Dr. Hildebrand Shayo

Kitila huwaga unanifurahisha sana...hupendi ubishi wala ugomvi....

Unabishana vipi na mtu ambaye tayari amesha-make conclusion hata kabla hamjaanza mjadala. Halafu utabishanaje na watu ambao hawawezi kutofautisha kati ya public opinion iliyoandikwa kwenye blog na magazeti na academic articles ambazo kawaida huandikiwa kwenye academic journals. Hapo inabidi unyoshe mikono juu; mwishowe tutaanza malumbano na matusi...
 
Bado natafuta academic articles za Profs na Drs wa udsm kwenye website yao……….ni masaa sasa
 
Kitila Mkumbo,

..lugha uliyoitumia hapo mwanzo haikuwa nzuri. nadhani ndiyo sababu kuna wachangiaji wameshindwa kuelewa hoja uliyokuwa ukijenga.

..article walizoandika Dr.Shayo na John Mashaka baadhi ya walengwa wake ni "mangumbaru" kama wakina jokaKuu. sidhani kama kuna mchangiaji yeyote mwenye mawazo kwamba article zile zinaweza kuchapishwa ktk academic journals.

..sasa tukiacha suala hilo hapo juu, ambalo liko wazi kabisa, kinachonishangaza ni negative comments zinazoelekezwa kwa hawa vijana. yaani kila kijana anayeonekana kuchomoza kidogo basi anarushiwa maneno, anachimbwa, ilimradi aonekani hafai.
 

*******************************************************************
Hili ni tatizo (hiyo kwenye bold). Ndiyo maana ukisoma huko nyuma kuna post nimekemea vikali kitendo cha kushuku na kuhoji usomi wa Dr Shayo kwa sababu tu alikosea lugha, tena grammar. Huo ndio nauita ushamba na ushambenga.

Lakini pia ni ushamba, ujinga na ushambenga kushuku, kuhoji na kudharau usomi wa watu wengine kwa sababu tu hawajaandika makala kwenye magazeti au kwenye blog za akina Michuzi, JF na zingine. Kuna njia nyingi sana za ku-disseminate information. Pengine bado tunavuna uathirika wa ukiritimba wa miaka mingi
.
 

My bad for making such a conclusion...mimi ni mwanataaluma kama wewe,na kwa ufahamu wangu sidhani kama kuna tatizo ku-publish an academic paper kwenye blog katika zama hizi ambazo dunia inaunganishwa na nyenzo za teknohama kama blogu na majukwaa ya mawazo (eg JF).Let's be honest,Mr Kitila,hivi kama una paper flani muhimu kwa jamii (lakini ni ya kitaaluma)hufikirii kwamba kuiweka kwenye blog au JF inaweza kuwa na manufaa makubwa zaidi kuliko ukiicha huko JSTOR,kwa mfano,ambako consumers wake wakuu watakuwa wanataaluma wenzako pekee?

Academic articles sio state secrets ambazo zikiwekwa kwenye public domain zita-compromise usalama wa nchi.Nakubaliana nawe kuwa academic journals zipo kwa ajili ya academic publications lakini what if unahitaji kuifikia wider audiance?Let's be honest again,hivi academic publication itakuwa more widely accessible katika tovuti ya REPOA,kwa mfano (ambayo si ajabu ikawa updated once in a month) au JF au Michuzi Blog ambako kuna hits makumi ya maelfu kwa siku?

Tofauti za kimtazamo haziwezi kupelekea matusi kwa vile lengo letu hapa ni kubadilishana experiences.Kama mwanataaluma,naamini kwamba mtindo wa baadhi ya wanataaluma kuamini kwamba academic journals ndiko mahala pekee pa kuweka mabandiko ya tafiti zao,kwa mfano,sio sahihi.Chapisho la kitaaluma litakuwa na manufaa zaidi kama litaweza kuufikia umma mkubwa zaidi,na wewe na mie tunajua kwamba academic journals zimekuwa kama sehemu za wateule wachache (i.e. wanataaluma na pengine wanahabari wanaotafuta references flani).

Naomba kutoafikiana nawe kwamba sikuweza kutofautisha public opinion iloandikwa kwenye blog au magazetini na academic paper ambazo MARA NYINGI (LAKINI SI MARA ZOTE) huandikwa kwenye academic journal.Nachoelewa ni kwamba wakati public opinion inaweza kuwa disqualified kuchapishwa kwenye academic journal,academic article inaweza kabisa kuchapishwa kwenye blog au gazeti.By the way,academic articles zinaweza kuwa nyenzo nzuri za ku-shape public opinion if published in public domains badala ya kuzihifadhi tu kwenye mafaili,removable media,etc.Kama matokeo ya tafiti zetu au mawazo yetu ya kitaaluma yataendelea kuwa limited kwa kikundi flani,ni dhahiri kuwa jamii itatutafsiri tofauti hata kama matokeo ya tafiti hizo yatakuwa na impact kwa jamii husika baada ya muda flani.

Nimalizie kwa kutoa wito kwa wanataaluma,hususan wa Kitanzania,kuitumia ipasavyo teknohama ili kutowatenga wenzetu ambao kwa sababu moja au nyingine hawana access na machapisho ya kitaaluma.Miongoni mwa faida za kufanya hivyo ni kuleta suluhu katika hoja zinazohitaji uthibitisho au ushahidi uliofanyiwa utafiti.Machapisho ya kitaaluma yataendelea kuwa ya manufaa makubwa kwa wanataaluma lakini nyenzo za mawasiliano kama blogu (mfano ya Michuzi na nyinginezo) na kumbi za mijadala (eg JF) pia ni mahala mwafaka pa kuelimisha,kukosoa na kuhabarisha kuhusu masuala mbalimbali yaliyotafitiwa kitaaluma.

Naweza kuwa siko sahihi lakini huo ndio mtizamo wangu.Na pia tunaweza kabisa kulumbana pasipo kuishia kwenye matusi kwani we could always agree to disagree if we wanted to.
 
Wanaotetea utumbo anaoandika 'Dr.' Shayo siwaelewi.
Being a 'Dr.' at South Bank is no big deal, dont test our intelligence.
Kuna vichwa vya kiTanzania viko downlow kwenye mambo kama ya uchumi na hawaongeii wala ku-type uncoordinated articles. Articles za maana zinakwenda kwenye journals, na kuna watu wengine hawana time ya kuandika articles. If you can find an article by 'Dr.' Shayo in a reputable international journal, then we can start rating him among 'vichwa'. And am not talking about articles on african development, diseases n usual malachy stuff, talk about economic issues.
Kama 'Dr.' Shayo ndio representation ya 'Vichwa' vya kiTanzania, then God save Tanzania and someone shoot me please, cos the future dont look bright at all as he seems to be taking quite a few people for a ride.
Everytime I read his articles I feel ashamed as a Tanzanian, cos that stuff is embarrasing. Imagine someone googling about Tanzania, bump into his article....and they read about a 'reputable Dr.' apparently.......ooooh shitesss........dudes need to go back to the blackboard!!

Halafu inabidi aache kujifanya ni specialist katika kila field; i.e uchumi, michezo, energy n.k. Ukisoma articles zake unajua kitu gani kaandika yeye, na kitu gani ameplagiarise. You can tell from the way the sentences dont connect.

Dude, go back to the drawing board and re-do your 'PhD'.
 

Mhh...Kama Mtanzania kuwa lecturer wa university ya nchi ya dunia ya kwanza sio big deal,then labda neno big deal lina tafsiri nyingine.Mzee hebu cheki hizi links chache hapo chini labda zinaweza kusaidia kukupa opinion tofauti na hiyo hapo juu.Pia ni vema tunapokosoa MADUDU tukayaweka hadharani (kuyanukuu).

http://www.lsbu.ac.uk/esbe/property-surveying-construction/ICBERG.shtml]ICBERG - Dept. Property, Surveying & Construction

http://www.commissionforafrica.org/english/consultation/submissions/ro/sb-nov-dec04-204.pdf

http://www.amazon.co.uk/Economic-Benefits-Employing-Previously-Unemployed/dp/095510212X]Amazon.co.uk: Economic Benefits of Training and Employing Previously Unemployed Local People: A Joint Project with Bovis Lend Lease: Hildebrand Shayo, John Hampson: Books

http://www.amazon.co.uk/exec/obidos/search-handle-url/279-1798635-0916741?_encoding=UTF8&search-type=ss&index=books-uk&field-author=Hildebrand%20Shayo]Amazon.co.uk: Hildebrand Shayo: Books

http://www.rics.org/NR/rdonlyres/982F8BB5-1949-4C7F-9969-A8FE66FAD7AF/0/Volume6Number5lowres.pdf
 
Kwa mtoto wa mkiulima aliyesomea kijijini na kufikia level yake ya Dr hata kama wengine mnamuona hafahamu grammar ni kuwa amejitahidi tena sana. Je, vipi wale watoto wa vigogo walipata nafasi za kwenda majuukwa sababu ya nyadhifa za wazazi wao wakaishia tu kufahamu kingereza, hasa speaking english lakini kichwani hakuna substance tusemeje????? Mifano hai tunayo wa watoto wa jinsi hiyo ambao wameishia kuwa walaunga tu!!!??? Kwa huyu Dr. Shayo namsifu sana kwa hatua aliyofikia. Halafu ndugu zanguni we learn through mistakes!!!!! Nikipitia uandishi wa kimombo changu miaka kumi iliyopita na sasa there is some improvement na hii ni kwa sababu English is mya third language kama ilivyo English kwa Wapan, Wakorea, Wachina, Wamalay na wengine tunaofahamu kuwa English is option.

Ukweli utabaki kuwa Dr. Shayo amefanikiwa kwa umri pia alioweza kupata PhD yake ni mdogo. Je kuna Suypervisor wake wa PhD amelalamika kuwa mwnafunzi wake alikuwa kilaza??? To me nimeona kuwa kuna ugomvi fulani katia ya aliyepost na huyo huyo ana members hapa wanafahamiana so they are teaming up to fire against Dr. Shayo.

Tujitahidi kuwa objective tunapojadili private achievement/life ya watu. Kwenye ukeli mpeni ukweli si kumkandia kwa kila kitu. Then mnathubutu kuweka hata confidential numbers za documents zake like passport, membership cards, etc.

Nimepitia google search ya taarifa zake mimi nimefurahishwa na efforts zake, amejitahidi kufanya kazi nyingi. Je tujiulize wengi nikiwemo mimi, je tukisearch taarifa zetu kwenye mitandao tuna mchango wowote constructive???? Kama upo ni kwa wachache wetu tu. Sasa inakuwake tunainuka kumpiga vita mwenzetu only tu kwa kuwa grammar imekuwa poor. How about the substance in his arcticles???? Unataka kuniambia u can not use his articles for references when required to do so???? Wengi au jamaa na marafiki zako wanatumia articles zake inluding both his Phd and Masters Thesis!!!!

Ukweli ni kwamba hata kama mtaleta andiko langu binafsi hapa eti mnachambua kiingereza changu ni kwamba nitaona kawaida tu kuwa watu wamekosa kazi ya maana kuchambua grammar ya kiingereza changu ambacho nilifundishwa na waalimu wa UPE. Kosoa education system ya Tanzania and not me. Wale ambao mmesoma nje au mlikwenda huko nje na wazazi wenu na mkaamua kubaki huko hata baada ya contract za wazazi wenu kumalizika na pengine tayari mmeshaoa au kuolewa huko ni bahati yenu. For sure hata watoto wa Dr. Shayo watakuwa na good command of English kuliko wazazi wao kwani mtoto ni mwepesi sana kukamata lugha. Wengi ambao watoto wenu walizauliwa ughaibuni au uliondoka huku wakiwa wadogo then utakubaliana nami.

Kwa upande wangu mpaka leo najifunza kimombo na kiswahili fahaha kwani lugha yangu ya kwanza ilikuwa ni kilugha!!!! So at this point nisipopata grammar ya kimombo na kiswahili nitadharaulika??? Please, no do not do so?????!!!!! All the best and keep up Dr. Shayo. Nafahamu Dr. Shayo aweza kuwa member na ameona jinsi ametupiwa makombora au pia marafiki zake wameshamtaarifu juu ya private affairs zake na academic kuanikwa hapa. Songa mbele mpiganaji, usiogope Jf wale waliokupiga vita, endelea kuimarisha kimombo chako na kwa kuwa umebahatika kufanya kazi hapo UK naamini grammar itanyooka tu. Fahamu katika dunia usitegemee kuwa kila mtu anafurahia maendeleao yako, jua kuna adui na rafiki, mpenda maendeleo na mpinga maendeo. Songa mbele mtanzania mwenzetu. Hata post hii sija edit ila naamini umepata substance!!!!!!
 
Dude,
You are trying your best lakini, tunajua hizi shule zinavyo-operate. Internal report, sio international report. Work on your links too.

Good University Guide

Na issue sio english wala nini, issue ni kwamba sentence zake huwa haziconnect. Kinachoandikwa katika sentensi moja, kwenda nyingine (within same paragraph) is not the same source.

Just slow your roll.
 
NZOKANHYILU, are you suggesting,kwamba most probably the 'Internal Report' would not make a good reading as a result of various flaws appearing now and then in his presentations?
 
NZOKANHYILU, are you suggesting,kwamba most probably the 'Internal Report' would not make a good reading as a result of various flaws appearing now and then in his presentations?

On the contrary. It can make great reading indeed. Infact katika vitu vya papers na reports, lazima upitishe kwa watu wengine wasome na wasahihishe. No one is perfect. Hata maprofesa wanashare articles zao na critics wao, kabla haijawa published.
Infact, mimi sim-doubt kwamba jamaa sio intelligent. Nadhani ishu hapa hiyo PhD vipi? Na swali la PhD linakuja kutoka na utumbo anaoandika online.
Haya, kaja mpambe hapa analeta link za articles.
Nimeweka link ya University Guides hapo. South Bank ni Uni ndogo sana, ilikuwa ni college within the last 10-15years. Uni kama hizi mara nyingi zinapasisha watu ili ranking zao zipande na wapate funds. Standard za acceptance ziko chini sana. Mara nyingi walimu hawako madarasani wanafanya miradi yao ya Tuition au miradi ya nguruwe.

Kama kweli mna mrank as a 'kichwa' academic, then I feel sorry for the state of Tanzania, and you are really taking the piss on real wasomi around the world (waKitanzania) ambao wametulia tuuuu. Angekuwa red-brick university na akatoa utumbo kama huo ningeshangaa sana. Lakini PhD alipopata, na utumbo anaoandika, havinishangazi. Nadhani ndio basis ya swali la GT.

You can hate this opinion, hate me or whattever, but the dude is passing out as a 'Tanzanian academic', now, that I dont and wont accept so long I come across those crappy articles!!

What he writes, is a reflection of his education level and as a result his educational title he fluffs about gets questioned.
 

Basis ya swali la GT,ni whether PhD ya Shayo ni authentic au ni kama ya kina Mponjoli.Hilo limeshajibiwa.Tatizo sio kama jibu hilo halitoshelezi,bali halikidhi matakwa ya haters wa academic achievement.

Hebu tuwekee basi huo UTUMBO kisha utuonyeshe namna wewe mwanazuoni ungeweza kuandika kilicho bora.Ni rahisi kuropoka hapa kwamba alichaondika flani ni utumbo ilhali kuandika kitu bora kuhusu maisha yako mwenyewe ni mgogoro.By the way,ungeweza kutupa kitu kikali sana kutokana na data ulizo kuwa UNASAKA HAPA

End of the day,Dr Shayo will always be referred to as Dr Shayo,and haters mtaendelea kuumia na kukosoa (pengine huku mki-wish nanyi siku moja katika maisha yenu mngepanda kibandiko kama hicho cha u-DR lakini it's too late now) but you cant change anything.

Simjiu Shayo personally lakini najua nini maana ya PhD,naimesoma baadhi ya machapisho yake ya kitaaluma,na nimeikubali kazi yake.Do you have to?It's up to you.Conclusion uloweka HAPA inatosha kabisa kueleza mantiki ya hoja zako.
 

Poa. Sijaclaim kuwa academic.
Mimi ni kijana kwa Dr. Shayo. Nikitaka PhD kwenye top-tier university napata. Na hapa naongelea top 5. Sijawahi kuandika article, kwasababu kwa background yangu, sio financially interesting. Nikitaka kuwa charterted, hayo mambo yana matter. Ila field yangu experience counts more that papers you write.
But I have the right to point a crappy article when I see one.
 

Nzokanhyilu,

Come on, not everything is about money. Counting more does not stop you from sharing novel and useful stuff that you have discovered. What a lame excuse, that is? You can also fix your english Umefundisha at a top-tier University with a Bachelor degree at what capacity?
 

mlinzi wa getini.
mimi mhandisi, english least of my worries. but i know a crap article when i see one. And if I had to write something on Prof. Ndulu, I will do the right thing and ask someone to double check it for me, au proof read. Hii kitu ni common hata maofisini tunafanya ukiandika external report.
Pamoja na english mbovu nimefundisha wahandisi madingi wenye experience ya miaka 10 kuendelea. We umeshakaa darasani, kijana mweusi, mbele ya wazungu wazee wanakuangalia 'huyu kijana mweusi atanifundisha nini?', baada ya hapo wanakubali?

Get it into your head. I dont doubt 'Dr.' Shayo's intelligence, what I doubt is the quality of that PhD, plus the crap that he writes. English is my 4th language, and om on my 5th and 6th soon. So long I communicate as an Engineer, am happy. Nikiandika article, it will get proof read (correct this sentence, and sample that).

Na nani alikwambia sijawahi kujibu article za Dr Shayo?
 

Najua namna academicians wanavyokosoana....a lecturer (former or current) from a top tier uni atapom-criticize lecturer mwenzie anatarajiwa kuja na thematical or theoretical arguements rather than analysis ya personal character or attributes.Kumbuka,great minds discuss iDEAS,average minds discuss events,and small minds discuss people.Hence it goes without saying kwamba central theme ya criticism yako,a (former/current) top-tier lecturer,ingekuwa kwenye issues zilizokuwa addressed na Dr Shayo katika article yake na hayo ya madudu ya lugha yangekuwa secondary.

By the way,top-tier university inayoajiri bachelor graduates kufundisha lazima itakuwa na matatizo binafsi.Anyway,labda iwe kufundisha in the sense of a tutorial assistant!But even that wouldnt make sense kwa a Bachelor degree holder kufundisha Bachelor degree students.Hiyo haihitaji research.I doubt kama Cambridge,Oxford,Imperial College,LSE au St Andrews (ndio top 5 hizo) wanakabiliwa na shortage ya staffs kiasi cha kuajiri Bachelor holders wenye experience but lacking Masters or PhD!Hata Mlimani (UDSM) hawa-entertain MADUDU ya aina hiyo regardless ya acute shortage of staff.

Bottom line is,just like you excercise your constitutional right to criticise crappy papers so does Dr Shayo,who's excercising his academic obligation to air his academic views based on HIS ACADEMIC QUALIFICATIONS and not mere EXPERIENCE!

PS....
Sijawahi kuandika article, kwasababu kwa background yangu, sio financially interesting
....Kwani siku hizi ukiweka bandiko kwa Michuzi au JF kuna malipo.Uandishi ni sehemu ya usomi,na visingizio vya backgrounds au financial interests do surely not hold water.Hivi kuna background isiyohitaji machapisho?Ulifundisha top-tier university,and that would definitely involve publication of some sort.....Finally,could yo do us "wapambe wa Dr Shayo" a little favour by pin-pointing madudu yaliyomo kwenye article unayoizungumzia (I have no idea which one you've been referring to)?
 

Poa. Kalagabaho. But his articles are crap. I am happy not to write articles. When I write I will holla you.

Hivi kwanza PhD thesis yake inahusu nini?
Anyways, napoteza muda kujadili kitu hakina maendeleo kwangu.
But he is not academic. Trust me, kuna academics waKiTanzania katika shule za maana. Fanya research utakutana nao. Kaa chini, fanya research.
 

Hoja hujibiwa na hoja.You are talking about HIS ARTICLES,nimekuomba kwa heshima na taadhima utupe reference ya article unayoizungumzia,umekwepa.Najua tatizo sio kwamba huwezi kuipata,bali ukiipata utashindwa kuthibitisha madai yako KISOMI.

May be true,he might not be academic to you but remains academician to those who value what he does.

I know kwamba kuna "academics" wa Kitanzania katika shule za maana,na pengine hiyo ilisaidia kwa mwenzetu kukubaliwa kufundisha a top-tier university na Bachelor yako!

You talking of research couldn't get funnier...Mwenyekiti Mao alisema no research,no right to speak.Unanishauri nikae chini kufanya research (actually ninamalizia moja hivi sasa out of a couple I have managed to do) ilhali wewe unashindwa ku-substantiate arguements zako kwa kuweka reference ya articles unazozungumzia!!!?Just quote japo sehemu ndogo tu ya said article,onyesha madudu uliyoyaona,kisha tupatie kilicho bora!Nadhani hivyo ndivyo mlivyokuwa mnafanya (au bado mnafanya) hapo kwenye top-tier university when it comes to criticising a paper or an arguement!

Much literary criticism comes from people for whom extreme specialization is a cover for either grave cerebral inadequacy or terminal laziness, the latter being a much cherished aspect of academic freedom- John Kenneth Galbraith

One mustn't criticize other people on grounds where he can't stand perpendicular himself"-Mark Twain
 

Poa. Nimeshindwa. Kuna kitu muhimu zaidi nafanya hapa. Ila article zake mbofu. And if he is academic, basi ndio maana tunajifunza kusign contract Norway.
 
Mods mko wapi hapa. Yaani mnaachia mtu anapakwa matope na kuchafuliwa sifa yake namna hii? Mmeshindwa kazi ama?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…