, ni bora kusisitiza kuvaa mask kuliko kuwakataza.
 
Mi kinachonikera ni watu kuvaa kidevuni, mfano Mbatia jana, alivyokua anaongea na waandishi wa habari, huku amevaa kidevuni, huo ni ulimbukeni tu, ni kama dr kumkuta nje au kwenye studio akihojiwa huku ametundika stethoscope mabegani.
Mbona hawatembei na syringe kwenye corido za hospitali!

Pia kwenye ishu ya corona, kumzuia mtu kuvaa mask hata kama ni kitambaa kuziba pua na mdomo, huku una msisitiza akipiga chafya ajizipe mdomo kwa kitambaa kuepusha kusambaza vijidudu ni kujichanganya, ni bora kusisitiza kuvaa mask kuliko kuwakataza.
Bwashee hujakatazwa kuvaa maski!
 
Back
Top Bottom